wapenzii, naomba ushauri wenu. Nilifahamiana na dada x nilipokuw alikizoni tena ilikuwa kwa bahati tu, tukaachiana namba na kumbe kwa vile wote tulikuwa likizoni hatukuweza kukutana so kila moja akaendelea na safari yake. Tukawa na uhusiano mzuri wa kwa njia ya email na hivi pole pole kuanza kujuana, naye akawa ananielezakuhusu mchumbake ambaye kwa kweli inaonyesha hampendi tena. Sababu zilizomfanya asimpende tena ni kuwa akiwa Tanzania jamaa alikuwa na mshikaji mwingine kitu ambacho x alikitambua, achana na hilo, jamaa tayari anamtoto na yule mama mtoto bado anauhusiano naye, zaidi ya hayo huyo jamaa tayari amezaa na mdogo wake huyo mama mtoto wake, hayo yote x anayafahamu. Kwa kuongezea tu tofauti zao za kimadhehebu hazipokeleki katika familia zao. x alitokea kunipenda ghafla nami kwa kweli nampenda. X amemwambia jamaa kuhusu nia yake ya kuacha uhusiano naye lakini jamaa amekuwa akimtishia kumuua na ujiua mwenyewe, kadili yake y huyo jamaa ni mara kibao tu ameshachukua bunduki na kutaka kujilipua... nisiseme mengi kwani siwezi kuyasema yote, my issue is, huyu jamaa ameahidi kuja kumuua dada x na kisha kujiua mwenyewe, sasa bado yuko likizoni na mbioni kusafiri, je nifanye nini ili dada x asipoteze maisha? kingine dada x alishaanza kufanya mipango ya kuja kunitembelea kumbe jamaa kampiga mkwara na x hana nguvu tena, je nifanyeje ili kumotoa hofu x? zaidi ya hayo mimi na x bado hatufahamiani sana lakini tayari tuna nia kuoana kumbe kwa upande wangu naona tayari uhusianowake na jamaa yake ni kikwazo kikubwa kwangu, nifanyeje? Naomba ushauriwenu wadau!