Igombe fisherman
JF-Expert Member
- Apr 28, 2017
- 2,025
- 3,562
Kuna matatizo mengine huwa hatuombi hata mungu. Maana unaona kabisa kuwa hili hata yeye hatoliweza
Uongo mwingine bhana!!!mimi ilinitokea nilipewa mtihani mgumu kweli kweli chuoni sikujua naanzia wapi nikamwomba mungu nikasikia sauti inaniambia tizama ubaoni nikaona notisi za majibu yote ya maswali zimeandikwa ubaoni nikawa nanyanyua kichwa naangalia ubaoni nakopi kama ilivyo hadi msimamizi wa mitihani akawa ananikodolea macho ananishanga shangaa nikaibua na A KWENYE HILO SOMO
NILIPOMALIZA KUANDIKA YAKAFUTIKA YENYEWE
Coincidence ndio kitu gani?Ukiomba alafu kikatokea basi ni eidha juhudi zako au COINCIDENCE tu, hamna kingine hapo!
Mungu acha aitwe Mungu
Ipo hivi, nilienda kuchakata demu wangu kwao si nkajisahau bwana hadi mida ya jioni ambapo hiyo mida mama yake ndo huwa anarudi kutoka job( huyu mama ni mkali balaa yani kukutia kisu hashindwi).
Mara tukamuona mdogo mtu anakuja mbio oooh mama anakuja, hatujajiandaa kwa lolote Mara huyo tunamuona kwenye dirisha anapita ili aingie ndani dah hiyo siku nilidata aisee!
Kilichofanyika pale demu kanichukua mpaka chumbani kwa mama yake kwenya mabegi akatoa manguo akanambia lala juu ya mabegi halafu akafunika juu zile nguo halafu demu hakuondoka hapo akajifanya kama anatafuta nguo.
Mama mtu kaingia chumbani kwake kamkuta mtoto mtu kama anatafuta nguo kumbe mimi nipo kwa ndani basi wakasalimiana halafu mama mtu akaanza yani wewe mbona nguo umeharibu hivyo mtoto kajibu nilikuwa natafuta nguo yangu ila sijafanikiwa na ndo naendelea kuitafuta dadeq yani ndani humo nililia machozi kwa Mungu, yani niliomba kila sala na nkaapa uzinzi naacha.
Mara mtoto akaanza mama amekuja hapa mama flani amenambia ukija tu uende anakuita (sasa hapa sijui alikuwa anadanganya au ilikuwa ukweli maana sikufanikiwaga kumuuliza) mama yake kaanza yani si aje tu mimi nimechoka kipindi hicho wapo chumbani nkasema leo nafia humu Mara nasikia anabadilisha nguo anamwambia mtoto wake aah ngoja tu niende daah aisee sikuamini yani alovyoondoka tu demu kanichomoa kanitoa yani miguu inatetemeka balaa aisee Mungu huyu acheni aitwe Mungu
Mungu ni mwema kila saa japo sisi binadamu tunamtenda kila kukicha ila haachi kutuonesha ukuu wake
Huu Ni ushuhuda wangu Mimi ,Mimi ndie najua ukweli wake sio wewe .Wewe una uhuru kuukubali au kuukataa sababu Soo wa kwakoUongo mwingine bhana!!!
Miaka kadhaa nyuma nikiwa Safarini Kikazi kwenda Mwanza nikapitia Moro kwa Bi Mkubwa kumsabahi na kulala home kwa siku mbili tatu maana nilikuwa na Private Car.Kuna muda bwana unaweza ukabanwa na mambo magumu katika maisha, na ukashindwa njia zote hatimae ukaamua kumuomba Mungu moja kwa moja na akakujibu?
Mimi kuna matukio kadhaa aisee naamini moja kwa moja Mungu ndiye alinisaidia.
1. Kukingwa na mvua kubwa
Mnamo mwaka 2008 nilikuwa katika moja ya shughuli za utafutaji katika Kijiji kimoja kinaitwa MKANYAGENI huko Tanga. Tulikuwa katika mapori fulani huko tukichana mbao. Lakini siku mbele baadae nilianza kuumwa na homa kali Sana. Jamaa zangu wakaamua kuniruhusu na kurudi mjini ili nisije nikawafia kule.
Safari ilikuwa Ni ndefu na ni ya mguu, nilitembea kilomita kadhaa na hatimae nikashindwa kabisa kutembea kutokana na kuishiwa nguvu.
Nikiwa nimekaa chini sijui cha kufanya, angani ilitanda mvua moja kubwa Sana, dakika chache baadae ikaanza kunyesha. Pale nilipo hapakuwa na nyumba wala sehemu yoyote ya kujizuia na mvua.
Kiukweli niliamua kumwambia Mwenyezimungu kana kwamba naongea na mtu. Nikasema "Ewe Mwenyezimungu, nakuomba uizuie mvua hii mpaka ntakapofika mjini kwani Kama ikininyeshea hapa hakika sitoweza hata kutembea"
Basi mvua ile ilikata na nilijikongoja mpaka kufika pale MKANYAGENI majira ya saa 2 usiku tangu saa 10 jioni.
Nilipofika tuuuu, aisee mvua iliachiwa sijapata ona... Daaah nkasema kweli Mungu yupo.
2. Chakula cha hapo kwa hapo.
Mwaka 2015, siku moja nikiwa sina hata mia mbovu. Mipango yangu yote imepinda. Njaa inaniuma sijakula siku nzima mpaka nikafikia hatua ya kulegea kwa njaa.
Niliamua kumwambia Mungu nisaidie, nitakufa na hii njaa mimi mja wako.
Nilitoka kuelekea nisikokujua, lakini baada ya dakika kadhaa niliamua kurudi tu geto.
Aisee kitu cha kushangaza WALLAAHI nilimkuta mtoto wa jirani pale mlangoni kwangu akinisubiri na akiwa ameshika bakuli ya wali.. kwa kudai kuwa amepewa na mama yake aniletee... Nilishangaa Sana maana huyo mama wala Sina mazoea nae wala HAKUWA jirani wa karibu...
Nkasema kweli Mungu amejibu maombi. Asante sana Mungu.
3. Kuokoka ka kufumaniwa na mke wa mtu.
Hii ilikuwa ni mwaka 2017... Sitosahau.
Nikiwa ndani kwa mtu na mke wake.. Jamaa hakuwa mji ule kabisa alikuwa kikazi mji mwingine. Lakini hammad ghafla tukasikia sauti za honi ya gari getini ikimaanisha kuwa msela ameshafika.... Yule mama alikwenda kufungua geti nikiwa nimejificha nyuma ya friji nikisali maombi yote.
Mara mprado huo ndani mzee kaingia..
Daah kumbe alisahau simu mfuko wa mbole katika duka flan huko mjini, ikabidi awashe tena gari arudi kuchukua kwa ajili ya matumizi ya kesho.
Nafkiri mbio nilizotoka nazo pale Ni zaidi ya BOEING 787. Na ikawa mwisho wa kudate na Iile shuga mamy. Hakika mzee angenikamata Ningekufa tu.
Acheni wake za watu hata wakijirahisisha.
Ila jaman MUNGU ANAJIBU MAOMBI kwa aombae kwa dhati.
Amen, always God is good.Mungu acha aitwe Mungu
Ipo hivi, nilienda kuchakata demu wangu kwao si nkajisahau bwana hadi mida ya jioni ambapo hiyo mida mama yake ndo huwa anarudi kutoka job( huyu mama ni mkali balaa yani kukutia kisu hashindwi).
Mara tukamuona mdogo mtu anakuja mbio oooh mama anakuja, hatujajiandaa kwa lolote Mara huyo tunamuona kwenye dirisha anapita ili aingie ndani dah hiyo siku nilidata aisee!
Kilichofanyika pale demu kanichukua mpaka chumbani kwa mama yake kwenya mabegi akatoa manguo akanambia lala juu ya mabegi halafu akafunika juu zile nguo halafu demu hakuondoka hapo akajifanya kama anatafuta nguo.
Mama mtu kaingia chumbani kwake kamkuta mtoto mtu kama anatafuta nguo kumbe mimi nipo kwa ndani basi wakasalimiana halafu mama mtu akaanza yani wewe mbona nguo umeharibu hivyo mtoto kajibu nilikuwa natafuta nguo yangu ila sijafanikiwa na ndo naendelea kuitafuta dadeq yani ndani humo nililia machozi kwa Mungu, yani niliomba kila sala na nkaapa uzinzi naacha.
Mara mtoto akaanza mama amekuja hapa mama flani amenambia ukija tu uende anakuita (sasa hapa sijui alikuwa anadanganya au ilikuwa ukweli maana sikufanikiwaga kumuuliza) mama yake kaanza yani si aje tu mimi nimechoka kipindi hicho wapo chumbani nkasema leo nafia humu Mara nasikia anabadilisha nguo anamwambia mtoto wake aah ngoja tu niende daah aisee sikuamini yani alovyoondoka tu demu kanichomoa kanitoa yani miguu inatetemeka balaa aisee Mungu huyu acheni aitwe Mungu
Mungu ni mwema kila saa japo sisi binadamu tunamtenda kila kukicha ila haachi kutuonesha ukuu wake
Miaka kadhaa nyuma nikiwa Safarini Kikazi kwenda Mwanza nikapitia Moro kwa Bi Mkubwa kumsabahi na kulala home kwa siku mbili tatu maana nilikuwa na Private Car.
Kesho yake jioni Bi Mkubwa akanipeleka nje ya Mji kwenda kuangalia Shamba / Kiwanja ambacho nilikinunua Baadae.
Mara baada ya kumaliza kuangalia Shamba hamad Funguo za Gari sizioni,nilikuwa nimevaa Jeans yangu moja mfuko mmoja wa mbele kwa ndani ulikuwa umetoboka.
Sikukumbula niliweka mfuko gani ila nikahisi ntakuwa niliweka kwenye huo mfuko.
Tukaanza kutafuta kuanzia nilipo park Gari,Kumbuka giza lilishaingia na tuko Mashambani, Gari New Model,huwezi kuchonga funguo kiholela Mpaka uende through Manufacturer na kazini wanajua Mwanaume niko Safarini Mwanza.
Tafuta na kutafuta hamna kitu.
Bi Mkubwa akaanza ku Panic, Mzee mwenye Shamba ka Panic,anaogopa, Akaja kijana wake wa Maziwa kusaidia kutafuta, mimi Simu yangu charge imeisha hivyo torch imezimika.
Kijana akaja na torch.
Nikamwambia Mungu, wewe wajua hizi funguo nilipozidondosha, naomba uniongoze nizipate, nikamuweka Kijana Mbele na torch Mimi nyuma kwenda katika Manyasi nilipokuwa nakagua shamba, kufika katikati nikahisi nimeona kitu cheusi,akili ya mwanzo ikaniambia ni kinyesi cha Ng'ombe tu,nikapiga hatua kuendelea, lakini kuna kitu kikaniambia hebu rudi hatua moja nyuma uangalie vizuri.
Kurudi that was the Car Key
Lile tukio ni dogo ila liliiikuza sana Imani.
yangu juu ya uwezo wa Mungu.
Rest in Peace my Bi Mkubwa, Shamba nililonunua kwa ajili yako wala hukulifaidi
Ahsante MkuuPole sana mkuu... Apumzike kwa amani
Mmmh like serious?..hii ni zaidi ya miraclemimi ilinitokea nilipewa mtihani mgumu kweli kweli chuoni sikujua naanzia wapi nikamwomba mungu nikasikia sauti inaniambia tizama ubaoni nikaona notisi za majibu yote ya maswali zimeandikwa ubaoni nikawa nanyanyua kichwa naangalia ubaoni nakopi kama ilivyo hadi msimamizi wa mitihani akawa ananikodolea macho ananishanga shangaa nikaibua na A KWENYE HILO SOMO
NILIPOMALIZA KUANDIKA YAKAFUTIKA YENYEWE
Ubarikiwe kwa hili.Kumkufuru Mungu ni kujitafutia laana. Haujui ulitendalo. Mungu akusamehe.