Mambo ambayo Mungu hayapendi lakini Waislamu na Wakristu wamefichwa

LIKUD

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
15,111
27,096
Kabla sija enda kwenye mada nauliza hivi wewe ambae unawaachiaga siti wazee kwenye daladala tangu uanze kufanya hivyo ni mambo mangapi ambayo umeshafanyiwa wepesi kwenye maisha yako?

Tafakari! Chukua hatua! HAKI ELIMU.

Back to the point.

Yapo mambo ambayo kiuhalisia Mungu hayapendi ila wakristu na waislamu wamefichwa (nimewataja wakristu na waislamu kwa sababu hawa ndio wanaamini dini/imani zao ndio za ukweli kwamba wao ndio wanamjua sana Mungu kuliko watu wengine).

Jambo zuri (linalotoka kwa Mungu) huwa linatazamwa kwenye matokeo (results) na siyo vinginevyo.

Kama unafanya jambo lolote lile hata kama unaamini limeagizwa na Mungu lakini likawa linaleta matokeo hasi basi tafsiri yake ni kwamba Mwenyezi Mungu hapendezwi na jambo hilo.

Kwenye uzi huu nitataja baadhi ya mambo ambayo Mungu hayapendi lakini wakristu na waislamu wanadhan kwamba Mungu anayapenda.

Haya twende kazi;

1. Mungu hapendi nini? Mungu hapendi baba anae taka watoto wake wajifunze kuhusu neno lake( Bible/Qur'aan). Ndio maana baba anawapeleka watoto wake madrassa au Sunday school/mafundi kwa wakatoliki, mwisho wa siku watoto wanaishia kulawitiwa na kunajisiwa na mwalimu wa madrasa au katekista/Mchungaji. Tafsiri yake ni kwamba Mungu hapendi uwapeleke watoto wako madrassa au Sunday school.

2. Mungu hapendi nini? Mungu hapendi kijana wa kiume anae enda kwa heshima ukweni kumchumbia binti ili amuoe. Ndio maana ukienda kuchumbia KWANZA unaonekana fala.halafu pili unawekewa vikwazo ambavyo havina kichwa wala.

Miguu na usumbufu wa kutosha plus kurogwa juu. But kijana huyo huyo akiwa anakula demu huyo huyo kimasihara mambo huwa fresh kabisa na demu huyo anapo pata ujauzito na kujifungua wazazi humtaka binti huyo aende kuishi kwa baba wa mtoto bure kabisa bila mahari yoyote na vitu vya kuanzia maisha juu.

3. Mungu hapendi nini? Mungu hapendi wanadamu waingie katika ndoa. Ndio maana asilimia kubwa ya ndoa ni matatizo matupu. Talaka ni nyingi kupita maelezo na walioko ndani ya ndoa wanatamani kutoka.

4. Mungu hapendi nini? Mungu hapendi mwanaume ambae anampenda sana mkewe anamjali sana mkewe na watoto na anajitoa sana kutunza familia.

Ndio maana wanaume wa hivyo huwa wanaishia kuwa disappointed na wake zao. Mke hucheat, mke huwafundisha watoto kumchukia baba yao/ watoto huharibikiwa, mume kutangulizwa ili mke abaki na mali n.k.

6. Mungu hapendi nini? Mungu hapendi mtu anae sema ukweli ndio maana msema.ukweli huchukiwa na watu na mara nyingi huuliwa KWA sababu ya kusema na kusimamia ukweli.

7. Mungu hapendi nini? Mungu hapendi mtu anae swali mara tano au anaesali sana (mkristu), ndio maana wanao swali mara tano au wanao sali sana ( walokole) kila.siku wanalalamika kusumbuliwa na matatizo ya kiroho kama vile uchawi, majini, vifungo vya kichawi n.k.

Mifano ni mingi sana.

Suluhisho: Just enjoy ur life
 
Hii bangi ni kiporo, umebangukwa kisawa sawa

Shindana na hoja mkuu usishindane na.mtoa hoja. Unless otherwise FANYA kama unapita kushoto hivi..ni nuksi kwenda sehemu ambayo uwepo wako hauhitajiki.


Najua una akili nyingi sana mkuu, lakini akili zako nyingi hazihitajiki kwenye uzi huu.

Siku nikipost uzi unao hitaji mtu mwenye akili nyingi kama wewe nita kutag.

Vunga.
 
Wewe ni ndugu au mtoto wa shetani mwenyewe siyo? Nadhani huna unachotafuta hapa zaidi ya kiki mwanangu. Ulaaniwe milele na milele
Nakupa dakika tano futa hii taka taka y'ako or else naku ignore.
 
Back
Top Bottom