Mambo ambayo kijana hutakiwi kufanya ili ujiwekee misingi ya maisha

KANYEGELO

JF-Expert Member
Nov 12, 2019
2,113
4,714
===. KUCHAGUA KAZI.
Ni vigumu kupata Kazi ukiwa nje ya Kazi. Fanya Kazi uliyoipata upate Kazi unayoitaka.

===√. KUCHAGUA SEHEMU YA KUISHI /KUFANYIA Kazi.
Maisha ni safari ndefu, maisha ni popote, si lazima kukaa mjini. Hauwezi kujua ni sehemu gan iliyobeba mafanikio yako. Chagua sehemu yenye FURSA na si yenye MAGHOROFA.

===√. KUISHI BILA KUWA NA MALENGO.
Maisha si bahat mbaya au nzuri. Maisha ni mipango, Maisha yanaongozwa na malengo. Vile ulivyo leo ni matokeo ya jinsi ulivyopanga jana, na vile unavyoishi leo ndivyo kesho yako itakavyokuwa. PANGA KESHO YAKO SASA.

°===√. MAISHA YA KUIGA.
Maisha yako si ya mwenzako, na ya maisha ya mwenzako si ya kwako. Si kila ukionacho ni lazima ufanye, chagua kipi cha kufanya na kipi cha kuacha. Kupitwa na jambo wakat mwingine sio USHAMBA ni BUSARA.

===√ KUISHI JUU YA KIPATO CHAKO.
Ishi kulingana NA vile ulivyonavyo na si usivyonavyo. Kuwa na Busara katika MATUMIZI uepukane na MADENI yasiyo na ULAZIMA. RIDHIKA NA VILE ULIVYONAVYO.

===√.KUISHI BILA AKIBA.
kuweka akiba ni TABIA sio kiwango kikubwa cha Pesa. Jenga tabia ya kujiwekea akiba. Haujui ni kipi kitakupata muda USIOTEGEMEA.

===√. KUISHI KWA kutegemea MSHAHARA.
Mshahara haujawahi kutosha na hautatosha kama ukishindwa kuishi chini ya kipato chako na kuwa na njia mbadala za kuinua kipato chako. JARIBU NJIA ZINGINE MBALI NA MSHAHARA.

===√KUSHINDWA Kupangilia MATUMIZI YA PESA.
Maamuzi yako ya pesa ndiyo yatajayoamua hali yako ya kiuchumi baadaye. Ni muhimu kujua kipi cha kununua, kwa wakat gani na kwa sababu gani. Jifunze kutofautisha kati ya liability (dhima) mfano: gari ya kutembelea na assets (kitegauchumi) mfano:nyumba au kiwanja . TUMIA PESA YAKO KUNUNUA ASSETS KULIKO LIABILITY.

sent from toyota Allex
 
Kanyegelo, mada yako ni nzuri ila hapo unapo-generalize kwa kusema nyumba au kiwanja ni Assets hapo inategemeana na matumizi ya hizo mali.

Asset ni mali/kitu ambacho kinakuingizia kipato,, sasa kama umejenga/kumiliki nyumba kwa kuishi wewe mwenyewe basi hio nyumba ni LIABILITY kwasababu haikuingizii pesa yoyote isipokuwa itakuwa inakukamua hela kwa maintanance& repairing, kulipia kodi ya majengo nk, so haitokuwa tofauti na kumiliki gari la kutembelea cuz nalo linahitaji huduma za repairing, bima, wese kila liwapo road.

Ila kama utajenga nyumba kwa matumizi yoyote ya kibiashara kama kupangisha, hotel, lodge etc basi hio nyumba ni Asset kwasababu itakuingizia kipato.

Kwa kumalizia tu, ASSET ni mali/ kitu chochote kinachopelekea wewe mmiliki kuingiza kipato wakati LIABILITY ni mali/vitu vinavyonyonya pato lako!!!
 

Similar Discussions

18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom