Mambo 7 yanayohusu haki za Zanzibar kwenye Muungano ambayo Kikosi Kazi cha Zanzibar walikubaliana yafanyiwe kazi

aleesha

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
768
1,104
1. Kuundwa kwa Tume ya Pamoja ya Fedha na kuanzishwa kwa Akaunti ya Pamoja ya Fedha kwa mujibu wa Katiba ya Muungano ili mapato na matumizi ya Muungano yawe wazi.

2. Gawio la Zanzibar kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) lizingatie hisa za Zanzibar zilizotoka Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki (EACB) wakati wa uanzishwaji wa Benki Kuu hiyo ambazo ni 11.02% badala ya 4.5% inayotumika sasa. Asilimia hiyo pia itumike katika misaada na mikopo.

3. Pamoja na Ushuru wa Forodha, Ushuru wa Bidhaa na Kodi ya Mapato kuwa suala la Muungano, mfumo na viwango vya kodi vizingatie uchumi wa Zanzibar ambao ni uchumi wa huduma (service economy) ulio tofauti na uchumi wa Bara ambao unategemea rasilimali (resource based economy).

4. Mipaka ya Bahari kati ya Zanzibar na Tanganyika iwekwe na itambuliwe wazi ili kujua eneo la utawala la kila upande na pia kuepusha uwezekano wa mivutano katika kufaidi rasilimali hasa katika maeneo yasiyo ya Muungano.

5. Umiliki wa Zanzibar wa kisiwa cha Fungu Mbaraka (Latham Island) uwekwe wazi kwa kutambua kuwa kisiwa hicho kimekuwa ni sehemu ya mamlaka ya Zanzibar tokea 1898 na hakujawahi kuwa na mzozo wa umiliki huo.

6. Suala la Mafuta na Gesi Asilia likamilishwe kuondolewa kwenye orodha ya mambo ya Muungano ndani ya Katiba ya Muungano ili Zanzibar iweze kusimamia kikamilifu sekta hiyo badala ya hali iliopo sasa ambapo mamlaka iliyopewa Zanzibar yametoka kwenye Sheria ya Bunge.

7. Nafasi na Uwakilishi wa Zanzibar kwenye Baraza la Mawaziri la Muungano uwekwe wazi ili kuhakikisha taswira halisi ya Muungano wa nchi mbili inaonekana wazi kwenye chombo hicho kikuu kinachosimamia sera na uendeshaji wa Serikali ya Muungano.
 
8. Raisi wa zanzibar ajaye atokee bara
Zinjibari una sifa moja! Kila wakitaka kukuvunja, huvunjika wao! Siku yako ya kusimama tena nchi yetu tukufu itafika, bi idhni Llah! Silali naingojea siku hiyo, Mwana Zinjibari!
 
Atakaye jaribu kuuvunja muungano “atavunjika yeye “
I remember that voice.
Zinjibari una sifa moja! Kila wakitaka kukuvunja, huvunjika wao! Siku yako ya kusimama tena nchi yetu tukufu itafika, bi idhni Llah! Silali naingojea siku hiyo, Mwana Zinjibari!
 
..Vipi kuhusu haki za Tanganyika ndani ya muungano?
Kimahesabu Lazima Jibu la msingi lipatikane kwanza ili iwe rahisi kukamilisha vipengele vyote vyenye changamoto ndani ya Muungano.:

1. Muungano ni baina ya Tanganyika na Zanzibar.Zanzibar inaendelea kudai haki zaidi,huku Tanganyika ikiwa imemezwa.Kuna umuhimu wa kuangalia aina ya Muungano.

2. Muungano ubainishe nafasi ya nchi zilizounda Muungano (Zanzibar na Tanganyika).

3. Mtizamo wa "Chako ni Chetu(cha wote) ,"Changu ni Changu" itatuchelewesha sana kuondoa kasoro zilizopo.
Kwani kuna baadhi ya vitu mwananchi wa bara(Tanganyika) hana haki,lakini mwananchi wa visiwani (Zanzibar)ana haki.

4. Mbinu zile zile za enzi hizoo,Tutajikuta Zanzibar ina zalisha nchi iitwayo Pemba.
Maana tuienda kwa "HAKI",kesho Muungano hautakuwepo,bali inakuja "Zanzibara" na "Zanzibar" na hatimaye "Mimi ni wa Unguja na sisi ni Wapemba.

Hii inaenda pole pole,Ilidaiwa Bendera,wakapewa Bendera;Ilidaiwa wimbo wa Taifa,wakepewa wimbo wa Taifa.
Likaletwa swali la mtego,"Zanzibar ni nchi au sio nchi?!

Ikatafutwa mbinu nyingine kwenda kuomba wanachama umoja wa Mataifa,bado haikutosha jaribio kupitia Micheal wa mpira wa miguu(kuomba wanachama wa Shirikisho la Mpira Afrika).

Kwa mtazamo wa mtiririko wa matukio ipo siku vizazi vijavyo vitakuja na Ufumbuzi wa kero za Muungano,kwa sasa Wanasiasa watengeneza maisha yao ya kisiasa.
 
Inatumika nguvu kubwa kuulinda muungano huu lakini kiukweli watu wameuchoka na hawautaki tena kwani hata mfumo wake hauleweki.
Wakati umefika sasa pande zote kukaa chini na kufanya mashauriano kuendana na mazingira ya sasa.
 
1. Kuundwa kwa Tume ya Pamoja ya Fedha na kuanzishwa kwa Akaunti ya Pamoja ya Fedha kwa mujibu wa Katiba ya Muungano ili mapato na matumizi ya Muungano yawe wazi.
2. Gawio la Zanzibar kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) lizingatie hisa za Zanzibar zilizotoka Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki (EACB) wakati wa uanzishwaji wa Benki Kuu hiyo ambazo ni 11.02% badala ya 4.5% inayotumika sasa. Asilimia hiyo pia itumike katika misaada na mikopo.
3. Pamoja na Ushuru wa Forodha, Ushuru wa Bidhaa na Kodi ya Mapato kuwa suala la Muungano, mfumo na viwango vya kodi vizingatie uchumi wa Zanzibar ambao ni uchumi wa huduma (service economy) ulio tofauti na uchumi wa Bara ambao unategemea rasilimali (resource based economy).
4. Mipaka ya Bahari kati ya Zanzibar na Tanganyika iwekwe na itambuliwe wazi ili kujua eneo la utawala la kila upande na pia kuepusha uwezekano wa mivutano katika kufaidi rasilimali hasa katika maeneo yasiyo ya Muungano.
5. Umiliki wa Zanzibar wa kisiwa cha Fungu Mbaraka (Latham Island) uwekwe wazi kwa kutambua kuwa kisiwa hicho kimekuwa ni sehemu ya mamlaka ya Zanzibar tokea 1898 na hakujawahi kuwa na mzozo wa umiliki huo.
6. Suala la Mafuta na Gesi Asilia likamilishwe kuondolewa kwenye orodha ya mambo ya Muungano ndani ya Katiba ya Muungano ili Zanzibar iweze kusimamia kikamilifu sekta hiyo badala ya hali iliopo sasa ambapo mamlaka iliyopewa Zanzibar yametoka kwenye Sheria ya Bunge.
7. Nafasi na Uwakilishi wa Zanzibar kwenye Baraza la Mawaziri la Muungano uwekwe wazi ili kuhakikisha taswira halisi ya Muungano wa nchi mbili inaonekana wazi kwenye chombo hicho kikuu kinachosimamia sera na uendeshaji wa Serikali ya Muungano.
Samia ana siasa kali za Uzanzibari huenda akasababisha kuvunjika kwa muungano wakija viongozi makini wasio machawa kutoka bara. Haiingii akilini watu milioni 2 wachukue 11% ya mapato ya watu milioni 60
 
1. Kuundwa kwa Tume ya Pamoja ya Fedha na kuanzishwa kwa Akaunti ya Pamoja ya Fedha kwa mujibu wa Katiba ya Muungano ili mapato na matumizi ya Muungano yawe wazi.
2. Gawio la Zanzibar kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) lizingatie hisa za Zanzibar zilizotoka Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki (EACB) wakati wa uanzishwaji wa Benki Kuu hiyo ambazo ni 11.02% badala ya 4.5% inayotumika sasa. Asilimia hiyo pia itumike katika misaada na mikopo.
3. Pamoja na Ushuru wa Forodha, Ushuru wa Bidhaa na Kodi ya Mapato kuwa suala la Muungano, mfumo na viwango vya kodi vizingatie uchumi wa Zanzibar ambao ni uchumi wa huduma (service economy) ulio tofauti na uchumi wa Bara ambao unategemea rasilimali (resource based economy).
4. Mipaka ya Bahari kati ya Zanzibar na Tanganyika iwekwe na itambuliwe wazi ili kujua eneo la utawala la kila upande na pia kuepusha uwezekano wa mivutano katika kufaidi rasilimali hasa katika maeneo yasiyo ya Muungano.
5. Umiliki wa Zanzibar wa kisiwa cha Fungu Mbaraka (Latham Island) uwekwe wazi kwa kutambua kuwa kisiwa hicho kimekuwa ni sehemu ya mamlaka ya Zanzibar tokea 1898 na hakujawahi kuwa na mzozo wa umiliki huo.
6. Suala la Mafuta na Gesi Asilia likamilishwe kuondolewa kwenye orodha ya mambo ya Muungano ndani ya Katiba ya Muungano ili Zanzibar iweze kusimamia kikamilifu sekta hiyo badala ya hali iliopo sasa ambapo mamlaka iliyopewa Zanzibar yametoka kwenye Sheria ya Bunge.
7. Nafasi na Uwakilishi wa Zanzibar kwenye Baraza la Mawaziri la Muungano uwekwe wazi ili kuhakikisha taswira halisi ya Muungano wa nchi mbili inaonekana wazi kwenye chombo hicho kikuu kinachosimamia sera na uendeshaji wa Serikali ya Muungano.
Chako chako changu chetu
 
Mimi nadhani na sisi huku tuunde tume yetu ya bara ije na mambo ya msingi tunayoyataka kutetea ubara wetu

Binafsi sionagi faida ya muungano,

Nafikiria ile April 26 mwaka 1964 muungano usingetokea kungepungua nini, naona labda haya malumbano ndio yangekosekana, kitu ambacho ni heri

Kwaheri Muungano karibu Jamhuri ya watu wa Tanganyika

It is about time, tujiite kwa fahari,

Sisi ni watanganyika

Mimi ni mtanganyika
 
Kuna kitu hakiko sawa,hivi lile deni la tanesko limefika bei gani sasa.

Bila kupambana kuwa na serikali moja na nchi moja huu upuuzi hauta isha.

Laa sivyo kila mtu achukue mbao zake.

Wanasiasa tunaitaka tanganyika yetu.
 
Hii yote mbona kama wanataka kupora na kuchukua vitu vya bara.
1.Swali haki ya Tanganyika ni hipi?
2(8.) Raisi wa zanzibar ajaye atokee bara.
3.Kwa nini wazanzibari wanamiliki ardhi bara?
4.Kwa nini wazanzibari wanakuja kufanya kazi bara tena kwenye sector zisizo za muungano kama Afya na ujenzi?
5.kila kitu wazanzibari wanacho changia kiwe wazi ili wakipewa mgawo wao tujui kwamba wamepata kutokana kiasi walicho changia.
1. Kuundwa kwa Tume ya Pamoja ya Fedha na kuanzishwa kwa Akaunti ya Pamoja ya Fedha kwa mujibu wa Katiba ya Muungano ili mapato na matumizi ya Muungano yawe wazi.
2. Gawio la Zanzibar kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) lizingatie hisa za Zanzibar zilizotoka Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki (EACB) wakati wa uanzishwaji wa Benki Kuu hiyo ambazo ni 11.02% badala ya 4.5% inayotumika sasa. Asilimia hiyo pia itumike katika misaada na mikopo.
3. Pamoja na Ushuru wa Forodha, Ushuru wa Bidhaa na Kodi ya Mapato kuwa suala la Muungano, mfumo na viwango vya kodi vizingatie uchumi wa Zanzibar ambao ni uchumi wa huduma (service economy) ulio tofauti na uchumi wa Bara ambao unategemea rasilimali (resource based economy).
4. Mipaka ya Bahari kati ya Zanzibar na Tanganyika iwekwe na itambuliwe wazi ili kujua eneo la utawala la kila upande na pia kuepusha uwezekano wa mivutano katika kufaidi rasilimali hasa katika maeneo yasiyo ya Muungano.
5. Umiliki wa Zanzibar wa kisiwa cha Fungu Mbaraka (Latham Island) uwekwe wazi kwa kutambua kuwa kisiwa hicho kimekuwa ni sehemu ya mamlaka ya Zanzibar tokea 1898 na hakujawahi kuwa na mzozo wa umiliki huo.
6. Suala la Mafuta na Gesi Asilia likamilishwe kuondolewa kwenye orodha ya mambo ya Muungano ndani ya Katiba ya Muungano ili Zanzibar iweze kusimamia kikamilifu sekta hiyo badala ya hali iliopo sasa ambapo mamlaka iliyopewa Zanzibar yametoka kwenye Sheria ya Bunge.
7. Nafasi na Uwakilishi wa Zanzibar kwenye Baraza la Mawaziri la Muungano uwekwe wazi ili kuhakikisha taswira halisi ya Muungano wa nchi mbili inaonekana wazi kwenye chombo hicho kikuu kinachosimamia sera na uendeshaji wa Serikali ya Muungano.
 
Hii yote mbona kama wanataka kupora na kuchukua vitu vya bara.
1.Swali haki ya Tanganyika ni hipi?
2(8.) Raisi wa zanzibar ajaye atokee bara.
3.Kwa nini wazanzibari wanamiliki ardhi bara?
4.Kwa nini wazanzibari wanakuja kufanya kazi bara tena kwenye sector zisizo za muungano kama Afya na ujenzi?
5.kila kitu wazanzibari wanacho changia kiwe wazi ili wakipewa mgawo wao tujui kwamba wamepata kutokana kiasi walicho changia.
Kwa ajili ya kukusaidia tu kidogo, Tume ya Pamoja ya Fedha iliajiri kampuni kubwa ya kimataifa ya ukaguzi (PriceWaterhouseCoopers) kufanya kazi hiyo na kutoa Ripoti ambapo ukiona mahesabu waliyoyagundua unaweza ukakimbia na hii hoja yako.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom