Sam Gidori
Senior Member
- Sep 7, 2020
- 165
- 414
Rais wa Marekani na mgombea wa chama cha Republic, Donald Trump anatarajiwa kukutana uso kwa uso na mpinzani wake, Joe Biden katika mdahalo wa kwanza wa urais unaotarajiwa kufanyika baadaye hii leo katika ukumbi wa Chuo cha Case Western Reserc, Cleveland, Ohio.
Mdahalo huo unatarajiwa kufanyika kwa muda wa dakika 90 bila kuwa na kipindi chochote cha mapumziko, kuanzia saa tatu kamili usiku kwa majira ya Ohio (Sawa na saa 10 alfajiri kwa majira ya Afrika Mashariki), ukiongozwa na mtangazaji wa kituo cha televisheni cha Fox News, Chriss Wallace.
Mdahalo wa leo ni wa kwanza kati ya midahalo minne inayotarajiwa kufanyika kabla ya uchaguzi mkuu wa Novemba 3, kwa mujibu wa Kamisheni inayosimamia midahalo ya uraisi. Tofauti na ilivyokuwa miaka yote iliyopita, mdahalo wa leo hautahusisha wagombea hao wawili kupeana mikono, na watu wote watakaoshiriki katika mdahalo huo watalazimika kupima virusi vya corona na kuchukua tahadhari zote za kiafya kuepusha maambukizi ya virusi vya corona.
Mambo yanayotarajiwa kutawala katika mdahalo wa leo ni Rekodi za Trump na Biden, Mahakama Kuu, Virusi vya Corona, Uchumi, Ubaguzi wa rangi, na Uadilifu katika zoezi la Uchaguzi, kwa mujibu wa Kamisheni ya Midahalo ya Urais.
Katika mdahalo huo, kila kipengele kitatengewa muda wa dakika 15, na kila mgombea ataruhusiwa kujibu swali kwa muda wa dakika 2 baada ya mwendesha mdahalo kufungua kipengele kwa kuuliza swali, kisha muda uliobaki utatumika kuendeleza mjadala kuhusu mada katika kipengele husika.
Ukwepaji kodi wa Trump
Moja kati ya mambo yanayoongeza joto la mdahalo wa leo ni suala lililoibuliwa na gazeti la New York Times siku ya Jumapili kuwa Rais Trump hakuwahi kulipa kodi kwa miaka 10 kati ya 15 kuanzia mwaka 2000, na kuwa tangu aliposhinda uchaguzi wa mwaka 2016, Trump alilipa kodi yenye thamani ya dola 750 tu.
Kampeni ya Biden ilitawaliwa na matangazo yaliyoonesha ni kwa kiasi gani waalimu, madaktari na manesi, kati ya wafanyakazi wengine, wanavyolipa kodi nyingi kuliko Trump, huku wengi wakiamini kuwa Biden atatumia hoja hiyo katika mdahalo wa leo. Hii si mara ya kwanza kwa suala la kodi ya Trump kuletwa katika mdahalo wa urais. Mwaka 2016, mgombea wa chama cha Democrat, Hillary Clinton aliwahi kusema kuwa Trump hataki kuweka wazi hesabu za kodi anayolipa, na kuwa kuna uwezekano wa ukwepaji wa kodi, kisha Trump akamjibu kwa kusema kuwa hilo ndilo jambo linalomfanya [Trump] kuwa mwerevu kuliko Clinton!
Ubaguzi wa Rangi
Ubaguzi wa rangi ni suala linalotarajiwa kuleta changamoto hasa katika mdahalo huu wa kwanza, kutokana na tofauti za wagombea hao wawili katika matukio ya ubaguzi wa rangi. Wakati Biden alionekana kuwa karibu na wahanga wa matukio ya ubaguzi wa rangi yaliyotendwa na polisi wa Marekani, Trump alitumia nguvu kubwa kulaumu vitendo vya uvunjifu wa amani na uporaji wa mali uliofanywa na waandamanaji, huku akionya kuwa kumchagua Biden ni kuchagua uvunjifu mkubwa zaidi wa amani. Biden, kwa upande wake, amesema kuwa kitendo cha Trump kushindwa kuwachukulia hatua waandamanaji wanaounga mkono utawala wa weupe mwaka 2017 ndicho kilichomshawishi kugombea urais, akisema kuwa misingi ya taifa ipo mashakani.
Kauli za Trump za upotoshaji
Rais Trump pia anafahamika kwa kutoa kauli zenye upotoshaji, na wengi wamekuwa wakijiuliza ikiwa kutakuwa na mtu atakayekuwa tayari kuhakiki kauli zake akiwa katika mdahalo huo. Lakini Mwenyekiti Msaidizi wa Kamisheni ya Uchaguzi amesisitiza kuwa hakutakuwa na mwongozaji yeyote katika mdahalo wa leo atakayekuwa akihakiki kauli za Trump pindi atakapokuwa jukwaani, lakini amesema kuwa wapo watazamaji wengi watakaokuwa wakisubiri atakachozungumza Rais Trump kwa ajili ya kuhakiki ukweli.
Chanzo: CNN
Mdahalo huo unatarajiwa kufanyika kwa muda wa dakika 90 bila kuwa na kipindi chochote cha mapumziko, kuanzia saa tatu kamili usiku kwa majira ya Ohio (Sawa na saa 10 alfajiri kwa majira ya Afrika Mashariki), ukiongozwa na mtangazaji wa kituo cha televisheni cha Fox News, Chriss Wallace.
Mdahalo wa leo ni wa kwanza kati ya midahalo minne inayotarajiwa kufanyika kabla ya uchaguzi mkuu wa Novemba 3, kwa mujibu wa Kamisheni inayosimamia midahalo ya uraisi. Tofauti na ilivyokuwa miaka yote iliyopita, mdahalo wa leo hautahusisha wagombea hao wawili kupeana mikono, na watu wote watakaoshiriki katika mdahalo huo watalazimika kupima virusi vya corona na kuchukua tahadhari zote za kiafya kuepusha maambukizi ya virusi vya corona.
Mambo yanayotarajiwa kutawala katika mdahalo wa leo ni Rekodi za Trump na Biden, Mahakama Kuu, Virusi vya Corona, Uchumi, Ubaguzi wa rangi, na Uadilifu katika zoezi la Uchaguzi, kwa mujibu wa Kamisheni ya Midahalo ya Urais.
Katika mdahalo huo, kila kipengele kitatengewa muda wa dakika 15, na kila mgombea ataruhusiwa kujibu swali kwa muda wa dakika 2 baada ya mwendesha mdahalo kufungua kipengele kwa kuuliza swali, kisha muda uliobaki utatumika kuendeleza mjadala kuhusu mada katika kipengele husika.
Ukwepaji kodi wa Trump
Moja kati ya mambo yanayoongeza joto la mdahalo wa leo ni suala lililoibuliwa na gazeti la New York Times siku ya Jumapili kuwa Rais Trump hakuwahi kulipa kodi kwa miaka 10 kati ya 15 kuanzia mwaka 2000, na kuwa tangu aliposhinda uchaguzi wa mwaka 2016, Trump alilipa kodi yenye thamani ya dola 750 tu.
Kampeni ya Biden ilitawaliwa na matangazo yaliyoonesha ni kwa kiasi gani waalimu, madaktari na manesi, kati ya wafanyakazi wengine, wanavyolipa kodi nyingi kuliko Trump, huku wengi wakiamini kuwa Biden atatumia hoja hiyo katika mdahalo wa leo. Hii si mara ya kwanza kwa suala la kodi ya Trump kuletwa katika mdahalo wa urais. Mwaka 2016, mgombea wa chama cha Democrat, Hillary Clinton aliwahi kusema kuwa Trump hataki kuweka wazi hesabu za kodi anayolipa, na kuwa kuna uwezekano wa ukwepaji wa kodi, kisha Trump akamjibu kwa kusema kuwa hilo ndilo jambo linalomfanya [Trump] kuwa mwerevu kuliko Clinton!
Ubaguzi wa Rangi
Ubaguzi wa rangi ni suala linalotarajiwa kuleta changamoto hasa katika mdahalo huu wa kwanza, kutokana na tofauti za wagombea hao wawili katika matukio ya ubaguzi wa rangi. Wakati Biden alionekana kuwa karibu na wahanga wa matukio ya ubaguzi wa rangi yaliyotendwa na polisi wa Marekani, Trump alitumia nguvu kubwa kulaumu vitendo vya uvunjifu wa amani na uporaji wa mali uliofanywa na waandamanaji, huku akionya kuwa kumchagua Biden ni kuchagua uvunjifu mkubwa zaidi wa amani. Biden, kwa upande wake, amesema kuwa kitendo cha Trump kushindwa kuwachukulia hatua waandamanaji wanaounga mkono utawala wa weupe mwaka 2017 ndicho kilichomshawishi kugombea urais, akisema kuwa misingi ya taifa ipo mashakani.
Kauli za Trump za upotoshaji
Rais Trump pia anafahamika kwa kutoa kauli zenye upotoshaji, na wengi wamekuwa wakijiuliza ikiwa kutakuwa na mtu atakayekuwa tayari kuhakiki kauli zake akiwa katika mdahalo huo. Lakini Mwenyekiti Msaidizi wa Kamisheni ya Uchaguzi amesisitiza kuwa hakutakuwa na mwongozaji yeyote katika mdahalo wa leo atakayekuwa akihakiki kauli za Trump pindi atakapokuwa jukwaani, lakini amesema kuwa wapo watazamaji wengi watakaokuwa wakisubiri atakachozungumza Rais Trump kwa ajili ya kuhakiki ukweli.
Chanzo: CNN