Mambo 5 yatakayoviangusha vyama vya Upinzani katika Uchaguzi Mkuu 2020

zandrano

JF-Expert Member
Jan 24, 2017
7,121
7,705
Mbali na kampeni zenye maneno matamu na ahadi kabambe kutoka vyama vya upinzani lakini Watanzania walio wengi hawaviamini vyama vya upinzani kwa sababu zifuatazo;

1. Wananchi wengi hawaviamini vyama vya upinzani kutokana na kutokukomaa lakini pia kukosekana kwa hazina ya viongozi walioiva kuongoza nchi.

Hivyo wananchi bado wana hofu na mashaka makubwa kuwapigia Kura vyama vya upinzani, wanachi wana hisi kuwapa nchi wapinzani ni sawa sawa na kumkabidhi bunduki mtoto mdogo.

2. Wananchi wengi hawaviamini vyama vya upinzani kutokana na baadhi ya vyama vya upinzani kuwa na "UBIA" na mataifa ya kibeberu, hivyo wananchi wana hofu juu ya usalama wa rasilimali zao, wanahisi ubia huo unalengo la kukaribisha unyonyaji wa rasilimali zetu. yaani inawezekana baadhi ya vyama vina malengo ya siri na washirika wa kibeberu.

3. Ukali wa matamshi yatolewayo na baadhi ya vyama vya upinzani, wananchi wengi wanawasiwai juu ya kauli kali zinazotolewa na vyama vya upinzani ambazo zinaashiria au kuchochea vurugu na kutisha amani ya wananchi, wananchi wengi wamezoea amani na utulivu.hawataki purukushani za vyama vya upinzani.

4. Utitiri wa wagombea wa kiti cha uraisi, tofauti na chaguzi zilizo pita mwaka huu 2020 kumekuwa na idadi kubwa ya wagombea kiti cha uraisi kwa vyama vya upinzani, ambapo kila chama kina nia ya kuing'oa CCM, sawa tunaweza kusema ndio kukomaa kwa demokrasia lakini unapo dhamiria kukiondoa chama kikubwa na kikongwe kama CCM chenye umri wa miaka 43 hamna budi kuunganisha nguvu kinyume chake ni sawa sawa na kutaka kuuangusha/kukata mbuyu kwa kutumia kiwembe, wananchi wengi wanaamini kuwa hakuna chama cha upinzani kitakacho simama peke yake na kikafanikiwa kuiangusha CCM.

5. Wanachi wengi wanaamini kuwa uhakika wa AMANI yao na UTULIVU wao unapatikana chini ya utawala wa CCM na sio vyama vya upinzani. uthibitisho wa hayo ni kutokana na uzoefu kuanzia TANU na kisha CCM . wananchi wengi wana tathimini na kubaini kuwa bado chama mbadala zaidi ya ccm hakijapatikana.

Zaidi ya miaka 68 nchi imetulia tuliii hivyo hakuna haja ya chama kingine. Ni kazi ngumu sana kuiangusha CCM sio mwaka huu tu wa 2020 bali hata miaka 50 ijayo bado itakuwa vigumu hadi pale patakapo patikana wapinzani imara na walio iva kuiongoza nchi.
 
Huo utafiti wako umeufanyia wapi mkuu?

Wananchi wa miaka hii si wale wa 2010-2015 , Tangu enzi tunazaliwa tulikutana na uongozi wa chama cha mapinduzi katika tawalaza nchi yetu.

Sasa umefika wakati ambapo hatuwezi kuvumilia kuendelea kushuhudia hali ngumu ya maisha ikiendelea kudidimiza ndoto zetu,Uchaguzi wa 2020 ni kati ya Haki na dhulma hivyo tunatarajia asilimia80 ya wapiga kura kuchagua haki dhidi ya dhulma, Serikali ya kidicteta inakwenda kufika ukingoni 28 oct.
 
Hapo hoja ya maana uliyoitoa ni Na.4 pekee. Ubinafsi wa vyama pinzani unatupa ugumu sana kuiondoa ccm madarakani. Wengi wanamsifu Lowassa kwa 2015 lakini ule muungano wa UKAWA uliongeza nguvu kubwa sana. Hapo wamenikera sana, mtu kama Membe anaona kabisa hakuna uwezekano wa ushindi hata kwa kutambikia ila bado amegangamala tu hadi naanza kuamini katumwa.

Hizo hoja zingine ungeziunganisha na kuwa hoja moja tu: ujinga/ukosefu wa elimu/umbumbumbu/ungumbaru wa watanzania wengi sana. Kufikiri amani, uhuru, na haki ni vitu vinavyopatikana ccm ni zaidi ya ujinga/ni upumbavu kabisa.
 
Hujitambui wewe mbuzi wewe
Hivi migodi yote nchi hii hujui wamepewa mabeberu,au kuna mgodi unaujua unamilikiwa na ccm
juzi pale kakola wazawa wamefurushwa na beberu kazungusha uzio
Hujui mashirika ya umma yaliuzwa kwa mabeberu ,ikiwemo NBC
 
Vyama havina Sura ya kitaifa, Vyama vimezubaa havina mipango madhubuti ya kuwa chama mbadala , wanavizia chaguzi na Huruma kwa wanachi, ni lazima vife tuu.
 
Kwa mtazamo wangu ni hiyo namba nne tu ndio ina mashiko. Siwaelewi wapinzani kila wakati wa uchaguzi kurudia kosa lile lile na kuunganishwa nguvu miezi michache kabla ya uchaguzi. Mwakachuu 2020 ndio hata sikuona hiyo dhamira.
Sijui kwa nini mara uchaguzi unapokwisha hawaoni ndio muda wa kuanza kuunganisha nguvu na kujitanabaisha kwa umma wanachosimamia, hatimaye kwa miaka minne wananchi wawazoee.
 
Mawazo haya uliyoyaandika leo ndiyo mawazo hayo hayo waliyokuwa nayo raia mwaka '92 kwenye kura ya maoni kuhusu kurejeshwa kwa mfumo wa siasa ya vyama vingi.

Raia %kubwa walisema 'no to mult partism', lakini Alhaji Mwinyi akatuingiza kwenye system hii ki'makame nguvu'!

Sidhani kama yalikuwa ni maamuzi yake sahihi toka moyoni mwake, maana kama siyo ushauri wa 'mchonga' basi lilikuwa ni shinikizo lilitoka Imf kwa wenye hela.

Sanduku la kura halali ndiyo sauti ya majority, je zaidi ya miongo miwili kuwa na mawazo yale yale ni kweli kuwa raia hawaupendi mfumo wa vyama vingi au mfumo wa vyama vingi wenyewe ndiyo hauwapendi raia wa Tz?
 
Mawazo haya uliyoyaandika leo ndiyo mawazo hayo hayo waliyokuwa nayo raia mwaka '92 kwenye kura ya maoni kuhusu kurejeshwa kwa mfumo wa siasa ya vyama vingi.

Raia %kubwa walisema 'no to mult partism', lakini Alhaji Mwinyi akatuingiza kwenye system hii ki'makame nguvu'!

Sidhani kama yalikuwa ni maamuzi yake sahihi toka moyoni mwake, maana kama siyo ushauri wa 'mchonga' basi lilikuwa ni shinikizo lilitoka Imf kwa wenye hela.

Sanduku la kura halali ndiyo sauti ya majority, je zaidi ya miongo miwili kuwa na mawazo yale yale ni kweli kuwa raia hawaupendi mfumo wa vyama vingi au mfumo wa vyama vingi wenyewe ndiyo hauwapendi raia wa Tz?
Kama raia hawapendi mfumo wa vyama vingi ni kwanini uchaguzi unakua siri kubwa sana kati ya NEC na serikali?
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Kama raia hawapendi mfumo wa vyama vingi ni kwanini uchaguzi unakua siri kubwa sana kati ya NEC na serikali?
Katika mambo ambayo 'raia huru' hatuyapendi ni pamoja na hayo makandokando!

Kuna mambo mengi tu ya kijingajinga yanafanywa na watu utadhani hawajaenda shule!

Kila mtu anajua suala la kunywa maji punda ni la hiyari, lakini ukifika muda wa kumnywesha, watu wanataka kujizolea umaarufu kuwa wamemsimamia na kumnywesha punda maji, hivyo wanastahili sifa na pongezi!

Yaani kuna watu walihemka hadi aibu!
 
Ishu sio kuwa na sura ya kitaifa..
Tatizo wamefanyiwa USHENZI NA UJAMBAZI .
kwanini ccm na NEC waingize kura feki?
Vyama havina Sura ya kitaifa, Vyama vimezubaa havina mipango madhubuti ya kuwa chama mbadala , wanavizia chaguzi na Huruma kwa wanachi, ni lazima vife tuu.
 
Katika mambo ambayo 'raia huru' hatuyapendi ni pamoja na hayo makandokando!

Kuna mambo mengi tu ya kijingajinga yanafanywa na watu utadhani hawajaenda shule!

Kila mtu anajua suala la kunywa maji punda ni la hiyari, lakini ukifika muda wa kumnywesha, watu wanataka kujizolea umaarufu kuwa wamemsimamia na kumnywesha punda maji, hivyo wanastahili sifa na pongezi!

Yaani kuna watu walihemka hadi aibu!
Hiyo mihemko iliathiri vipi za Duku la kura?
 
Ishu sio kuwa na sura ya kitaifa..
Tatizo wamefanyiwa USHENZI NA UJAMBAZI .
kwanini ccm na NEC waingize kura feki?
Sijasikia uthibitisho wa hilo.

Sisi wasema ovyo hatuna cha Ccm wala cha nini ili mradi kuwepo ukweli.

Na ninasema Ccm wanacheka sana na ngedere, kama lipo hilo basi ni doa lisilovumilika na litawachafua sana.

Hizi figisu za kijingajinga kuanzia mchezo wa wasimamizi kuengua wagombea kwa sababu za makosa madogo madogo katika ujazaji fomu za kutia nia ni matusi na matope kupakwa Ccm bila ulazima wowote.

Haya hayakutakiwa kukemewa na kuachwa, bali zilitakiwa kuchukuliwa hatua madhubuti za watu kuswekwa jela kwa hukumu, ili siku nyingine wasije kurudia michezo ya kipumbafpumbaf inayoweza kuligharimu taifa.
 
Ehee kura feki zimekamatwa za kutosha.unakaa nchi gani?.
Malori kwa malori..
Cha ajabu NEC WANAKATAA WANASEMA HAKUNA KURA FEKI.sasa wamekwenda kuziangalia na kujua Kama ni karatasi zao au sio zao?
Kwanini wakatae kuwa HAKUNA KURA FEKI?
Sijasikia uthibitisho wa hilo.

Sisi wasema ovyo hatuna cha Ccm wala cha nini ili mradi kuwepo ukweli.

Na ninasema Ccm wanacheka sana na ngedere, kama lipo hilo basi ni doa lisilovumilika na litawachafua sana.

Hizi figisu za kijingajinga kuanzia mchezo wa wasimamizi kuengua wagombea kwa sababu za makosa madogo madogo katika ujazaji fomu za kutia nia ni matusi na matope kupakwa Ccm bila ulazima wowote.

Haya hayakutakiwa kukemewa na kuachwa, bali zilitakiwa kuchukuliwa hatua madhubuti za watu kuswekwa jela kwa hukumu, ili siku nyingine wasije kurudia michezo ya kipumbafpumbaf inayoweza kuligharimu taifa.
 
Hiyo mihemko iliathiri vipi za Duku la kura?
Athari ni kama hizo tunazozisikia za kura feki na tangia mwanzo wa zoezi hili kuengua watia nia kwa makosa madogo madogo ya ujazaji wa fomu!

Sisi hatukutaka madoa haya yasiyo ya lazima yawepo ili kuulinda upande utakaokuwa umejizolea ushindi.

Lakini kusherehekea ushindi huku kuna minong'ono ya kura feki ni doa lisilokubalika.

Tena ngoja nilifuatilie vizuri toka huko kwenye vyanzo vya habari hii mbaya.
 
Athari ni kama hizo tunazozisikia za kura feki na tangia mwanzo wa zoezi hili kuengua watia nia kwa makosa madogo madogo ya ujazaji wa fomu!

Sisi hatukutaka madoa haya yasiyo ya lazima yawepo ili kuulinda upande utakaokuwa umejizolea ushindi.

Lakini kusherehekea ushindi huku kuna minong'ono ya kura feki ni doa lisilokubalika.

Tena ngoja nilifuatilie vizuri toka huko kwenye vyanzo vya habari hii mbaya.
Kwanini Magufuli asiapishwe kama Mfalme wa Tanzania na awe anateua wasaidizi wake wanaompendeza kuanzia ngazi ya mitaa. Tutaokoa pesa za maigizo ya uchaguzi na hatapata watu wa kupinga hoja zake.
 
Hongera sana kwa hizi nondo zako.. na walipita kama hawakukusoma. Leo umemgusa Bibie juu yangu.. :D:D:D.. tabu hawapendi kuambiwa ukweli.. wametekwa akili.. huku wengi ni wale wavivu.. walioisoma namba etc
 
Back
Top Bottom