Mkuu Ritz
Huyo Mikael P Aweda ni wale wale tu hana jipya unajua tena wanaishi mjini kiujanjaujanja lazima aishi kwa kujipendekeza!
Last edited by a moderator:
Hili nalo linaukweli wake , kuna namna Lema anatakiwa achukuliwe hatua za kinidhamu.
utata juu ya wote waliojiuzulu chadema
.
Mimi kwenye Elimu ya shule za secondary mpaka high school na kuendelea niliopt kusoma masoma ya arts ikiwepo Lugha nk. kwa mantiki hiyo, nikichukua tamko la M/kiti wa Temeke, nikilinganisha na M/kiti Feki wa matawi ya Chadema mwanza, halafu nikiMalizia na m/kiti wa mkoa Singida na wengineo akiwepo Chatanda kama wewe ni mtaalam wa Lugha utagundua mambo yafuatayo.
Mosi, Staili ya uandishi kuanzia kichwa cha habari fonti inayotumika, upangaji wa aya mfumo wa uwasilishaji hoja au kwa ujumla tunasema staili ya uandishi ni ya mtu moja tu. Swali ni kwa nini na mtu huyo ni nani?
Pili, Hoja au tuhuma zinazotolewa zinafanana na msisitizo wake pia unafanana sana kiasi kwamba mwandishi huyo siyo mzuri hata wa kubadilisha lugha ili afiche malengo yake. Je kwanini na nani???
Tatu, kuanzia press kubwa ya Dsm, uchomaji wa ofisi za Chadema Arusha, Tamko la Mwanza na Singida nyuma yake utawakuta UVCCM wakiratibu. swali ni kwa nini na kwa ufadhili na mwongozo wa nani??
Nne, leo nimepata mahali taarifa zisizo rasmi kuwa kuna fungu la Sh mil 5 na kuendelea za kuwapa viongozi wa chadema nchi nzima. Sasa sina hakika kama hawa waliotangaza uamuzi wa kujiuzulu wamefikiwa na mafungu ya ccm au ni dhamiri zao. Time will tell.
Kwa kuhitimisha, matamko haya kuandikwa na mtu moja na kusomwa na watu wengine, pengine kwa kulipwa fedha kama fununu zinavyodai, kufanana kwa hoja za wanaojiuzulu na uwepo wa uvccm nyuma ya mikakati hiyo, kunanifanya niamini kuwa huu ni mchezo wa intelijensia fulani feki ambayo kiukweli ni mchezo wa danganya toto.- hadanganyiki mtu hapa.
Akili za kuambiwa nikichanganya na zangu, napata jawabu kuwa huu ni mkakati wa ccm. Chadema tutuvuka haya majaribu ni madogo sana kwangu. Aluta continua.
Hii hoja ya mdau nayo ina mashiko ukiunganisha dots ya malalamiko ya Mwigulu Fb.
CCM NI CHAMA PINZANI KINACHOHISI KITAKOSA MWANA KM CUF...WAPO BUSY.KUTETEA UPINZANI WAO.
yaani CCM na CDM wangekuwa viumbe hai basi CCM ingekuwa nyumbu,CDM ingekuwa Binadamu.
mkuu mbona unajifanya kama ukuona hoja za walio amua kujiuzulu?hebu zijibu. Au wote ni wasaliti na ni waongo?
Unajua watu kama wewe ndo mnastahili kufungwa jiwe shingoni na kutumbukizwa katikati ya bahari. Hapa mambo ya uchaga yanatoka wapi. mimi siyo mchaga lakini kwa nini unaingiza uchaga hapa. Nina mashaka sana na weledi wako
na moja kati ya mashitaka yao ni kuwa chadema imeshikwa na watu wa kaskazini, lakini cha kusikitisha mpaka sasa wanaojitokeza kuwapinga wote ni wa kaskazini.
1. MICHAEL AWEDA - KULE KULE
2, EBENEZAR KWAYU - KULE KULE
3. ELIREHEMA - KULE KULE
Nami nazidi kupata mashaka na kuelewa kilichopo ndani ya watetezi wa chama kwanini wote watoke eneo moja.