mbinguni
JF-Expert Member
- Jan 2, 2013
- 2,746
- 1,051
Ulichokisema kamanda ni kweli kabisa.Wote wanaofanya huu upumbavu ni walala njaa wa ccm ambao kwao wakishafanya upumbavu huu, hurudi kwa mabwana zao ili walipwe ujira wao.Hakuna dhambi mbaya kama njaa ya kutumika ili kuharibu juhudi mbadala za kuwakomboa watanganyika wanaoishi maisha ya kifukara bila sababu ya msingi wakati wana rasilimali nyingi zisizowasaidia kutoka katika ufukara huo.Pamoja na juhudi zote hizi za kujaribu kudhoofisha harakati hizi za ukombozi lakini ukombozi lazima utapatikana tu.
utata juu ya wote waliojiuzulu chadema
.
Mimi kwenye Elimu ya shule za secondary mpaka high school na kuendelea niliopt kusoma masoma ya arts ikiwepo Lugha nk. kwa mantiki hiyo, nikichukua tamko la M/kiti wa Temeke, nikilinganisha na M/kiti Feki wa matawi ya Chadema mwanza, halafu nikiMalizia na m/kiti wa mkoa Singida na wengineo akiwepo Chatanda kama wewe ni mtaalam wa Lugha utagundua mambo yafuatayo.
Mosi, Staili ya uandishi kuanzia kichwa cha habari fonti inayotumika, upangaji wa aya mfumo wa uwasilishaji hoja au kwa ujumla tunasema staili ya uandishi ni ya mtu moja tu. Swali ni kwa nini na mtu huyo ni nani?
Pili, Hoja au tuhuma zinazotolewa zinafanana na msisitizo wake pia unafanana sana kiasi kwamba mwandishi huyo siyo mzuri hata wa kubadilisha lugha ili afiche malengo yake. Je kwanini na nani???
Tatu, kuanzia press kubwa ya Dsm, uchomaji wa ofisi za Chadema Arusha, Tamko la Mwanza na Singida nyuma yake utawakuta UVCCM wakiratibu. swali ni kwa nini na kwa ufadhili na mwongozo wa nani??
Nne, leo nimepata mahali taarifa zisizo rasmi kuwa kuna fungu la Sh mil 5 na kuendelea za kuwapa viongozi wa chadema nchi nzima. Sasa sina hakika kama hawa waliotangaza uamuzi wa kujiuzulu wamefikiwa na mafungu ya ccm au ni dhamiri zao. Time will tell.
Kwa kuhitimisha, matamko haya kuandikwa na mtu moja na kusomwa na watu wengine, pengine kwa kulipwa fedha kama fununu zinavyodai, kufanana kwa hoja za wanaojiuzulu na uwepo wa uvccm nyuma ya mikakati hiyo, kunanifanya niamini kuwa huu ni mchezo wa intelijensia fulani feki ambayo kiukweli ni mchezo wa danganya toto.- hadanganyiki mtu hapa.
Akili za kuambiwa nikichanganya na zangu, napata jawabu kuwa huu ni mkakati wa ccm. Chadema tutuvuka haya majaribu ni madogo sana kwangu. Aluta continua.