Mamba asingewekwa kwenye kundi la Super Predator hastaili kabisa

Maghayo

JF-Expert Member
Oct 5, 2014
13,634
28,785
Mzuka wanajamvi!

Mamba hakidhi vigezo vya kuitwa au kuwa Super Predator. Kwa mtazamo wangu hastaili kuwa kabisa kwenye Hilo kundi la Super predator.

Wanyama wengine ambao wako kwenye Hilo kundi Simba, Chui, Duma, Mbwa mwitu na Fisi wanastahili sifa zote na wanakidhi vigezo.

Licha ya uhodari wa Mamba, nguvu, kuogopwa, ukubwa wa mwili ushupavu na nguvu zote anazo anavyowinda na kutwaa windo Bado tu ni mchumbaaa kwasababu ANATAGA.
 
Kuna mwamba anaitwa jaguar, anafuta mamba kumayi na kumburuta
Huwa wanatafuna vile vi-cayman au alligators vya America na Asia. Ila sio African crocodile. Huyu kiumbe ni habari nyingine!

Kila kiumbe kinachoishi Africa kimevurugwa. Kuna documentary moja niliona simba aliingia mtoni kwa kiburi chake akajua jamaa hawamuwezi. Alinusurika ila akabaki taya linaning'inia, akaenda kufia mbele huko!
 
Huwa wanatafuna vile vi-cayman au alligators vya America na Asia. Ila sio African crocodile. Huyu kiumbe ni habari nyingine!

Kila kiumbe kinachoishi Africa kimevurugwa. Kuna documentary moja niliona simba aliingia mtoni kwa kiburi chake akajua jamaa hawamuwezi. Alinusurika ila akabaki taya linaning'inia, akaenda kufia mbele huko!
Upo sahihi, viumbe vya Africa vyote vimevurugwa, kuna kuku ana vifaranga Leo kanirukia aniparue bila kosa lolote.
 
Huwa wanatafuna vile vi-cayman au alligators vya America na Asia. Ila sio African crocodile. Huyu kiumbe ni habari nyingine!

Kila kiumbe kinachoishi Africa kimevurugwa. Kuna documentary moja niliona simba aliingia mtoni kwa kiburi chake akajua jamaa hawamuwezi. Alinusurika ila akabaki taya linaning'inia, akaenda kufia mbele huko!
Bado Simba alionyesha umwamba tu kutoka hai
 
Back
Top Bottom