Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Wazungu wana vituko vyao, ati leo wao ndio wanautangazia ulimwengu kuwa wamegundua mamalia mpya. Hivi haka kamnyama hakuna aliyewahi kukaona huko Tanzania?
Ndo tabia yao hiyo, si mnakumbuka wanavyosema walivyovumbua Mlima Kilimanjaro wakati kila siku wachagga walikuwa wanauona, na kwenda kutambika huko au Ziwa Nyanza wakati wasukuma, wahaya, wajaluo, nk kila siku walikuwa wanavua samaki pale!,na kinachonipandisha hasira zaidi wakabadilisha na jina la ziwa hili na kuliita Victoria (Malkia wao ambaye hana faida yeyote na wazawa wa eneo hilo!) Mimi binafsi kupingana na huo ujinga wao siku zote naliita lile ziwa kwa jina lake halisi yaani "Ziwa Nyanza" na siyo Victoria!!,Wazungu wana vituko vyao, ati leo wao ndio wanautangazia ulimwengu kuwa wamegundua mamalia mpya. Hivi haka kamnyama hakuna aliyewahi kukaona huko Tanzania?
Ndo tabia yao hiyo, si mnakumbuka wanavyosema walivyovumbua Mlima Kilimanjaro wakati kila siku wachagga walikuwa wanauona, na kwenda kutambika huko au Ziwa Nyanza wakati wasukuma, wahaya, wajaluo, nk kila siku walikuwa wanavua samaki pale!,na kinachonipandisha hasira zaidi wakabadilisha na jina la ziwa hili na kuliita Victoria (Malkia wao ambaye hana faida yeyote na wazawa wa eneo hilo!) Mimi binafsi kupingana na huo ujinga wao siku zote naliita lile ziwa kwa jina lake halisi yaani "Ziwa Nyanza" na siyo Victoria!!,
Hebu fikiria leo hii M-bantu aenda USA na Mississipi auite (Mtemi) Milambo, au River Danube uite River Mkwawa je watakubali au Mto Thames wa Uingereza uitwe Kinjeketile je watakubali?
1. Hii habari tayari ilikuwa hapa ingeunganishwa iwe moja!