Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
Asema hana mpinzani
na Deogratius Temba
JITIHADA za kuhakikisha Rais Kikwete anaendelea kukubalika kwa wananchi na kuchaguliwa zinazidi kushamiri ambapo mama wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) Zitto Kabwe ametangaza kuwa hakuna mtu yeyote mwenye kufaa nafasi hiyo hivi sasa.
Mama huyo, Shida Salum, ambaye ni mwenyekiti wa walemavu, alitangaza kumuunga mkono Kikwete juzi kwenye viwanja vya Temeke, jijini Dar es salaam, alipokuwa kwenye mkutano wa Aman Forum.
Alisema Rais amefanya kazi nzuri ya kuimarisha amani na kuwatetea walemavu hivyo ni vema Watanzania wakampa fursa ya kuongoza kwa kuwa wanasiasa waliopo hivi sasa iwe wa CCM au wa vyama vya upinzani hawajafikia viwango vya kuwania urais.
Ninasema hivi; hakuna mtu anayeweza kuwatetea walemavu kama Rais Kikwete, amewakamata wauaji wa maalbino, na sasa anatutetea zaidi, kura zote za urais ni kwa Rais Kikwete, wapinzani watapata za ubunge tu! alisema.
Aliongeza kuwa wapinzani wanapaswa kujiandaa kumsimamisha mgombea urais mwaka 2015 ili kuepuka matokeo mabaya wanayoweza kuyapata iwapo watamsimamisha mgombea wa urais ili kukabiliana na Kikwete.
Mkutano huo ambao uliongozwa na Mbunge wa Bunge la Afrika ya Mashariki, Walid Aman Kaborou, na pia kuhudhuriwa na wajumbe kutoka vyama vya Tanzania Labour (TLP) na NCCR- Mageuzi, limewashambulia viongozi wa Taasisi ya Mfuko wa Mwalimu Nyerere (MNF) kuwa ni wachochezi.
Akizungumza kwenye mkutano huo uliohudhuriwa na watu wachache, Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema, alisema amejiunga na taasisi ya Aman Forum, kwa sababu amegundua kuwa nchi ina tatizo hasa unapofikia wakati wa uchaguzi wa urais.
Kuna kundi la watu lina njama za kumdhuru au kumsambaratisha Rais Kikwete na serikali yake, wajue kuwa wakifanya hivyo hawatakuwa wamekidhuru chama tawala bali ni Watanzania wote, mimi nimeamua kujiunga na Amani Forum, ili sasa nitangaze vita na kundi hilo, alisema Mrema.
Mrema alibainisha kuwa ameamua kuitetea nchi na hajahongwa wala kununuliwa na mtu yeyote kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakimtuhumu.
Aidha, aliwashambulia makada wa CCM na viongozi wastaafu walioshiriki kuchangia hoja katika tamasha la kumuenzi hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, lililofanyika katika ukumbi wa Karimejee mwishoni mwa mwaka jana kuwa ni wachochezi na wanatakiwa kukamatwa kwa sababu hawana heshima kwa rais wa nchi.
Kuna tamasha la Mwalimu Nyerere, makada wa CCM wamelitumia kama kichaka cha kuendesha uhaini hawa walinunuliwa; wamesema Kikwete amezungukwa na wezi, wanamtukana rais? Nyie CCM mnamtusi kiongozi wenu anayewapeperushia bendera?
Mrema ambaye aliwahi kuibua kashfa ya ufisadi wa kuibiwa kwa sh bilioni 900, ambayo ilimhusisha pia Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, alisema katika miaka minne, Rais Kikwete amefanya mambo makubwa ikiwepo kuruhusu wasaidizi wake wajiuzulu, kwa kuhusishwa.
Hivi mnamtaka afanye maamuzi gani mazito, wakati amekubali rafiki yake aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa ajiuzulu? Serikali si imewajibika? Mnasema mtamtosa kwa kosa gani alilofanya Rais Kikwete?
Mrema aliendelea kusema kuwa suala la ufisadi hata Baba wa Taifa alilishindwa kwa sababu baadhi ya viongozi waliokuwa wakifanya naye kazi walipohusishwa na ufisadi aliwahamisha au kuwaongezea majukumu badala ya kuwawajibisha.
Mwingira aliuza ndege ya serikali, mbona Nyerere alimhamisha na kumpa ukuu wa mkoa wa Arusha? Balozi Mustafa Nyanganyi alinunua kivuko kibovu Mwalimu akampa ubalozi wa Marekani; Rais Kikwete amewapeleka watu mahakamani ninyi mnasema mtamtosa! alishangaa Mrema.
Mrema aliyekuwa amefuatana na baadhi ya viongozi wa chama chake makao makuu, akiwemo Naibu Katibu Mkuu, Hamad Tao, aliendelea kusema kuwa hajanunuliwa, na Rais Kikwete, lakini atahakikisha anampigia debe ili ashinde urais Oktoba mwaka huu.
Watanzania tuache uongo, unafiki na uzandiki, sijanunuliwa na Rais Kikwete, mbona Seif anayempigia debe Rais Karume kuwa aongezewe muda hamsemi amenunuliwa? Ninasema kura zote za urais ziende kwa Rais Kikwete! aliongeza.
Naye Walid Kaborou, ambaye ni mwenyekiti wa taasisi hiyo, alisema wanaosimama na kusema kuwa Rais Kikwete atoswe wanazungumzia kazi ambayo hawajawahi kuifanya. Hawa hawajawahi kuwa marais leo wanasema rais atoswe; hao Mwalimu Nyerere Foundation kati yao nani aliyewahi kuwa rais? Hao ni wachochezi na kwa uchochezi kama huo hatuwezi kufika! alisemea Kaborou.
na Deogratius Temba
JITIHADA za kuhakikisha Rais Kikwete anaendelea kukubalika kwa wananchi na kuchaguliwa zinazidi kushamiri ambapo mama wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) Zitto Kabwe ametangaza kuwa hakuna mtu yeyote mwenye kufaa nafasi hiyo hivi sasa.
Mama huyo, Shida Salum, ambaye ni mwenyekiti wa walemavu, alitangaza kumuunga mkono Kikwete juzi kwenye viwanja vya Temeke, jijini Dar es salaam, alipokuwa kwenye mkutano wa Aman Forum.
Alisema Rais amefanya kazi nzuri ya kuimarisha amani na kuwatetea walemavu hivyo ni vema Watanzania wakampa fursa ya kuongoza kwa kuwa wanasiasa waliopo hivi sasa iwe wa CCM au wa vyama vya upinzani hawajafikia viwango vya kuwania urais.
Ninasema hivi; hakuna mtu anayeweza kuwatetea walemavu kama Rais Kikwete, amewakamata wauaji wa maalbino, na sasa anatutetea zaidi, kura zote za urais ni kwa Rais Kikwete, wapinzani watapata za ubunge tu! alisema.
Aliongeza kuwa wapinzani wanapaswa kujiandaa kumsimamisha mgombea urais mwaka 2015 ili kuepuka matokeo mabaya wanayoweza kuyapata iwapo watamsimamisha mgombea wa urais ili kukabiliana na Kikwete.
Mkutano huo ambao uliongozwa na Mbunge wa Bunge la Afrika ya Mashariki, Walid Aman Kaborou, na pia kuhudhuriwa na wajumbe kutoka vyama vya Tanzania Labour (TLP) na NCCR- Mageuzi, limewashambulia viongozi wa Taasisi ya Mfuko wa Mwalimu Nyerere (MNF) kuwa ni wachochezi.
Akizungumza kwenye mkutano huo uliohudhuriwa na watu wachache, Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema, alisema amejiunga na taasisi ya Aman Forum, kwa sababu amegundua kuwa nchi ina tatizo hasa unapofikia wakati wa uchaguzi wa urais.
Kuna kundi la watu lina njama za kumdhuru au kumsambaratisha Rais Kikwete na serikali yake, wajue kuwa wakifanya hivyo hawatakuwa wamekidhuru chama tawala bali ni Watanzania wote, mimi nimeamua kujiunga na Amani Forum, ili sasa nitangaze vita na kundi hilo, alisema Mrema.
Mrema alibainisha kuwa ameamua kuitetea nchi na hajahongwa wala kununuliwa na mtu yeyote kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakimtuhumu.
Aidha, aliwashambulia makada wa CCM na viongozi wastaafu walioshiriki kuchangia hoja katika tamasha la kumuenzi hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, lililofanyika katika ukumbi wa Karimejee mwishoni mwa mwaka jana kuwa ni wachochezi na wanatakiwa kukamatwa kwa sababu hawana heshima kwa rais wa nchi.
Kuna tamasha la Mwalimu Nyerere, makada wa CCM wamelitumia kama kichaka cha kuendesha uhaini hawa walinunuliwa; wamesema Kikwete amezungukwa na wezi, wanamtukana rais? Nyie CCM mnamtusi kiongozi wenu anayewapeperushia bendera?
Mrema ambaye aliwahi kuibua kashfa ya ufisadi wa kuibiwa kwa sh bilioni 900, ambayo ilimhusisha pia Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, alisema katika miaka minne, Rais Kikwete amefanya mambo makubwa ikiwepo kuruhusu wasaidizi wake wajiuzulu, kwa kuhusishwa.
Hivi mnamtaka afanye maamuzi gani mazito, wakati amekubali rafiki yake aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa ajiuzulu? Serikali si imewajibika? Mnasema mtamtosa kwa kosa gani alilofanya Rais Kikwete?
Mrema aliendelea kusema kuwa suala la ufisadi hata Baba wa Taifa alilishindwa kwa sababu baadhi ya viongozi waliokuwa wakifanya naye kazi walipohusishwa na ufisadi aliwahamisha au kuwaongezea majukumu badala ya kuwawajibisha.
Mwingira aliuza ndege ya serikali, mbona Nyerere alimhamisha na kumpa ukuu wa mkoa wa Arusha? Balozi Mustafa Nyanganyi alinunua kivuko kibovu Mwalimu akampa ubalozi wa Marekani; Rais Kikwete amewapeleka watu mahakamani ninyi mnasema mtamtosa! alishangaa Mrema.
Mrema aliyekuwa amefuatana na baadhi ya viongozi wa chama chake makao makuu, akiwemo Naibu Katibu Mkuu, Hamad Tao, aliendelea kusema kuwa hajanunuliwa, na Rais Kikwete, lakini atahakikisha anampigia debe ili ashinde urais Oktoba mwaka huu.
Watanzania tuache uongo, unafiki na uzandiki, sijanunuliwa na Rais Kikwete, mbona Seif anayempigia debe Rais Karume kuwa aongezewe muda hamsemi amenunuliwa? Ninasema kura zote za urais ziende kwa Rais Kikwete! aliongeza.
Naye Walid Kaborou, ambaye ni mwenyekiti wa taasisi hiyo, alisema wanaosimama na kusema kuwa Rais Kikwete atoswe wanazungumzia kazi ambayo hawajawahi kuifanya. Hawa hawajawahi kuwa marais leo wanasema rais atoswe; hao Mwalimu Nyerere Foundation kati yao nani aliyewahi kuwa rais? Hao ni wachochezi na kwa uchochezi kama huo hatuwezi kufika! alisemea Kaborou.