gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,274
- 20,670
Sasa mama yangu mpenzi gfsonwin, ili kudhihirisha upendo wangu kwako nakuletea zawadi za kufa mtu na wamasai
wawili! Kwanza nimefungasha mabox ya Dodoma wine na zabibu zake! Halafu ninapitia dubai nitakuletea kile kiitwacho 'set
adimu ya mwanamke' yaani hereni, mkufu, bangili, pete, saa, shanga za matumizi ya 'kawaida', zote za dhahabu safi kwa
gramu za kutosha! Nitakulete pia wallet na pochi ambazo hakika kila ubebapo watu hawatachoka kugeuza macho. Hapo
sijazema vile vigauni na viatu kutoka Gucci na Chanel! Haya yote ni sign ya upendo wangu kwako. Siwezi kusahau mikono
yako mwororo ilipokuwa inaniogesha enzi za utoto wangu!
Ronn M nakupenda sana manangu, nisomapo haya najikuta nalia kwa uchungu wa kukukosa. u mwanangu mwema sana kila mara wadogo zako huniuliza kaka Rony yuko wapi nawaambia upo utakuja tu. baba yako Kaizer alipata msongo wa mawazo sana juu yako wewe ila nakushukuru na kufuraah umekuja. njoo mwananu nikukumbatie, nikubusu, niiskie harufu a ngozi yako.
Last edited by a moderator: