Mama Yangu anavunja ndoa za Dada zangu, nifanye nini ili kuzinusuru?

Status
Not open for further replies.

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
56,342
92,618
Hii si Tamthilia na wala si swala la rafiki yangu kama ilivyozoeleka jukwaa hili watu huogopa kusema ni wao ndio wahusika. Hili linaihusu Familia yangu halisi.

Kwa sababu mtandao huu unasomwa na watu wengi sitakuwa wazi kwa 100% ili kuficha identificantion, inshort dada zangu wameolewa lakini nikiangalia kwa jicho la ziada nagunduwa kwamba wao ndio wameoa.

Nitafafanuwa, Mama yangu amekuwa ni Dictactor mno wa kuingilia ndoa zao, kiasi kwamba wakiyumba kidogo kimaisha yeye uingilia kati kuwaamishia Dada zangu kwenye baadhi ya nyumba tunazomiliki hapa Dar na kupelekea waume zao kuwa na Inferiority Complex.

Lakini hii ya sasa ndio kali zaidi, mmoja ya Dada zangu yeye amepewa appartment ambayo ipo ndani ya same compound wanayoishi Wazazi wangu na ndio msingi wa Thread hii.

Nimepokea malalamiko kutoka kwa shemeji yangu jinsi anavyonyanyaswa na Dada yangu na thanks God huyu jamaa kwa sasa yupo mkoa katika kuzichanga lakini ameniahidi kwamba hawezi kukanyaga pale nyumba mpaka mke wake ahame na yeye uwezo wa kulipa kodi anao, kama mwanzoni walivyokuwa wamepanga nyumba tofauti.

N;b. Mimi nina maisha yangu na ninakaa kwangu, sijaelewa labda ukwasi huu walionao hawa wazazi wangu ndio unawatia upofu hawa madada au ni kipi hasa?

Labda tu kwa ufupi hapo naomba ushauri maana ninachopanga kukifanya nikiwa kama kiongozi wa Familia kinaweza kuzuwa chuki na nisielewane na mama yangu kwa rest of my life.
 
sema kwanza icho ulichopanga kukifanya ili 2weze kuchangia vzri zaidi
 
Hii si Tamthilia na wala si swala la rafiki yangu kama ilivyozoeleka jukwaa hili watu huogopa kusema ni wao ndio wahusika. Hili linaihusu Familia yangu halisi.

Kwa sababu mtandao huu unasomwa na watu wengi sitakuwa wazi kwa 100% ili kuficha identificantion, inshort dada zangu wameolewa lakini nikiangalia kwa jicho la ziada nagunduwa kwamba wao ndio wameoa.

Nitafafanuwa, Mama yangu amekuwa ni Dictactor mno wa kuingilia ndoa zao, kiasi kwamba wakiyumba kidogo kimaisha yeye uingilia kati kuwaamishia Dada zangu kwenye baadhi ya nyumba tunazomiliki hapa Dar na kupelekea waume zao kuwa na Inferiority Complex.

Lakini hii ya sasa ndio kali zaidi, mmoja ya Dada zangu yeye amepewa appartment ambayo ipo ndani ya same compound wanayoishi Wazazi wangu na ndio msingi wa Thread hii.

Nimepokea malalamiko kutoka kwa shemeji yangu jinsi anavyonyanyaswa na Dada yangu na thanks God huyu jamaa kwa sasa yupo mkoa katika kuzichanga lakini ameniahidi kwamba hawezi kukanyaga pale nyumba mpaka mke wake ahame na yeye uwezo wa kulipa kodi anao, kama mwanzoni walivyokuwa wamepanga nyumba tofauti.

N;b. Mimi nina maisha yangu na ninakaa kwangu, sijaelewa labda ukwasi huu walionao hawa wazazi wangu ndio unawatia upofu hawa madada au ni kipi hasa?

Labda tu kwa ufupi hapo naomba ushauri maana ninachopanga kukifanya nikiwa kama kiongozi wa Familia kinaweza kuzuwa chuki na nisielewane na mama yangu kwa rest of my life.

Mkuu, kama vile tatizo la dada zako na shemeji zako unalijua by 100%; tatizo ni kwamba hujiamini. Chukua hatua. Pitia hizo rangi hapo juu.
 
Mkuu pole sana kwa hayo matatizo.. Sio madogo hayo..
Ninavyoona mie hapo kwanza mama anaweza kuwa tatizo from ur perspective.. But from ur mother's perspective anajiona yuko sahihi.. Mama anawapenda na anapenda watoto wake waishi vizuri.. Kitu ambacho cijakielewa labda Mkuu
Matola unapomuuliza au kumshauri kuhusu hali hiyo anasemaje..?
 
Hao dada zako wanaumri gani mpaka wanashwindwa kuheshimu waume zao? au hizo nyumba kwani ni zao mpaka wajisahau
hivyo? nyumba ya mama na baba mie siamini kama ni yakwangu yangu ni ile ntakayo jenga na mumewangu au ntakayo jenga mwenyewe hao nii ulimbukeni walokua nao na dharau, Mume wangu tunaishi kwenye nyumba yangu mbona tuko na furaha na hakuna mtu anaejua ktk familia yetu na sio kama yeye hana nyumba zake.
 
Mkuu, kama vile tatizo la dada zako na shemeji zako unalijua by 100%; tatizo ni kwamba hujiamini. Chukua hatua. Pitia hizo rangi hapo juu.
Aisee ukiona mtu anashare vitu personal kama hivi na hasa mtu wa kariba yangu basi ujuwe tatizo ni kubwa kuliko unavyolitazama, siyo kwamba sijafanya effort zozote, na ujiulize kwa nini sijamtaja Baba na yuko hai na wanaishi pamoja.
 
Waeleze dada zako ukweli kuwa wameolewa hvy wakae na waume zao hukohuko hata kama wanakula ugali wa chumvi wavumilie tu na wawaheshimu waume zao mana hayo ndio mapenzi ya kweli.
 
Hii si Tamthilia na wala si swala la rafiki yangu kama ilivyozoeleka jukwaa hili watu huogopa kusema ni wao ndio wahusika. Hili linaihusu Familia yangu halisi.

Kwa sababu mtandao huu unasomwa na watu wengi sitakuwa wazi kwa 100% ili kuficha identificantion, inshort dada zangu wameolewa lakini nikiangalia kwa jicho la ziada nagunduwa kwamba wao ndio wameoa.

Nitafafanuwa, Mama yangu amekuwa ni Dictactor mno wa kuingilia ndoa zao, kiasi kwamba wakiyumba kidogo kimaisha yeye uingilia kati kuwaamishia Dada zangu kwenye baadhi ya nyumba tunazomiliki hapa Dar na kupelekea waume zao kuwa na Inferiority Complex.

Lakini hii ya sasa ndio kali zaidi, mmoja ya Dada zangu yeye amepewa appartment ambayo ipo ndani ya same compound wanayoishi Wazazi wangu na ndio msingi wa Thread hii.

Nimepokea malalamiko kutoka kwa shemeji yangu jinsi anavyonyanyaswa na Dada yangu na thanks God huyu jamaa kwa sasa yupo mkoa katika kuzichanga lakini ameniahidi kwamba hawezi kukanyaga pale nyumba mpaka mke wake ahame na yeye uwezo wa kulipa kodi anao, kama mwanzoni walivyokuwa wamepanga nyumba tofauti.

N;b. Mimi nina maisha yangu na ninakaa kwangu, sijaelewa labda ukwasi huu walionao hawa wazazi wangu ndio unawatia upofu hawa madada au ni kipi hasa?

Labda tu kwa ufupi hapo naomba ushauri maana ninachopanga kukifanya nikiwa kama kiongozi wa Familia kinaweza kuzuwa chuki na nisielewane na mama yangu kwa rest of my life.
kwna kaka hapo red naomba utubu maana unapoongele kuhusu mama najua thamani yake na nimeumia kumpoteza hapa nilipo naumwa mwili wote hadi utumbo nasikia unashake ..nina maumivu yasiyoelezeka
back to topic..kwanza unatakiwa ujue wanawake wengi ni wabinafsi na wachoyo sana..especialy wakiwa na hela
mama yako anataka jamii imuone watoto wake wakike wameolewa na waonekane wanajiweza ..wamama wengi wanapenda kujishow off kwa ndoa za watoto wao hata kama hela wanatoa wenyewe,achekwe watoto wake wameolewa wanauza chapati asubuhi? au mume wa mwanae ni dereva tex? wewe? sasa the worst party ni pale hao wume wanapokubali kuwa mazoba .... na kukubali hizo offer za mamamkwe za kununuliwa hadi......
kama anataka kuwasaidia awape hata mtaji hukohuko kwao. big up kwa huyo shem wenu mmoja alogoma kuhamia hapo kwenu tena mwambie aoe mke mwingine uko alipo
 
Hao dada zako wanaumri gani mpaka wanashwindwa kuheshimu waume zao? au hizo nyumba kwani ni zao mpaka wajisahau
hivyo? nyumba ya mama na baba mie siamini kama ni yakwangu yangu ni ile ntakayo jenga na mumewangu au ntakayo jenga mwenyewe hao nii ulimbukeni walokua nao na dharau, Mume wangu tunaishi kwenye nyumba yangu mbona tuko na furaha na hakuna mtu anaejua ktk familia yetu na sio kama yeye hana nyumba zake.
kiumri wote wako under 30 years, najuwa sana kwa sisi ambao tuko over 35 wengi unakuwa ndio unarekebisha maisha sasa nadhani ni wakati kama umeowa kama ni msoto ule na mkeo na siyo kuwa na mke asiyejuwa msoto ni nini.

Nadhani Mama yangu asichokijuwa wale si watoto tena bali aifuate na aisome vizuri Biblia ambayo anaiamini Inayosema kwamba Mke atamuacha Mama yake na Baba yake na ataambatane na mume wake na watakuwa mwili mmoja. ndio maana naamini wanaojazana makanisani na misikiti 99% ni unafki mtupu.
 
kama anataka kuwasaidia awape hata mtaji hukohuko kwao. big up kwa huyo shem wenu mmoja alogoma kuhamia hapo kwenu tena mwambie aoe mke mwingine uko alipo
Huu ni ushauri mwema sana, ni kama vile unalijuwa tatizo lilivyo deep.
 
Nadhani Mama yangu asichokijuwa wale si watoto tena bali aifuate na aisome vizuri Biblia ambayo anaiamini Inayosema kwamba Mke atamuacha Mama yake na Baba yake na ataambatane na mume wake na watakuwa mwili mmoja. ndio maana naamini wanaojazana makanisani na misikiti 99% ni unafki mtupu.

Mkuu analisemeaje hilo la kuingilia kwenye nyumba za watoto wake..? Au hamjawahi kum-confront kwa issue hiyo..?
 
Hii si Tamthilia na wala si swala la rafiki yangu kama ilivyozoeleka jukwaa hili watu huogopa kusema ni wao ndio wahusika. Hili linaihusu Familia yangu halisi.

Kwa sababu mtandao huu unasomwa na watu wengi sitakuwa wazi kwa 100% ili kuficha identificantion, inshort dada zangu wameolewa lakini nikiangalia kwa jicho la ziada nagunduwa kwamba wao ndio wameoa.

Nitafafanuwa, Mama yangu amekuwa ni Dictactor mno wa kuingilia ndoa zao, kiasi kwamba wakiyumba kidogo kimaisha yeye uingilia kati kuwaamishia Dada zangu kwenye baadhi ya nyumba tunazomiliki hapa Dar na kupelekea waume zao kuwa na Inferiority Complex.

Lakini hii ya sasa ndio kali zaidi, mmoja ya Dada zangu yeye amepewa appartment ambayo ipo ndani ya same compound wanayoishi Wazazi wangu na ndio msingi wa Thread hii.

Nimepokea malalamiko kutoka kwa shemeji yangu jinsi anavyonyanyaswa na Dada yangu na thanks God huyu jamaa kwa sasa yupo mkoa katika kuzichanga lakini ameniahidi kwamba hawezi kukanyaga pale nyumba mpaka mke wake ahame na yeye uwezo wa kulipa kodi anao, kama mwanzoni walivyokuwa wamepanga nyumba tofauti.

N;b. Mimi nina maisha yangu na ninakaa kwangu, sijaelewa labda ukwasi huu walionao hawa wazazi wangu ndio unawatia upofu hawa madada au ni kipi hasa?

Labda tu kwa ufupi hapo naomba ushauri maana ninachopanga kukifanya nikiwa kama kiongozi wa Familia kinaweza kuzuwa chuki na nisielewane na mama yangu kwa rest of my life.

Wazazi wamekuwa chanzo cha migogoro ktk ndoa nyingi, hasa kama hawa wazazi wana wadhifa au vijisenti mifukoni, kuna my bro nae ametendwa the same na mkwewe yaani anaishi maisha ya hofu na the same amepewa Apart kwenye milki ya mkwewe na kila ndg zetu akifika anachambuliwa kama karanga or mara mchafu, mshamba, mwizi ilimradi asikose sababu ya kukukera uondoke.....Nini cha kufanya......Sisi kama familia tuliamua kutojihusisha na mambo yanayowahusu huku tukidumisha undugu na bro kwani ni ngumu kumtupa....Upande wako unaposema kuja jambo utafanya unaleta hofu kiasi, ila kaa kitako na mama yako mweleze madhara na faida ya hayo anayoyafanya kwani mwisho hao wanaume wakichoka watasepa na kumwachia watoto kama wakati anasomesha....Maisha ya ndoa yanahitaji mawazo ya mke na mme na sio mke+mzazi na mme.Note; Kwenye ndoa akishaongezeka mtoa maamuzi mwingine nje ya wanandoa toka upande wowote mwanamme au mwanamke hiyo ndoa imejichimbia kaburi kusubiri mauti
 
Huu ni ushauri mwema sana, ni kama vile unalijuwa tatizo lilivyo deep.
hivi utakaaje na mumeo kwenu? hao dada zako bwana ,yaani huyo shem wako ni mstaaarabu kweli hivi angefanyeje mfano mapenzi kwenye ardhi ya wakwe? huyo sister haoni hata aibu jamani? mwambie hakunaga bwana ...
 
Mhhhhhhhhhhh!!!!!!! Kumbe Mama Lara 1 wako wengi kweli! Hapa nilipo kanifanya niahidi nikiolewa tunaenda wote!!!!!! Yaaani badala akakae kwa dume la mbegu lake, hataki kusikia habari hizo, yeye na mimi tu!

Back to Topic Hao wanaume wana makosa ya kukosa sauti ndani ya nyumba zao! Hapo hata mama yako asingekuwepo dada zako wangewapeleka peleka tu! Kinchotakiwa wajikomboe na utumwa na kuwa VIDUME vya nyumba! Baaaaaaass! Wewe mwambie shemu akaze tuu sio kuwa legelege!

Kuna watu watabe, anaoa kwa pedeshee ila mkewe hamwambiii kitu! Mwanzo mwisho His words are final, hata mama mkwe anaona noma kuingilia!!!!!!!!!!!! Utagombana na mama yako bureeeeeeeee!!!!! Ila kama shemu deka deka untd atabakia hivo hivo!
 
Matola anataka amilikishwe kila kitu! Hofu yake hawa jamaa waliooa dada zake watapewa hizo mali kimoja! Jamaa anamalizia ETI YEYE NI KICHWA CHA NYUMBA! Dingi vipi kwani? Yeye sio kichwa?
 
Angalia na wewe asije akakuamuru urudi kukaa nyumbani, maana inaonekana she likes bossing people around
 
Mkuu analisemeaje hilo la kuingilia kwenye nyumba za watoto wake..? Au hamjawahi kum-confront kwa issue hiyo..?
Kuna siku huyu ambaye ndio kamuhamishia kwenye same Compound, aligombana na Mumewe wakati wamepanga nyumba sehemu nyingine, basi huyu Dada yangu akampigia simu Mama yake kwamba anapigwa na Mumewe basi Mother akawasha gari usiku ule ule na kwenda kumchukuwa binti yake na alikuwa ana Mimba.

Siku ya tatu mimi nilipopata taarifa nikasema nikenda nyumbani kwa Wazazi wangu sitaki nimkute Dada yangu, nataka apeklekwe akakae kwa ndugu wa Mumewe au kwa Mshenga mpaka watakapo patana, lakini nilipuuzwa.

hivi utakaaje na mumeo kwenu? hao dada zako bwana ,yaani huyo shem wako ni mstaaarabu kweli hivi angefanyeje mfano mapenzi kwenye ardhi ya wakwe? huyo sister haoni hata aibu jamani? mwambie hakunaga bwana ...
Mama yangu ni tatizo, na Baba naona kama kashikwa na Mother sijamuona akiwa yuko serious na mambo haya, labda wanawaza urithi wao mapema u never know.
 
kwna kaka hapo red naomba utubu maana unapoongele kuhusu mama najua thamani yake na nimeumia kumpoteza hapa nilipo naumwa mwili wote hadi utumbo nasikia unashake ..nina maumivu yasiyoelezeka
back to topic..kwanza unatakiwa ujue wanawake wengi ni wabinafsi na wachoyo sana..especialy wakiwa na hela
mama yako anataka jamii imuone watoto wake wakike wameolewa na waonekane wanajiweza ..wamama wengi wanapenda kujishow off kwa ndoa za watoto wao hata kama hela wanatoa wenyewe,achekwe watoto wake wameolewa wanauza chapati asubuhi? au mume wa mwanae ni dereva tex? wewe? sasa the worst party ni pale hao wume wanapokubali kuwa mazoba .... na kukubali hizo offer za mamamkwe za kununuliwa hadi......
kama anataka kuwasaidia awape hata mtaji hukohuko kwao. big up kwa huyo shem wenu mmoja alogoma kuhamia hapo kwenu tena mwambie aoe mke mwingine uko alipo

Kwenye Bold nakupa pole sana...ila tafadhali sana na mungu akusaidie jaribu kusahau yaliyopita japo pengo limebaki ila mungu ndie atakaeliziba, jitaidi siku ya kukaribisha mwaka mpya uwe na maandalizi ya kuuacha mwaka 2012 ambao naamini ulikusononesha sana..Umeandika maneno yaliyojaa huzuni sana na wataalam wa Saikolojia wanasema ukiishi na huzuni kali kwa kipindi kirefu unapata madhara ya muda mrefu zaidi. Penye underline hawa wamama wanafanya hivyo ili kutengeneza hali ya ubabe kwa watoto wao, hasa wale wanawake waliteswa sana na waume zao na kuhisi umasikini wao ndio uliochangia watawajengea watoto wao uwezo ili wajiamini huku watoto nao wakivunja ndoa zao pasi ya kujua.
 
Kumbe mama yako ana akili kama yako. No wonder....
Akili za Kibonde utazijuwa tu.

Matola anataka amilikishwe kila kitu! Hofu yake hawa jamaa waliooa dada zake watapewa hizo mali kimoja! Jamaa anamalizia ETI YEYE NI KICHWA CHA NYUMBA! Dingi vipi kwani? Yeye sio kichwa?
Aisee Baba yangu na Mama yangu wote wapo hai, nina maisha yangu na mimi siishi katika kuamini swala la kurithi, kwanza vijana ndio tunaokufa zaidi kuliko wazee.

Ni Mawazo ya kimaskini sana kwa kijana wa kileo kuwaza mambo ya kurithi badala ya kufanya kazi kwa bidii.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom