Mama Wassira Aiaga CCM Rasmi....

kiwatengu

Platinum Member
Apr 6, 2012
17,627
14,749
Hii habari ilipaswa leo iwe ni habari kubwa kidogo!

Katika harakati za kuendelea kwenye ukombozi, Jana tumeshuhudia watu wawili
Muhimu sana katika familia za CCM wakijiunga na Chadema.

Aliyekuwa DC wa Mbozi Bwana Kimolo na Mama Rachel Wassira!
Ndio waliyofanya maamuzi sahii siku ya jana kwa kuamua kuvua magamba na kuvaa magwanda.

Wakati Mama Wassira anajiunga na Chadema jana alisema hiki chama kina MUNGU!! Na hana sababu inayomfanya aendelee kuwa CCM.

Hongera sana Mama Wassira, na kwa kupitia wewe Tunaamini Mzee George Wassira atakuja huku pia..

Hongera Pia Mzee Kimolo.

 
Si mlisema majina ya watu sio issue ila chama kama chama ndio mpango mzima?????!!!!
Au majina yana umuhimu wakati wa kuingia tu wakati wa kutoka tunavua ubatizo????!!!!!


Thubutu yeeenu mkiwa waongo muwe na kumbukumbu pia!!!!!
 
huyu kimolo ni yule aliyekuwa analewa mpaka anaokotwa au ni kimolo yupi.
 
Hii habari ilipaswa leo iwe ni habari kubwa kidogo!

Katika harakati za kuendelea kwenye ukombozi, Jana tumeshuhudia watu wawili
Muhimu sana katika familia za CCM wakijiunga na Chadema.

Aliyekuwa DC wa Mbozi Bwana Kimolo na Mama Rachel Wassira!
Ndio waliyofanya maamuzi sahii siku ya jana kwa kuamua kuvua magamba na kuvaa magwanda.

Wakati Mama Wassira anajiunga na Chadema jana alisema hiki chama kina MUNGU!! Na hana sababu inayomfanya aendelee kuwa CCM.

Hongera sana Mama Wassira, na kwa kupitia wewe Tunaamini Mzee George Wassira atakuja huku pia..

Hongera Pia Mzee Kimolo.


Kuingia na kuishi kwenye nyumba yenye misingi imara ni maamuzi sahihi sana. CHADEMA ni kwa wote wenye mapenzi mema na Tanzania. Kama mtu yupo CHADEMA kwa sababu kuna Dr Slaa, Mzee Mtei, Mbowe, Zito, Msigwa, Mnyika, Mdee nk, atoke haraka sana maana amekosea mlango.

Tuliopo CHADEMA ni wale tu tunaoamini ktk katiba ya CHADEMA jinsi inavyotutaka wanachama tuwe.

KARIBUNI SANA.
 
Back
Top Bottom