Wale wanasema ndoa ni pesa basi wazidi kusomaa hii hali nadhani vifo vimefuwatanaWana JF,
Mama mmoja mke wa mzee maarufu wa Kiti Moto ya kwa Mzava, amekutwa amefariki na damu zimetapataa sakafuni. Haijulikani chanzo kilichopelekea kifo chake.
Baada ya kifo, mme hapatikani kwenye simu yake, gari la mme limekutwa limetelekezwa getini na halijafungwa. Huyu mama alikuwa mfanyakazi wa TRA Samora karibu na Salamander.
Mzava ni mtu maarufu kule Bunju kwa utaalam wa kupika kitimoto ambaye awali alikuwa wanafanya kiti moto Ubungo shekilango dagaadagaa.
Mama anaitwa Irene Mzava, alihamishwa kutoka TRA Temeke, akaletwa Tegeta. Wanyetishaji wanadai, waliandaa safari kwenda Moshi saa tisa. Lakini safari ikageuka shubiti, baba anaonekana alimpiga na kitu kizito ikawa ndio mwisho.
Baba akaenda baa akawaomba wahudumu wampatie mauzo ili apelekwe mgonjwa hospital, basi akafika getini na kutelekeza gari, akaingia ndani katoa gari jipya aina Toyota Harrier new model 2015 inaitwa matako ya nyani, gari ilikuwa full tank kwa ajiri ya safari na imepakia vitu, baada ya mauaji akaipiga mogul mpaka Moshi inawezekana alifika saa 11, akaitelekeza gari mpya na kutokomea. Yeye na mke wake ni majuzi walitoka kwenye msiba wa mama wa mauaji. R.i.P Mama Irene Mzava.
View attachment 2063586