Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,189
- 4,103
Polisi wilayani Serengeti mkoani Mara wamemkamata Kumari Mongita (23) mmoja kati ya wawili wanaodaiwa kumbaka mama mwenye miaka 58, mkazi wa Miseke ambaye amelazwa hospitali Teule ya Nyerere kwa ajili ya matibabu.
Tukio hilo linadaiwa kutokea Aprili 6 usiku katika kitongoji cha Senta wakati mama huyo, mkazi wa kitongoji cha Majengo akitoka kutafuta tumbaku na mboga na inadaiwa watuhumiwa walimfuatilia kwa nyuma na kumkaba na kumfanyia ukatili huo.
Mganga mkuu wa hospitali ya Nyerere, Tanu Warioba alidai mama huyo ana maumivu kifuani na sehemu nyingine za mwili. “Anadai baada ya kumwangusha walimvua nguo na mmoja akambana kifua, mwingine alimwingilia wakifanya kwa zamu kisha wakamtupa kwenye kajito”
Chanzo: Mwananchi
Tukio hilo linadaiwa kutokea Aprili 6 usiku katika kitongoji cha Senta wakati mama huyo, mkazi wa kitongoji cha Majengo akitoka kutafuta tumbaku na mboga na inadaiwa watuhumiwa walimfuatilia kwa nyuma na kumkaba na kumfanyia ukatili huo.
Mganga mkuu wa hospitali ya Nyerere, Tanu Warioba alidai mama huyo ana maumivu kifuani na sehemu nyingine za mwili. “Anadai baada ya kumwangusha walimvua nguo na mmoja akambana kifua, mwingine alimwingilia wakifanya kwa zamu kisha wakamtupa kwenye kajito”
Chanzo: Mwananchi