Mama Suzan Kolimba, nani alikutuma uunge mkono juhudi za mabeberu za kutaka tusifyatue kwa kwenda mbele?

dikteta2020

JF-Expert Member
Aug 14, 2018
595
3,990
Naona sasa mama yangu mambo yamekufika hapa. Japo kuwa kiubinadamu huko duniani ulikuwa sawa lakini hukuweza kusoma alama za nyakati. Hukuweza kumjua bwana mkubwa anataka nini.

Nakumbuka wakati mmoja JK aliwahi kutangaza idadi ya watu ambapo alishtuka sana baada ya kugundua kuwa mwaka 2012 wa Tz tulikuwa tumeongezeka sana na ndipo akaanzisha mpango wa kuhamasisha uzazi wa mpango. Wachumi tunaelewa na tutaendelea kuelewa athari za kufyatua hovyo hovyo kutokana na umasikini wetu.

Watu bado tuna omba omba sana halafu huku tunahamasisha ufyatuaji tena kwa kwenda mbere?

Zile NGOs ulizosema kuwa kuzuiwa kwao kutoa somo la kufyatua kwa mpango tutajiathiri wenyewe hatimaye zimekupeleka lupango bila bango. Pole sana kwa hilo.

Mzee anataka tufyatue na hapangiwi akishasema. Kina Ummy ngoma wanajua kuicheza bila kibao koma. Bado wapo wapo mama, bado wapo wapo sana. Nasi juhudi tunaziunga kwa kwenda kilimanjaro ingawa bado tupo chini ya mtaro kama mtatiro.
 
Ila kufyatua watoto wala siwezi unga mkono, hata niwe usingizini ukinikurupusha siwezi kubali pia

Ila kwa wasukuma nadhani ndio furaha yao kuzaa sana, ndio desturi ya kabila. Sasa tusiambukizane tabia, sisi wengine tukizaa sana ni watatu tu na hii kulingana na hali ya maisha itakayokuwa inaendelea wakati huo
 
Nilikuaga namchukuliaga Jiwe labda kuna mahali hua anakosea bahati mbaya tu kibinadamu,ila kuhusu swala la kuongezeka idadi ya watu ndio nikajua Jiwe ni hamnazo mazima !

Ukisikia TZ kupata accident basi ni Jiwe!
Kila MTU angebaki kwenye fani yake ingekuwa poa, aliyesoma kemia ajui uchumi, ajui madhara ya kufyatua,kusomesha no watu,chuki kwa matajiri,kodi kubwa,chochote kifanywacho kwa maagizo ya mwanasiasa serikali hio hio ndo inayoathirika.
 
Naona sasa mama yangu mambo yamekufika hapa. Japo kuwa kiubinadamu huko duniani ulikuwa sawa lakini hukuweza kusoma alama za nyakati. Hukuweza kumjua bwana mkubwa anataka nini.

Nakumbuka wakati mmoja JK aliwahi kutangaza idadi ya watu ambapo alishtuka sana baada ya kugundua kuwa mwaka 2012 wa Tz tulikuwa tumeongezeka sana na ndipo akaanzisha mpango wa kuhamasisha uzazi wa mpango. Wachumi tunaelewa na tutaendelea kuelewa athari za kufyatua hovyo hovyo kutokana na umasikini wetu.

Watu bado tuna omba omba sana halafu huku tunahamasisha ufyatuaji tena kwa kwenda mbere?

Zile NGOs ulizosema kuwa kuzuiwa kwao kutoa somo la kufyatua kwa mpango hatimaye zimekupeleka lupango bila bango. Pole sana kwa hilo.

Mzee anataka tufyatue na hapangiwi akishasema. Kina Ummy ngoma wanajua kuicheza bila kibao koma. Bado wapo wapo mama, bado wapo wapo sana!
Unatumika wewe siyo bure, eti Uzazi wa mpango, sababu umasikini. Ni mawazo ya kijinga kabisa, nani alikuambia kwamba watu wengi ni chanzo cha umasikini? Huo ni utafiti wa mabeberu, wa kimagharibi, ambao wanatumia vi NGOs na wakiwanunua watu kwa viposho uchwara ili wajikute wamenunuliwa kiakili bila kujua, kama wingi wa Watu ni chanzo cha umasikini, basi China ingekuwa masikini kupita nchi zote Duniani, kwa sababu idadi ya watu wake ni sawa na Waafrika wote na Simu zetu. Rwanda na Burundi zingekuwa tajiri kupundukia kwa kuwa na idadi ndogo za watu. Uzazi wa mpango ni mikakati ya wazungu kutafutia ajira watu wao kupitia NGOs. Hivyo ni Upumbavu na ujinga kutumika na wazungu kwa kuaminishwa kwa tafiti feki na za kipumbavu na kijinga. Mtu yeyote ukimuona anapinga ushauri wa JPM ambapo alisema watu wazae watoto ambao wanaweza kuwalea, wasipangiwe, eti zaa 2, 3, au 4 tu. Kama unaweza kuwatunza zaa kadri ya uwezo wako. Cha muhimu tuchape kazi tu. Hata mimi upumbavu wa kufuata mawazo ya kijinga ya Wazungu siyakubali kabisa.
 
Ili kwenda sawa na midundo ya ngoma,yatakiwa ucheze jinsi ngoma inavolia,kwenda sawa yatakiwa uwe na itikadi za kijamaa,uzamani,ukale,ni kusubiri maelekezo,zaidi usifu na kuabudu. Ukijifanya kutumia taaluma yako unakwenda na maji. Kama huwezi kuwa mnafiki,una hofu ya Mungu,una utu,ngoma itakushinda kucheza.
 
Unatumika wewe siyo bure, eti Uzazi wa mpango, sababu umasikini. Ni mawazo ya kijinga kabisa, nani alikuambia kwamba watu wengi ni chanzo cha umasikini? Huo ni utafiti wa mabeberu, wa kimagharibi, ambao wanatumia vi NGOs na wakiwanunua watu kwa viposho uchwara ili wajikute wamenunuliwa kiakili bila kujua, kama wingi wa Watu ni chanzo cha umasikini, basi China ingekuwa masikini kupita nchi zote Duniani, kwa sababu idadi ya watu wake ni sawa na Waafrika wote na Simu zetu. Rwanda na Burundi zingekuwa tajiri kupundukia kwa kuwa na idadi ndogo za watu. Uzazi wa mpango ni mikakati ya wazungu kutafutia ajira watu wao kupitia NGOs. Hivyo ni Upumbavu na ujinga kutumika na wazungu kwa kuaminishwa kwa tafiti feki na za kipumbavu na kijinga. Mtu yeyote ukimuona anapinga ushauri wa JPM ambapo alisema watu wazae watoto ambao wanaweza kuwalea, wasipangiwe, eti zaa 2, 3, au 4 tu. Kama unaweza kuwatunza zaa kadri ya uwezo wako. Cha muhimu tuchape kazi tu. Hata mimi upumbavu wa kufuata mawazo ya kijinga ya Wazungu siyakubali kabisa.
Masikini wanafanya Kazi?
 
labda tukifyatua tutauza rasilimali watu nchi nyingine watakodi watu wetu vitani mstari wa mbele,...otherwise does not compile we economics principle...
 
Huyu mtu atatuacha tukiwa taabani kwa kila kitu kuanzia madeni, hali duni ya maisha, n.k.
hebu geuka nyuma angalia amepiga hatua ngapi tufike anakotuburuza na tizama MBEREEE bado hatua ngapi tufike tukiwa hoiii???
 
Jamani, hebu tusemeni ukweli hapa, kama unauwezo wa kulea pesa ipo basi zaa utakavyo, ila ka unataka kuchangia mahouse boy, na wafagia barabara, na madada poa, na , huna nyumba huna kibanda, msosi wako wa siku tu ngumu, usipotunza makonda anakuita, mshahara wako laki na nusu, hujanunua umeme, hujalipia maji, wakiugua vipi, mambo mengine kupata majibu bwana
 
The total population in Tanzania was estimated at 52.6 million people in 2017, according to the latest census figures. Looking back, in the year of 1960, Tanzania had a population of 10.1 million people.

Nimeona hiyo data ..... nimechoka mwenyewe. Yaani kwa miaka 58 tumeongezeka zaidi ya mara 5. Kwa jinsi tunavyozaliana au kufwatua kama mwenyewe anavyodai ............ bado tu hajaridhika na huu ufwatuaji wa sasa!!
 
41 Reactions
Reply
Back
Top Bottom