Mama Samia: Wananchi wanaichukia Serikali kwa sababu ya rushwa

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kukithiri kwa rushwa nchini kumewafanya wananchi kuichukia Serikali.

Akizungumza leo (Alhamisi) katika mkutano wa kimataifa unaohusu mapambano dhidi ya rushwa jijini Dar es Salaam, Suluhu amesema Serikali imejidhatiti vilivyo na kwamba itaendelea kupambana na rushwa kwa nguvu zake zote.

Amesema kwa kuwa rushwa hufanyika kwa siri, mapambano dhidi yake yanahitaji ushirikiano mkubwa baina ya Serikali, wadau wengine na wananchi katika kuitokomeza.

"Serikali yetu chini ya Rais John Magufuli imepania kupambana na rushwa kwa namna yoyote ile na tayari ipo mikakati tuliyoiweka kwa ajili ya suala hili, " amesema.
 
Huyu mama (Makamu wa Rais) nimetokea kumkubali sana siku za hivi karibuni, namuona mwenye mapenzi ya kimama kwa Watanzania wake, anaongea kwa staha na kuonya kama mzazi wakati huo huo kiongozi.
 
Bora kasema ukweli wenzake hawaishi kutengeneza uongo na TWAWEZA
 
Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kukithiri kwa rushwa nchini kumewafanya wananchi kuichukia Serikali.

Si kweli Mama Samia, unatafuta kujifariji tu hapa. Wananchi wanaichukia serikali kwa sababu ya staili yenu ya uongozi katika hii awamu ya tano, wewe na Magufuli na chama chenu CCM.

Kwani rushwa imeanza leo? Infact kama ni kuichukia serikali kwa sababu ya rushwa basi serikali ingechukiwa sana enzi za Mwinyi na Kikwete, awamu zilizoongoza kwa rushwa.
 
Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kukithiri kwa rushwa nchini kumewafanya wananchi kuichukia Serikali.

Akizungumza leo (Alhamisi) katika mkutano wa kimataifa unaohusu mapambano dhidi ya rushwa jijini Dar es Salaam, Suluhu amesema Serikali imejidhatiti vilivyo na kwamba itaendelea kupambana na rushwa kwa nguvu zake zote.

Amesema kwa kuwa rushwa hufanyika kwa siri, mapambano dhidi yake yanahitaji ushirikiano mkubwa baina ya Serikali, wadau wengine na wananchi katika kuitokomeza.

"Serikali yetu chini ya Rais John Magufuli imepania kupambana na rushwa kwa namna yoyote ile na tayari ipo mikakati tuliyoiweka kwa ajili ya suala hili, " amesema.

Amesahahu kusema CHUKI,VISASI na UBAGUZI pia vimetufanya tuichukie kwa 100% serikali yao ya awamu ya tano.Wajichunguze
 
Huyu mama ni mtu mkweli apepesi macho. Kiukweli sisi wanaccm ambayo ndo imeunda serikali inachukiwa sana na wananchi sijui 2020 itakuwaje
 
Sababu ninyingi siyo rushwa tuu! Ubaguzi kwenyekazi,ubabe na udikteta,uwongo hasa kwenye bajeti,kutojali na kujijali Wao ikiwa ni pamoja na kujilipa vizuri,kutoshirikishwa kwenye maamuzi nk. nk.
 
Mama na ubabe/uonevu unaofanywa na ma DC na maRC wakisaidiwa na polisi ni zaidi ya rushwa

Wamepiga sana walemavu ambao hata kukimbia hawawezi?Mbona askari wanakula sana rushwa lakini sijachukia kama watu wakionewa
 
Back
Top Bottom