Mama Salma Kikwete, Wewe Ni Mtumishi wa Serikali?

Buchanan

JF-Expert Member
May 19, 2009
13,199
1,969
mama-salma-742819.jpg


Ni kutokana na kutumia raslimali za Serikali wakati wa kumnadi mumewe kuingia Ikulu wakati yeye si mtumishi wa serikali!

KAMPENI za uchaguzi mkuu zimezidi kunoga baada ya mgombea urais wa Chadema, Dk Slaa kumgeukia mke wa Rais Jakaya Kikwete akieleza kuwa anatumia vibaya rasilimali za nchi kumpigia kampeni mumewe huku akimtaka katibu mkuu wa CCM, Yusuph Makamba aeleze kisa cha kufukuzwa ualimu mkuu wa shule ya msingi.

Kwa muda mrefu Salma Kikwete, mke wa Rais Kikwete na ambaye pia ni mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (Wama), amekuwa katika ziara kwenye mikoa mbalimbali, jambo ambalo limekuwa likitafsiriwa kuwa anafanya ziara za kampeni kwa ajili ya mumewe. Kwa sasa yuko mkoani Manyara.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni, Dk Slaa ambaye ameripotiwa kuwa na makombora 20 kwa ajili ya kuimaliza CCM, alisema kitendo cha mke huyo wa rais kumpigia kampeni kwa kutumia rasilimali za umma ni ufisadi.

“Mke wa rais si rais," alisema Dk Slaa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Kwara ulio Babati Mjini.

"Mama Salma anatembea na askari wa serikali; magari ya serikali na wakuu wa mikoa na wilaya. Anatumia fedha za Ikulu kwa sababu walinzi wake wanalipwa na Ikulu. Huu ni ufisadi.”

Dk Slaa, ambaye alikuwa mbunge wa Karatu kwa tiketi ya Chadema), aliongeza kusema: “Nimepita huko nimeambiwa (mke wa rais) anatembea na msafara wa magari 20 na kila gari moja lina thamani ya Sh200 milioni ambayo pia yanatembea kwa mafuta ya serikali. Ni ufisadi.

“Kama mke wa rais anatembea na msafara wa magari 20, je rais mwenyewe atatembea na msafara wa magari mangapi? Wakati mgombea urais wa Chadema akitembea kwa basi, mke wa rais anatembelea magari ya serikali. Ni ufisadi mkubwa kutumia magari hayo kwa maslahi binafsi.”

Aliyeanza kumlipua Mama Kikwete katika mkutano huo ni mkurugenzi wa kampeni wa Chadema, Suzan Kiwanga ambaye alidai kuwa kama mke huyo wa rais anataka kushiriki kwenye siasa angesajili chama na kuchukua fomu ya kugombea badala ya kutumia Wama.

Kiwanga alidai kuwa Mama Kikwete anafanya ziara hizo bila ya ratiba iliyoidhinishwa na Tume ya Uchaguzi (Nec), akimpigia debe mumuwe jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

“Nataka nimwambie huyu mtu aitwaye Mama Salma kwamba kiherehere chako kitakufikisha mahali pabaya. Unatumia fedha za wanawake za Wama kwa maslahi yako... ni kinyume cha sheria,” alisema Kiwanga huku akishangiliwa.


Kwa habari zaidi soma: MWANANCHI.
 
hapana , bali ana hisa katika biashara ya familia, na sio ya watanzania. watanzania ni watumishi katika biashara hiyo ya kifamilia.
 
hapana , bali ana hisa katika biashara ya familia, na sio ya watanzania. watanzania ni watumishi katika biashara hiyo ya kifamilia.

Kama si mtumishi wa umma kwa nini anatumia raslimali za umma vibaya hivyo? Anafikiri kuwa nchi hii inaongozwa na ukoo wa kifalme?
 
Sasa huyu anatumia pesa za WAMA na ikulu .Wana WAMA wamrudi kama alivyofanya huyu
 
Jamani mama Salma ni mtumishi wa serikali kama mwalimu. Kwani alistaafu kazi hiyo lini? Nitaamini si mtumishi wa serikali kama tutathibitishiwa kuwa alistaafu pindi mumewe alipopata promotion.

Na kama ni mtumishi wa serikali basi nadhani pia atakuwa akifanya kosa kujihusisha na kampeni wakati akiwa mtumishi wa serikali. Hilo lawezakuwa kosa.

Mlio na habari zake mtujuvye
 
Jamani mama Salma ni mtumishi wa serikali kama mwalimu. Kwani alistaafu kazi hiyo lini? Nitaamini si mtumishi wa serikali kama tutathibitishiwa kuwa alistaafu pindi mumewe alipopata promotion.

Na kama ni mtumishi wa serikali basi nadhani pia atakuwa akifanya kosa kujihusisha na kampeni wakati akiwa mtumishi wa serikali. Hilo lawezakuwa kosa.

Mlio na habari zake mtujuvye

Kama ni mwalimu anafundisha saa ngapi wakati kila siku yuko majukwaani kumpigia debe mumewe?
 
Jamani mama Salma ni mtumishi wa serikali kama mwalimu. Kwani alistaafu kazi hiyo lini? Nitaamini si mtumishi wa serikali kama tutathibitishiwa kuwa alistaafu pindi mumewe alipopata promotion.

Na kama ni mtumishi wa serikali basi nadhani pia atakuwa akifanya kosa kujihusisha na kampeni wakati akiwa mtumishi wa serikali. Hilo lawezakuwa kosa.

Mlio na habari zake mtujuvye

Mkuu umeniwahi Mama Salma ni mwalimu asiye na darasa maalum inaelekea hata mshahara wake hauna maelezo maalum ana majukumu mengi ya kitaifa:becky:
 
Kama ni mwalimu anafundisha saa ngapi wakati kila siku yuko majukwaani kumpigia debe mumewe?

Mh hili swali zito but natumai ikulu wana maelezo ya kutusaidia na kama anafundisha anafanya nini katika kampeni?
 
Sasa fedha za WAMA zinatumikaje kumnadi mumewe?

Salma ni mwenyekiti wa Mfuko wa Wanawake na Maendeleo(WaMa) ,anapozunguka mikoani pia anatumia kivuli hicho kupiga kampeni .Anaenda kukusanya wanawake kama vile ni mkutano wa WAMA pia anatumia kupiga kampeni.
 
Sasa huyu anatumia pesa za WAMA na ikulu .Wana WAMA wamrudi kama alivyofanya huyu

UNAJUA WAMA NI NINI MKUU?
UKITAKA KWA UNDANI WA HIYO KITU SOMA HAPA UELEWE VIZURI "WHO IS WAMA" (kwa kifupi tu ni kuwa Mama Salma na Mumwewe JK waliamua kuanzisha WAMA na kuipa ofisi ndani ya IKULU baada ya Mama ANNA MKapa na Mumewe "Denja Man" Mkaaapa kukatalia NGO inayoitwa EOTL (Equal Oppoortunity for ALL (!???;;wajua ilivyo Equal"").
HII NDO WAMA - WANAWAKE NA MAENDELEO NA NI HAYO UNAYOONA SASA KWA MAMA NA NA WASHIRIKA WAKE NA SASA KAANCHA KABISA MAMBO MUHIMU AMEINGIA KWENYE SIASA.

Wanawake Na Maendeleo (WAMA) Foundation is a non- governmental, non-profit organization founded by the Tanzanian First Lady, Mama Salma Kikwete in October 2006 in Dar es Salaam, Tanzania. The main goal of the organization is to improve the life standard of women, girls and other vulnerable children through promoting them to access to education, health service: adolescent and sexual reproductive, maternal and infant, and capacity building for economic empowerment.

WAMA joins other NGOs that serve the interests of women and children. The Foundation has a strategic plan to make significant contributions to Tanzanian women and their families through working closely with the government and donors.
WAMA's overall objective is to improve social and economic advancement of women and girl children in Tanzania by increasing access to education, maternal, newborn health and sexual reproductive health services including HIV and AIDS.



Na hawa ndio washirika wa Mama Salma katika WAMA (angalia vizuri kama kuna mlalahoi hapo:

  1. Hon. Mama. Salma Kikwete - Chairaperson
  2. Hon. Mama. Sophia Simba - Chairperson of the Board (Minister)
  3. Hon. Mama. Zakia Zamdan Meghji - Board Member (Rrt Minister)
  4. Hon. Amb. Mwanaidi Majaar Sinare - Board Member (Balozi)
  5. Hon. Mama. Regina Lowassa - Board Member( the then PM Wife)
  6. Mama. Blandina Nyoni - Board Member (Permanent Secretary)
  7. Hon. Mama Hulda S. Kibacha - Board Member (MB)
UKITAFAKARI KWA KINA UTAFAHAMU HAYA, KWA NI NINI TAASISI YA WANAWAKE NA MAENDELEO ISIJUMUISHE HATA MDAU MMOJA WA NAFASI YA AKINA "KAPUKU" KULE VIJIJINI!!!...NA KWA NINI IKAPEWA OFISI IKULU KWA MZEE MWENYEWE!!!>

NI WAKATI ULE AMBAPO MAMA SITI MWILI ALICHEZA NA TWIGA NA TAUSI WAKATI MUMEWE NI PRESID WA NCHI HII, MAMA MKAPA NAE AKAJA NA SITAILI YA KUWA NA IKULU YAKE NDANI YA IKULU NA BAADAE MWAKA 1999 KUMSHAWISHI BEN KUANZISHA "KAMPUNI YA ANNA & BEN MKAPA" (ANBEM) KWA KUANZISHA EOFL AMBAYO ALITOKA NAYO NA ANAENDELEA NAYO..SALMA NAE ALIPOONA ISIWE TABU AKAMWOMBA JK NAO WAWE NA TAWI LA IKULU KUPITIA HAKO "KA KAMPUNI".

TEGEMEA MENGI YATAKUJA.
 
Salma ni mwenyekiti wa Mfuko wa Wanawake na Maendeleo(WaMa) ,anapozunguka mikoani pia anatumia kivuli hicho kupiga kampeni .Anaenda kukusanya wanawake kama vile ni mkutano wa WAMA pia anatumia kupiga kampeni.

Hivi WAMA ni CHAMA CHA SIASA?
 
UNAJUA WAMA NINI NINI MKUU?
UKITAKA KWA UNDANI WA HIYO KITU SOMA HAPA UELEWE VIZURI "WHO IS WAMA" (kwa kifupi tu ni kuwa Mama Salma na Mumwewe JK waliamua kuanzisha WAMA na kuipa ofisi ndani ya IKULU baada ya Mama ANNA MKapa na Mumewe "Denja Man" Mkaaapa kukatalia NGO inayoitwa EOTL (Equal Oppoortunity for ALL (!???;;wajua ilivyo Equal"").
HII NDO WAMA - WANAWAKE NA MAENDELEO NA NI HAYO UNAYOONA SASA KWA MAMA NA NA WASHIRIKA WAKE NA SASA KAANCHA KABISA MAMBO MUHIMU AMEINGIA KWENYE SIASA.

Wanawake Na Maendeleo (WAMA) Foundation is a non- governmental, non-profit organization founded by the Tanzanian First Lady, Mama Salma Kikwete in October 2006 in Dar es Salaam, Tanzania. The main goal of the organization is to improve the life standard of women, girls and other vulnerable children through promoting them to access to education, health service: adolescent and sexual reproductive, maternal and infant, and capacity building for economic empowerment.

WAMA joins other NGOs that serve the interests of women and children. The Foundation has a strategic plan to make significant contributions to Tanzanian women and their families through working closely with the government and donors.
WAMA's overall objective is to improve social and economic advancement of women and girl children in Tanzania by increasing access to education, maternal, newborn health and sexual reproductive health services including HIV and AIDS.



Na hawa ndio washirika wa Mama Salma:

Board Members NAMETITLE Hon. Mama. Salma KikweteChairaperson Hon. Mama. Sophia SimbaChairperson of the Board Hon. Mama. Zakia Zamdan MeghjiBoard Member Hon. Amb. Mwanaidi Majaar Sinare Board Member Hon. Mama. Regina Lowassa Board Member Mama. Blandina Nyoni Board Member Hon. Mama Hulda S. Kibacha Board Member

Kumbe Sophia Simba naye yumo?
 
Salma kawa mwenyekiti wa WAMA by default kama project za mke wa rais kwa nchi,haitakiwi kutumiaka kisiasa .Unawaza kusema ulichowezesha Wama kufanikiwa ila si kutumia fund kutoka wama ktk kampeni.

Aliye uliza kama najua wama ni nini post ya juu kabla hajauliza swali nilielezea wama ni nini.
 
Nyinyi watu mnapiga sana kelele, lakini watanzania ni viumbe wa ajabu sana!!! Hata wakisikia na kushuhudia wanavyoibiwa, ni waoga tu. WEZI WETU hawana wasiwasi katu!! Mama endelea kutafuna vya mabwege.., usitie shaka. Nenepa mama!!! Hahahahaaaaa!:confused2:
 
Nyinyi watu mnapiga sana kelele, lakini watanzania ni viumbe wa ajabu sana!!! Hata wakisikia na kushuhudia wanavyoibiwa, ni waoga tu. WEZI WETU hawana wasiwasi katu!! Mama endelea kutafuna vya mabwege.., usitie shaka. Nenepa mama!!! Hahahahaaaaa!:confused2:

Hao mabwege ni pamoja na wewe au mwenzetu umejiweka pembeni? Anyway, kelele zinasaidia, ndio maana tulishuhudia wezi ambao majina yao hayakutajwa walirudisha maburungutu ya EPA!
 
Kama ni mwalimu anafundisha saa ngapi wakati kila siku yuko majukwaani kumpigia debe mumewe?
Hapa ndipo wale wenye nyeti zake watupe tujue je alistaafu na ni pensionable au anapeta akila mshahara bila kufanya kazi?
 
Back
Top Bottom