Mama Salma Kikwete, kutaka wake wa viongozi wakuu wapewe pension ni kumkufuru Mungu!

Kwa kweli nilishtushwa Sana niliposikia mama Salma Kikwete, akilitumia Bunge la Jamhuri ya Tanzania, badala ya kuongelea Shida za watu wa Jimbo lake la Mchinga, anaongelea mambo yake binafsi.

Eti anataka yeye kama mke wa Rais mstaafu, naye alipwe pension!

Hivi hawa viongozi wa CCM wanatuonaje watanzania?

Hivi Katika kipindi kama hiki, ambacho Taifa linapitia Katika kipindi kigumu mno cha uchumi, kwa kupanda bei kwa kila kitu, kutokana na kupanda Sana kwa bei za mafuta, wakati kipato cha mtanzania hakijaongezeka, hivi ni wakati sahihi wa kutumbukiza maoni binafsi ya kuomba kulipwa pension kwa ajili tu ya kuwa ni mke wa Rais mstaafu?

Hata hivyo nimuulize mama Salma, hivi hatosheki na kipato anachopata cha maslahi ya ubunge wa "kupewa" wa kipato cha shilingi milioni 12 kwa mwezi, ukiacha maslahi mengine ya Mheshimiwa mbunge, kama vile "seating allowance" ya kila kikao cha Bunge kinavyoendelea?

Hebu nimuulize tena mama Salma, hivi haridhiki na pension anayolipwa mumewe, Jakaya Kikwete, ya kuwa Rais mstaafu, ambayo ni 80% ya mshahara aliokuwa akiupata alipokuwa Rais wa nchi hii?

Hebu pia nimuulize mama Salma, hivi haridhiki na "upendeleo" aliopewa mwanaye Ridhiwani Kikwete, ya ubunge, ambapo pia "amezawadiwa" u-Naibu Waziri, ambapo anapata maslahi kibao?

Hivi mama Salma, hayaoni matatizo ya mamilioni ya watanzania, wanaohangaika kila kukicha, kutafuta riziki zao za kila siku, ambao hata wakifika umri wa uzeeni hawalipwi pension yoyote?

Hivi mama Salma, hayo uliyoyaongelea Bungeni, ndiyo mawazo ya wapiga kura wako wa Jimbo la Mchinga, waliyokutuma uwasemee?

Hakika baada ya kusikia kauli za mama Salma, alizozitoa Bungeni, nmeamini kabisa, kuwa hatuna wawakilishi wa wananchi huko Bungeni, bali tuna viwavi wa CCM wanaotaka kula kwa kuvimbiwa na watuache watanzania tukiwa hatuna kitu kabisa!

Nimeamini kuwa nchi hii kuendelea kuwachagua wawakilishi toka chama tawala cha CCM ni kuendeleza laana, ambayo itaendelea kututafuna kwa vizazi vingi vijavyo!
waache wale mkuu mpaka wajiharishie , wala hatupaswi kumlaumu kwa hoja yake kwani ujinga tumeofanya sisi wenyewe japo uyo bi mkubwa ubunge wake wa kupewa

inatakiwa tujifunze sasa ili tusifanye makosa 2025

mtu mumewe alikuwa Rais ana pensheni za kutosha, mtoto ni naibu wazir, Mama ni mbunge lakini cha kusikitisha bado anaendekeza njaa tu

kweli kuna viongozi wengine ni viwavi jeshi jaman
 
Mimi naona kama ofisi ya first lady inatambulika kikatiba na inategewa bajeti, kwanini wasipewe pession? tuache ku waonea kisa wana pesa haki itendeke mbona maraisi wa bunge majaji wanapewa pension licha ya kua maisha na mishahara yao ilikua mizuri?

Kwanini mama Nyerere Mama Magufuri mama Mkapa wa sipewe pession, kwanini wabaki kupata msaada na zawadi wakati katiba ina watambua, hapana hapo kuna point, tusitangulize hali yetu ngumu ya maisha kufanya uamuzi
Umeandika ujinga.Maana inaonekana hata pension hujui inapatikanaje.
 
Watanzania wengi tunatabia ya kukurupuka na hata kudandia mada bila kujipa muda wa kuona au kusikiliza kitu husika.

Mbona madai ya Mama Salma yako sahihi??

Amesema pension zao za kazi ambazo walikuwa wanafanya kama watumishi wa Umma wapatiwe, akaenda mbali kwa kutolea mfano yy alikuwa mwalimu akisema mara baada ya mumewe kuwa Rais aliachishwa ile kazi lkn hakupata stahiki zake kama ilivyotakiwa kwa mtumishi wa Umma pindi anapostaafu.

Kwanini sisi watanzania ni wajinga wa kudandia vitu na kuanza kulaumu bila kuelewa kitu chenyewe??
Alikua wapi kwa miaka yote 10 kutofwatilia ilo.maana kama michango yake ilikua inamruhusu kupata mafao yake ni kipi kilimfanya asifwatilie.Maana hakutakiwa kulipwa pension kwasababu ni mke wa rais bali alitakiwa kulipwa mafao yake kwasababu alikua mtumishi wa umma na kaachana na hiyo kazi na ilikua haki yake endapo anakidhi vigezo.ndo maana wenye akili walipiga kelele pale serikali iliyopita iliopoondoa Fao la kujitoa.
 
Kwa kweli nilishtushwa Sana niliposikia mama Salma Kikwete, akilitumia Bunge la Jamhuri ya Tanzania, badala ya kuongelea Shida za watu wa Jimbo lake la Mchinga, anaongelea mambo yake binafsi.

Eti anataka yeye kama mke wa Rais mstaafu, naye alipwe pension!

Hivi hawa viongozi wa CCM wanatuonaje watanzania?

Hivi Katika kipindi kama hiki, ambacho Taifa linapitia Katika kipindi kigumu mno cha uchumi, kwa kupanda bei kwa kila kitu, kutokana na kupanda Sana kwa bei za mafuta, wakati kipato cha mtanzania hakijaongezeka, hivi ni wakati sahihi wa kutumbukiza maoni binafsi ya kuomba kulipwa pension kwa ajili tu ya kuwa ni mke wa Rais mstaafu?

Hata hivyo nimuulize mama Salma, hivi hatosheki na kipato anachopata cha maslahi ya ubunge wa "kupewa" wa kipato cha shilingi milioni 12 kwa mwezi, ukiacha maslahi mengine ya Mheshimiwa mbunge, kama vile "seating allowance" ya kila kikao cha Bunge kinavyoendelea?

Hebu nimuulize tena mama Salma, hivi haridhiki na pension anayolipwa mumewe, Jakaya Kikwete, ya kuwa Rais mstaafu, ambayo ni 80% ya mshahara aliokuwa akiupata alipokuwa Rais wa nchi hii?

Hebu pia nimuulize mama Salma, hivi haridhiki na "upendeleo" aliopewa mwanaye Ridhiwani Kikwete, ya ubunge, ambapo pia "amezawadiwa" u-Naibu Waziri, ambapo anapata maslahi kibao?

Hivi mama Salma, hayaoni matatizo ya mamilioni ya watanzania, wanaohangaika kila kukicha, kutafuta riziki zao za kila siku, ambao hata wakifika umri wa uzeeni hawalipwi pension yoyote?

Hivi mama Salma, hayo uliyoyaongelea Bungeni, ndiyo mawazo ya wapiga kura wako wa Jimbo la Mchinga, waliyokutuma uwasemee?

Hakika baada ya kusikia kauli za mama Salma, alizozitoa Bungeni, nmeamini kabisa, kuwa hatuna wawakilishi wa wananchi huko Bungeni, bali tuna viwavi wa CCM wanaotaka kula kwa kuvimbiwa na watuache watanzania tukiwa hatuna kitu kabisa!

Nimeamini kuwa nchi hii kuendelea kuwachagua wawakilishi toka chama tawala cha CCM ni kuendeleza laana, ambayo itaendelea kututafuna kwa vizazi vingi vijavyo!
Mumewe analipwa Pensheni Magufuli kawajengea Nyumba Kawe Beach ya Mabilioni yeye kapewa Ubunge Hebu kuweni na HURUMA hizo Pesa hamtakwenda nazo Mbinguni
 
Huyo naye anataka nini zaidi?
Rais akiondoka madarakani anaendelea kutumia Bajeti ya Serikali hadi siku ya kuingizwa kaburini.
Bajeti hiyo inamhusu yeye pamoja na familia yake yote.
 
Tutakuja sikia tumeuzwa na familia ya Jk
Hivi hizi familia za wastaafu zinajisikiaje watazania wanapozilalamikia kuwa mizigo isiyobebeka wakati familia ya baba w taifa ikiwa zawadi kwa watanzania. Jk ,Jk ,Jk family . Hii familia nimeiita mara tatu .
 
Jakaya Kikwete, ya kuwa Rais mstaafu, ambayo ni 80% ya mshahara aliokuwa akiupata alipokuwa Rais wa nchi hii?

Mkuu nilisikia analipwa 80% ya Mshahara anaolipwa Rais aliyepo madarakani...... na sio 80% ya salary aliyokuwa akilipwa yeye...

Hii ni kutokana na thamani ya pesa kubadilika...

Leo ukimlipa Mzee mwinyi 80% ya mshahara wake aliokuwa analipwa unadhani atapokea kiasi gani.???
 
Hakika kabisa alieshiba hamjui mwenye njaa!

Hivi Katika dimbwi hili la umaskini linalotukabili mamilioni ya watanzania, hivi mwakikishi wetu Bungeni, ndiyo atoe mawazo yake binafsi ya kuomba Bunge lifikirie wake wa ma-Rais wastaafu, wake wa ma-Waziri wastaafu nao walipwe pension?
Salma Kikwete = Marie Antoinette
 
Back
Top Bottom