Mama Salma Kikwete atesa na ndege ya Rais,JK aikwepa...

Mlalahoi

JF-Expert Member
Aug 31, 2006
2,182
883
Salma atesa na ndege ya Kikwete
Ni ile ambayo rais anaogopa kuitumia kikazi Ulaya
Aipanda kwenda na kurejea katika ziara binafsi
Aitumia kuendea sherehe za mila za Mswati III

na Mwandishi Wetu

BAADA ya Rais Jakaya Kikwete ‘kuogopa’ kutumia ndege yake iliyonunuliwa kwa mabilioni ya shilingi bila idhini ya Watanzania, sasa ndege hiyo inatumiwa na mkewe, Salma katika ziara binafsi.

Mara ya mwisho, Salma alitumia ndege hiyo kwenda kwenye sherehe za kimila nchini Swaziland, kushuhudia Mfalme Mswati III akichagua mke wa 13.

Uchunguzi wa Tanzania Daima umethibitisha kuwa Salma aliondoka Dar es Salaam Agosti 29, mwaka huu saa tisa jioni, akiwa amepanda ndege hiyo aina ya Gulfstreame Jet Engine kwenda Manzini, Swaziland.

Ndege hiyo ya rais namba 05H-ONE, iliondoka Dar es Salaam kuelekea Swaziland, alikokuwa anakwenda kuhudhuria sherehe za kimila, ambazo baadaye zimeshutumiwa na wanaharakati kwamba zinawadhalilisha wanawake.

Septemba 5, mwaka huu, ndege hiyo ilimfuata na kumrejesha Dar es Salaam.

Kwa hakika haya ni matumizi mabaya ya ndege ya rais, kwa kuwa mke wa rais, si rais, na hapaswi kuitumia kama anasafiri peke yake kwa safari binafsi.

Fursa pekee aliyonayo mke wa rais kutumia ndege hiyo, isiyoweza kunung’unikiwa hata kidogo, ni pale anaposafiri na mumewe katika safari za kikazi.

Matumizi haya ni kashfa nzito kwa serikali ya awamu ya nne, inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete, aliyesema tangu awali kwamba urais wake usingekuwa wa ubia na mtu yeyote.

Miezi miwili iliyopita, gazeti hili liliandika habari kuwa Rais Kikwete anahofu kupanda ndege hiyo katika safari zake za kikazi Ulaya, kwa madai kuwa ni gharama kubwa mno kwa nchi maskini kama Tanzania.

Badala yake, ameazimia kuitumia katika safari za Afrika, hali inayotafsiriwa pia kuwa anaona aibu kupanda ndege ya kifahari kwenda Ulaya kuomba misaada kwa serikali zinazoongozwa na viongozi wanaotumia ndege za kawaida katika safari zao za kikazi.
 
Ndugu Admin
Naomba fafanua huyu Salma anachafuliwa kivipi ?Hapandi ndege ? Hakupanda ndege ?Hajaitumia jinsi ilivyosema hapo juu ?
 
Hakuna cha JK kuwa serious hiyo ni danganya toto ya siku zote ya CCM na kada wao tangia mwalimu aachie Madaraka.

Tanzania haitakaa iwe na kiongozi serious baada ya Mwalimu, nadhani viongozi wa Tanzania wanaoweza kuwa serious bado hawajazaliwa.

I hate war but the only way to have a positive future for Tanzania and Tanzania is a limited socio-political war.

As long as we keep on recyclying the political machinery of Tanzania we will never see the light of the day.

Mungu ibariki Tanzania, walaani viongozi wake
 
Hivi ni kweli kuwa mke wa rais haruhusiwi kuipanda ndege hiyo mpaka awe anasafiri na rais? Kwa wanaofahamu utaratibu, je Mama Salma alitakiwa atumie usafiri gani?

Nnavyofahamu mimi, sio mke wa rais tu.. bali kuna wakati hata viongozi wengine au wageni maalum nchini pia wanaweza kuruhusiwa kuitumia ndege ya rais.

Je hii safari ni kweli ilikuwa ni ya binafsi? Yaani najiuliza, asingekuwa ni first lady huyu mama angealikwa huko Swaziland? Kama amealikwa in her capacity as first lady, kwa maoni yangu hiyo si safari binafsi. (maana hakuipanda hiyo ndege kwenda kufanya shopping dubai).

Mwandishi kaashiria kama vile imekuwa ni kawaida sasa mama Salma kuitumia ndege hii, na kuwa 'mara ya mwisho' ameitumia kwa safari ya swazi... bila kutuambia amesafiri mara ngapi na kwenda wapi kwengine. Mimi naona huo ni uandishi wa kijanja .. safari ni hii moja tu.

Msinielewe vibaya, hata mimi naona ingekuwa busara kutumia usafiri mwingine wenye gharama nafuu, lakini naona hii makala imeandikwa kiujanja ujanja sana katika kumuandama huyu mama na JK.

Yaani msomaji anaweza kudhani ni awamu ya JK ndio imenunua hiyo ndege kwa mabilioni ya pesa 'bila idhini ya wananchi', wakati ndege ilinunuliwa wakati wa Mkapa. Hili jidege bora liuzwe tu yaishe!
 
Kulikoni said:
Hivi ni kweli kuwa mke wa rais haruhusiwi kuipanda ndege hiyo mpaka awe anasafiri na rais? Kwa wanaofahamu utaratibu, je Mama Salma alitakiwa atumie usafiri gani?

Nnavyofahamu mimi, sio mke wa rais tu.. bali kuna wakati hata viongozi wengine au wageni maalum nchini pia wanaweza kuruhusiwa kuitumia ndege ya rais.

Je hii safari ni kweli ilikuwa ni ya binafsi? Yaani najiuliza, asingekuwa ni first lady huyu mama angealikwa huko Swaziland? Kama amealikwa in her capacity as first lady, kwa maoni yangu hiyo si safari binafsi. (maana hakuipanda hiyo ndege kwenda kufanya shopping dubai).

Mwandishi kaashiria kama vile imekuwa ni kawaida sasa mama Salma kuitumia ndege hii, na kuwa 'mara ya mwisho' ameitumia kwa safari ya swazi... bila kutuambia amesafiri mara ngapi na kwenda wapi kwengine. Mimi naona huo ni uandishi wa kijanja .. safari ni hii moja tu.

Msinielewe vibaya, hata mimi naona ingekuwa busara kutumia usafiri mwingine wenye gharama nafuu, lakini naona hii makala imeandikwa kiujanja ujanja sana katika kumuandama huyu mama na JK.

Yaani msomaji anaweza kudhani ni awamu ya JK ndio imenunua hiyo ndege kwa mabilioni ya pesa 'bila idhini ya wananchi', wakati ndege ilinunuliwa wakati wa Mkapa. Hili jidege bora liuzwe tu yaishe!

Yeah.. sawa kabisa
 
Wandugu
Mwaka jana kama sikosei mkewe GB alikuwa Tanzania .Je alikuja na Airpforce? Hivi ni kweli kwamba mke wa Rais hawezi kupata ndege za kawaida hata kwenye business aka save pesa kidogo za walala hoi ? Hii ndege imenunuliwa na wote JK na Mkapa maana wote walikuwa ni serikali moja na sioni ubaya hata tukisema ndege kanunuliwa yeye JK .Safari 2 ni nyingi kwa mke wa Rais kupelekwa na kufuatwa .Wangapia wana sida huku Tanzania wanakosa hata udhamini wa serikali kisa haina pesa ?
Juzi Chuo Kikuu wamerushwa na FFU wakidai pesa na wana njaa Salma yeye na dege la gharama angani bado nidhani ni kawaida kisa First woman ?
 
Gharama ya ndege ikiwa angani ni DOLA $6,000, au SHILLINGI MILLIONI SITA kwa saa, kama nilivyoambiwa na wataalamu wanaohusika nayo,
 
Mzee Es said:
Gharama ya ndege ikiwa angani ni DOLA $6,000, au SHILLINGI MILLIONI SITA kwa saa, kama nilivyoambiwa na wataalamu wanaohusika nayo,

Tanzania Daima walisema hivyo kabla. ni sawa kabisa
 
Ndege ni ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,sio ya mke,mtoto au bamdogo wa Rais.Huyo anaesema kwamba kuna kosa gani mke wa Rais kutumia ndege ya Rais anatakiwa kujiuliza je JK akipatwa na udhuru Mama Salma atakaimu Urais?Kabla ya kusema kuwa alichofanya huyo mwanamama si kosa,ulipaswa kujua iwapo ni kosa au la.Jibu ni kwamba,sheria haimruhusu,ila tu pale anapokuwa na mumewe.

Kuna kijitabia cha watu kubisha tu wakati hawana data.Kwanini kabla hamjapoteza muda wenu kubishana msihangaike kutafuta data kwanza?
 
Mlalahoi said:
Ndege ni ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,sio ya mke,mtoto au bamdogo wa Rais.Huyo anaesema kwamba kuna kosa gani mke wa Rais kutumia ndege ya Rais anatakiwa kujiuliza je JK akipatwa na udhuru Mama Salma atakaimu Urais? Kabla ya kusema kuwa alichofanya huyo mwanamama si kosa,ulipaswa kujua iwapo ni kosa au la.Jibu ni kwamba,sheria haimruhusu,ila tu pale anapokuwa na mumewe.

Kuna kijitabia cha watu kubisha tu wakati hawana data. Kwanini kabla hamjapoteza muda wenu kubishana msihangaike kutafuta data kwanza?

Mlalahoi,

My post was very clear, sikustate kuwa si kosa, I asked whether ni kosa or not. I still doubt kuwa eti ndege ya rais ni ya rais tuuu. Nasema hivi kwa sababu nnafahamu kuwa ni mwezi uliopita tu ilikuja delegation ya wataalamu wa Aviation wa UN, walipatiwa moja ya ndege za rais wakaenda nayo Zanzibar na Arusha (although nao pia hawawezi kukaimu urais JK akiwa na dharura).

My post was meant to highlight the exaggerations made by mwandishi... kuiita eti safari binafsi, kashfa nzitooo etc. My stand was also very clear: hata kama sheria inamruhusu, ingekuwa ni busara na more economical kutolitumia jidege hilo.
 
Inamana Laura Bush alivyokuja bongo, alikuja na Commercial Airlines au alikuja na Air Force One?

Mimi sijui alikuja na ndege gani. ila nauliza tuu
 
ninavyoelewa mimi hiyo ni ndege ya serikali. hivi salma aliondoka bila kuaga? hivi inawezekana salma atumie ndege hiyo bila ruhusa ya Jakaya?

pamoja na kwamba sikubaliani na maudhui ya ziara ya salma uswazi, nadhani tutakuwa tunamuonea kwa kumbebesha lawama za kutumia ndege ya serikali. zaidi, ziara yake uswazi ilikuwa ya kiserikali.
 
Huu nauita upotevu wa muda.

Angalia maudhui ya safari, nini hasa Taifa imefaidika na hiyo safari? JK aanze naye kuoa kila mwaka?, bila kujali katumia Gulf stream au BOTI, ni Ujinga Upotevu wa fikra na matumizi mabaya ya hela yangu!!!!

Naomba waache kutumia vibaya hela yangu, waitumie kujengea mahospitali au shule.

FD
 
Naam nami naamini kuna ''kadhambi'' katika kutumia hii ndege indeed nadhani ikiuzwa itakuwa bora zaidi manake imesemwa mno na hakuna cha ajabu tukiiuza.

Mkapa aliwahi kuwaita wanaobeza uamuzi wa kununua ile ndege ''wana wivu'' such is a mentality ya baadhi ya viongozi wetu, safari ni ndefu...

Nadhani kwa sasa upinzani ni dhaifu mno na CCM is too big for its own good,tunahitaji mabadiliko ndani ya ccm kidemokrasia tuweze kusonga mbele manake ni unlikely kupata opposition government in near future.

tuliwahi kuambiwa wamempa kazi dr gharib bilal aangalie namna viongozi wanavyopatikana ndani ya chama sijui kafikia wapi.

ni hatari sana kwa sasa ambapo waandishi takriban wote wana serve political interests za publishers and owners wao.

Mengi na magazeti yake unajua yamesimamia wapi...

TANZANIA DAIMA la Mbowe unajua kabisa limekaa kiupinzanipinzani tu manake kama alivyosema KULIKONI hii hadithi imekuwa twisted vibaya sana kama wanavyotwist THIS DAY on NSSF/MANJI manake sasa utadhani ni soap/drama hivi kila siku kuna version mpya nadhani wale jamaa wa special NSSF correspondent anaetumwa kila siku aweke uongo mpya!

Kama alivyosema MBOWE waandishi wasiogope na wawe huru kuandika lakini bwana MBOWE angalia boriti la jichoni mwako kwanza....
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom