Uchaguzi 2020 Mama Salma Kikwete akiwa Rais ajaye sitashangaa

usinijibu hivyo

JF-Expert Member
Nov 7, 2017
248
327
Natazama hapa mahojiano Mubashara Clouds TV kipindi cha 360 wakimuhoji huyu Mbunge na Mhe 1st Lady Mstaafu.

Ukweli ni kwamba ametulia sana akijieleza kama Mwalimu wa hesabu shule ya Msingi alieendelea kufundisha ata Mume wake alipokuwa Waziri.

Mara zote anasisitiza kuhusu malezi ya Familia ndio msingi wa maendeleo ya Taifa endapo jamii itazingatia kuwa watoto ni wa jamii nzima kwa kauli mbiu kuwa "MTOTO WA MWENZIO NI MWANAO,MLINDE"
Tukijenga watoto wenye nidhamu na adabu Taifa litaendelea

Mama huyu kumbe ameanzisha shule mbili za sekondari Wama Nakayama -Nyamisati na WamaSharifu -Lindi zilizoongoza kimkoa zikisomesha watoto wakike bure na wakipewa kila kitu muhimu.

Uongozi wa kijiji toka nchi nzima unakaa nakipitisha mtoto wa kike aliemaliza darasa La saba ambae ni yatima ama anaishi mazingira magumu bila kujali kabila lake wala Dini yake

Shule inamchukua anaishi shuleni hadi anapomaliza na ikibidi kwenda likizo anapewa nauli ya kwenda na kurudi na akifika kijijini anapokelewa na uongozi wa kijiji unaopewa jukumu la kumlinda

Baadhi ya mabinti waliopitia shule zake wameshahitimu vyuo vikuu na wapo makazini sasa.

Ukifatilia siasa za nchi zilizoendelea Mara nyingi wagombea Urais wa nchi kama Marekani wamekuwa wakielezea Sera zao katika kushindana nani akipewa nchi watoto na familia zitakuwa bora zaidi,kumbuka ile hotuba ya Obama maarufu alivyozunguzia mambo ya uzazi,bima ya matibabu ilivyompa umaarufu.

Kuwa Wamarekani wanachagua Rais ambae wanauhakika watoto wao watakuwa salama na watatimiza Malengo yao.

Katika dunia tuendayo lazima kuamini kuwa siku moja nchi yetu itaendeshwa na Mwanamke kwa kuwa Wanawake wanahaki hiyo,wanahuruma na ndio Mama zetu,Sasa tuna makamu wa Rais, basi ipo siku tutapata Rais MwanaMama

WANAWAKE WANAWEZA hasa unapokuwa na Mwanamke ametulia kama Mama Salma Kikwete ambae ni Mwalimu na Tayari ameishi Ikulu kwa Miaka 10

Hongera sana Mama Salma Kikwete,baada ya Rais wetu wa sasa kumaliza Miaka 10 yake,Mwenyezi akikusaidia ukiwa Rais wetu sitashangaa zaidi ya Kukuombea Mungu uwe kiongozi wa busara zaidi ya Zile za Mzee Jakaya.

SITASHANGAAAAA.

IMG-20200124-WA0004.jpeg
1579848597874.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Natazama hapa mahojiano Mubashara Clouds TV kipindi cha 360 wakimuhoji huyu Mbunge na Mhe 1st Lady Mstaafu.

Ukweli ni kwamba ametulia sana akijieleza kama Mwalimu wa hesabu shule ya Msingi alieendelea kufundisha ata Mume wake alipokuwa Waziri.

Mara zote anasisitiza kuhusu malezi ya Familia ndio msingi wa maendeleo ya Taifa endapo jamii itazingatia kuwa watoto ni wa jamii nzima kwa kauli mbiu kuwa "MTOTO WA MWENZIO NI MWANAO,MLINDE"
Tukijenga watoto wenye nidhamu na adabu Taifa litaendelea

Mama huyu kumbe ameanzisha shule mbili za sekondari Wama Nakayama -Nyamisati na WamaSharifu -Lindi zilizoongoza kimkoa zikisomesha watoto wakike bure na wakipewa kila kitu muhimu.

Uongozi wa kijiji toka nchi nzima unakaa nakipitisha mtoto wa kike aliemaliza darasa La saba ambae ni yatima ama anaishi mazingira magumu bila kujali kabila lake wala Dini yake

Shule inamchukua anaishi shuleni hadi anapomaliza na ikibidi kwenda likizo anapewa nauli ya kwenda na kurudi na akifika kijijini anapokelewa na uongozi wa kijiji unaopewa jukumu la kumlinda

Baadhi ya mabinti waliopitia shule zake wameshahitimu vyuo vikuu na wapo makazini sasa.

Ukifatilia siasa za nchi zilizoendelea Mara nyingi wagombea Urais wa nchi kama Marekani wamekuwa wakielezea Sera zao katika kushindana nani akipewa nchi watoto na familia zitakuwa bora zaidi,kumbuka ile hotuba ya Obama maarufu alivyozunguzia mambo ya uzazi,bima ya matibabu ilivyompa umaarufu.

Kuwa Wamarekani wanachagua Rais ambae wanauhakika watoto wao watakuwa salama na watatimiza Malengo yao.

Katika dunia tuendayo lazima kuamini kuwa siku moja nchi yetu itaendeshwa na Mwanamke kwa kuwa Wanawake wanahaki hiyo,wanahuruma na ndio Mama zetu,Sasa tuna makamu wa Rais, basi ipo siku tutapata Rais MwanaMama

WANAWAKE WANAWEZA hasa unapokuwa na Mwanamke ametulia kama Mama Salma Kikwete ambae ni Mwalimu na Tayari ameishi Ikulu kwa Miaka 10

Hongera sana Mama Salma Kikwete,baada ya Rais wetu wa sasa kumaliza Miaka 10 yake,Mwenyezi akikusaidia ukiwa Rais wetu sitashangaa zaidi ya Kukuombea Mungu uwe kiongozi wa busara zaidi ya Zile za Mzee Jakaya.

SITASHANGAAAAA.

View attachment 1332733View attachment 1332734

Sent using Jamii Forums mobile app
HILARY CLINTON alifanikiwa?
 
Kwa kipimo hicho,vipi msukuma wa darasa la Saba? Nae anajua kuongea vizuri kwa mpangilio kwenye media. Mpaka kufikia mwaka 2050 sitashangaa hii nchi kutangazwa ni nchi inayoongoza kwa umasikini na mazwazwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom