Mingoi
JF-Expert Member
- Jul 21, 2012
- 11,715
- 6,119
Huyu mama ni mroho wa madaraka na dhahiri inaonyesha ameamua kumtelekeza mumewe kwa tamaa za madaraka.Miaka miatno ya ubunge wa ikulu ilimtosha kabisa kukaa pembeni kipindi hiki na kuruhusu wengine kushika nafasi za uongozi. Baada ya mumewe kustaafu na kurudi kijijini Msoga angetulia tu kwani atawezaje kutumikia jimbo wakati huo huo familia? Mwezi Mei mwanzoni aliingia matatani na kamati ya siasa ya wilaya Lindi vijijini baada mbinu zake za kuanza kampeni kabla kubainika pale ambapo aliwabeba wajumbe 15 wa CCM na kuwasafirisha Dar es salaam ili kwenda kumshawishi mumewe ambae anaonyesha kutokubaliananae mpango huo ulivuja na suala zima kufika katika mikono ya TAKUKURU Lindi kwa mahojiano. Suala hili halikuripotiwa na chombo chochote na juhudi kubwa zilifanyika kutaka kulizima lakini maagizo ya chama makao makuu ya kumtaka kuhojiwa yalitekelezwa. Baadhi ya wajumbe hao walipatwa na hata ya kuzuiliwa kufanya shughuli za kisiasa kwa vipindi vya mwaka mmoja, miezi 6 na wengine waliishia kupewa onyo kali lakini mama hakupewa adhabu yeyote. Lakini kama haitoshi jana tar 15 amechukua fomu mbili za kugombea,UWT viti maalum na fomu ya jimbo la Mchinga.(Yaleyale aliyoyasema Humphrey Polepole ya viongozi kuridhika) CCM na vyombo vya usalama visiingilie huu uchaguzi wauache uwe huru ili demokrasia ichukue mkondo wake na Salma avune anachostahili.