CK Allan
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 2,723
- 5,899
Nikusalimu mama, kwanza kabla ya yote mama niseme mimi nakukubali sana utendaji wako tangu ukiwa necta na hata kuchaguliwa kwako nilifurahi sana maana nakukujua na binafsi nimeshafanya kazi Mara mbili na wewe hivyo nakujua kidogo..
Kadri siku zinavyosogea umaarufu wako unazidi kuporomoka kutokana na matamko yako na si utendaji wako!! wadadavuzi Wa mambo wanadai kinachokuponza ni kutamka tu...kila unapopita!! nimejaribu kufuatilia matamko yako nikaona una nia njema ya kuua nyoka lakini unapiga kwenye mkia bila kutafuta kichwa!!
Nakuhakikishia ukipiga kichwani ni fimbo moja tu nzito kuliko kupiga fimbo mia mkiani...
Mama ubora Wa Elimu nchi hii ni WALIMU !! hiki ndio kichwa cha nyoka! Mara majoho, sijui nini, ohh sijui hivi!! huko kote mama unapiga mkiani!!
Kaa vizuri na walimu wako changamoto zao unazijua vyema!! poteza muda wako mwingi kukaa nao na kuwaambia kipi unataka wakifanye katika Elimu Yetu, tatua kero zao, boresha maslahi yao...rudisha ile morali yao ya kazi hiki ndicho kichwa mamaangu!!
Najua siasa inaanza kukutawala kidogo na wapo watakaokunong'oneza kuwa nyoka ukimkata mkia atakufa pole pole!! achana nao .
Kadri siku zinavyosogea umaarufu wako unazidi kuporomoka kutokana na matamko yako na si utendaji wako!! wadadavuzi Wa mambo wanadai kinachokuponza ni kutamka tu...kila unapopita!! nimejaribu kufuatilia matamko yako nikaona una nia njema ya kuua nyoka lakini unapiga kwenye mkia bila kutafuta kichwa!!
Nakuhakikishia ukipiga kichwani ni fimbo moja tu nzito kuliko kupiga fimbo mia mkiani...
Mama ubora Wa Elimu nchi hii ni WALIMU !! hiki ndio kichwa cha nyoka! Mara majoho, sijui nini, ohh sijui hivi!! huko kote mama unapiga mkiani!!
Kaa vizuri na walimu wako changamoto zao unazijua vyema!! poteza muda wako mwingi kukaa nao na kuwaambia kipi unataka wakifanye katika Elimu Yetu, tatua kero zao, boresha maslahi yao...rudisha ile morali yao ya kazi hiki ndicho kichwa mamaangu!!
Najua siasa inaanza kukutawala kidogo na wapo watakaokunong'oneza kuwa nyoka ukimkata mkia atakufa pole pole!! achana nao .