Mama mzazi amzika mwanaye usiku wa manane baada ya mtoto kufa kwa njaa

Salah Jackson (5) mwenye ulemavu wa viungo, mkazi wa kijiji cha Makiwaru Mkoani Kilimanjaro amefariki dunia kutokana na njaa na kisha mama yake mzazi kumzika kimyakimya usiku wa manane.

Mtoto huyo anadaiwa kuzikwa na mama yake mzazi aitwaye Rebecca Siowi (30) usiku wa kuamkia Aprili 22, 2022 nyumbani kwa bibi yake walikokuwa wakiishi yeye pamoja na mama yake baada ya mume kumtelekeza na watoto watano.

Tukio hilo liligundulika baada ya mtoto huyo kutoonekana jioni ya Aprili 21 nyumbani alikokuwa akiishi kwa bibi yake, ambapo bibi yake huyo alifanya jitihada za kumtafuta mjukuu wake huyo bila mafanikio ndipo Aprili 22 alipobainika kuwa amezikwa.

Akizungumzia tukio hilo leo Aprili 23, 2022 Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amekiri kuwepo kwa tukio hilo, akisema baada ya kupata taarifa ya tukio hilo kutoka kwa wananchi walifika eneo la tukio kuona sehemu alipozikwa mtoto huyo.

Kamanda Maigwa amesema walipofika eneo la tukio walilazimika kuomba kibali cha kuufukua mwili wa mtoto huyo ili kujua sasababu hasa za kifo cha mtoto huyo kutokana na maneneo ambayo yalikuwa yakisemwa mtaani.

"Hili tukio kweli lipo na baada ya Jeshi la polisi kupata taarifa juu ya tukio hilo tulienda kuomba kibali cha kufukua mwili wa mtoto ili kujiridhisha sababu za kifo cha mtoto huyo ni nini kutokana na maneno mengi yaliyokuwepo mtaani.

"Tulifukua mwili jana na kuupeleka hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na majibu ya daktari yalipotoka yalionyesha kwamba huyu mtoto alikufa kutokana na njaa,” amesema Kamanda Maigwa

Akizungumzia tukio hilo, jirani wa familia hiyo, Maria Nko amesema hata kama mtoto huyo alikufa kwa njaa mama yake huyo hakupaswa kumzika mwanaye kama mbwa tena usiku wa manane.

"Kwa kweli hili tukio linaumiza na inaonekana huyu mama alikuwa akimtesa huyu mtoto kutokana na ulemavu aliokuwa nao, inakuwaje hao watoto wake wengine hawajafa na njaa na kwa nini amzike mwenyewe tena?” amehoji.


Source: Mwananchi
Si huwa mnasema kwamba kilimanjaro ni matajiri inakuwaje mtoto anakufa kwa njaa ?
 
Jamii mbona haijamsaidia kitu hilo gazeti limeweza kupata habari na kuuza ila hawakuweza kupata taarifa ya mtoto mwenye njaa..
Majirani husika ndio ujua watoto wanaishije then wao ndo utoa taarifa kwa mamlaka husika au media,kisha Media inapost kisha Jamii utoa msaada husika
 
Salah Jackson (5) mwenye ulemavu wa viungo, mkazi wa kijiji cha Makiwaru Mkoani Kilimanjaro amefariki dunia kutokana na njaa na kisha mama yake mzazi kumzika kimyakimya usiku wa manane.

Mtoto huyo anadaiwa kuzikwa na mama yake mzazi aitwaye Rebecca Siowi (30) usiku wa kuamkia Aprili 22, 2022 nyumbani kwa bibi yake walikokuwa wakiishi yeye pamoja na mama yake baada ya mume kumtelekeza na watoto watano.

Tukio hilo liligundulika baada ya mtoto huyo kutoonekana jioni ya Aprili 21 nyumbani alikokuwa akiishi kwa bibi yake, ambapo bibi yake huyo alifanya jitihada za kumtafuta mjukuu wake huyo bila mafanikio ndipo Aprili 22 alipobainika kuwa amezikwa.

Akizungumzia tukio hilo leo Aprili 23, 2022 Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amekiri kuwepo kwa tukio hilo, akisema baada ya kupata taarifa ya tukio hilo kutoka kwa wananchi walifika eneo la tukio kuona sehemu alipozikwa mtoto huyo.

Kamanda Maigwa amesema walipofika eneo la tukio walilazimika kuomba kibali cha kuufukua mwili wa mtoto huyo ili kujua sasababu hasa za kifo cha mtoto huyo kutokana na maneneo ambayo yalikuwa yakisemwa mtaani.

"Hili tukio kweli lipo na baada ya Jeshi la polisi kupata taarifa juu ya tukio hilo tulienda kuomba kibali cha kufukua mwili wa mtoto ili kujiridhisha sababu za kifo cha mtoto huyo ni nini kutokana na maneno mengi yaliyokuwepo mtaani.

"Tulifukua mwili jana na kuupeleka hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na majibu ya daktari yalipotoka yalionyesha kwamba huyu mtoto alikufa kutokana na njaa,” amesema Kamanda Maigwa

Akizungumzia tukio hilo, jirani wa familia hiyo, Maria Nko amesema hata kama mtoto huyo alikufa kwa njaa mama yake huyo hakupaswa kumzika mwanaye kama mbwa tena usiku wa manane.

"Kwa kweli hili tukio linaumiza na inaonekana huyu mama alikuwa akimtesa huyu mtoto kutokana na ulemavu aliokuwa nao, inakuwaje hao watoto wake wengine hawajafa na njaa na kwa nini amzike mwenyewe tena?” amehoji.


Source: Mwananchi
Aafu kuna wachungaji na manabii wananunua ma VX,Range na Prado badala ya kusaidia wasiojiweza km hawa. Upuuzi mtupu!
 
Salah Jackson (5) mwenye ulemavu wa viungo, mkazi wa kijiji cha Makiwaru Mkoani Kilimanjaro amefariki dunia kutokana na njaa na kisha mama yake mzazi kumzika kimyakimya usiku wa manane.

Mtoto huyo anadaiwa kuzikwa na mama yake mzazi aitwaye Rebecca Siowi (30) usiku wa kuamkia Aprili 22, 2022 nyumbani kwa bibi yake walikokuwa wakiishi yeye pamoja na mama yake baada ya mume kumtelekeza na watoto watano.

Tukio hilo liligundulika baada ya mtoto huyo kutoonekana jioni ya Aprili 21 nyumbani alikokuwa akiishi kwa bibi yake, ambapo bibi yake huyo alifanya jitihada za kumtafuta mjukuu wake huyo bila mafanikio ndipo Aprili 22 alipobainika kuwa amezikwa.

Akizungumzia tukio hilo leo Aprili 23, 2022 Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amekiri kuwepo kwa tukio hilo, akisema baada ya kupata taarifa ya tukio hilo kutoka kwa wananchi walifika eneo la tukio kuona sehemu alipozikwa mtoto huyo.

Kamanda Maigwa amesema walipofika eneo la tukio walilazimika kuomba kibali cha kuufukua mwili wa mtoto huyo ili kujua sasababu hasa za kifo cha mtoto huyo kutokana na maneneo ambayo yalikuwa yakisemwa mtaani.

"Hili tukio kweli lipo na baada ya Jeshi la polisi kupata taarifa juu ya tukio hilo tulienda kuomba kibali cha kufukua mwili wa mtoto ili kujiridhisha sababu za kifo cha mtoto huyo ni nini kutokana na maneno mengi yaliyokuwepo mtaani.

"Tulifukua mwili jana na kuupeleka hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi na majibu ya daktari yalipotoka yalionyesha kwamba huyu mtoto alikufa kutokana na njaa,” amesema Kamanda Maigwa

Akizungumzia tukio hilo, jirani wa familia hiyo, Maria Nko amesema hata kama mtoto huyo alikufa kwa njaa mama yake huyo hakupaswa kumzika mwanaye kama mbwa tena usiku wa manane.

"Kwa kweli hili tukio linaumiza na inaonekana huyu mama alikuwa akimtesa huyu mtoto kutokana na ulemavu aliokuwa nao, inakuwaje hao watoto wake wengine hawajafa na njaa na kwa nini amzike mwenyewe tena?” amehoji.


Source: Mwananchi
Kweli Tanzania tumefikia njaa ya namna hiyo, ya kuua mtoto na kuzika usiku? Hili tukio lina ukakasi
 
Jamani hamna hata majirani, angepewa japo uji tu? Kufa kwa njaa Tz hii😪, ndiyo maana najisikia vibaya nikibakisha chakula nikataka either kukitupa kumbe kuna watu wanakufa njaa, so sad
 
Mtu kazika mwanae kwa uchungu wewe unashauri asizike peke yake wakati wa njaa hamkumsaidia
Kabla hawajamsodoa huyu mama walikuwa wapi kumpa Msaada!! Sasa hata wakichonga midomo hiyo mama akifungwa hao wengine nao si watakufa!? Serekali imuonee huruma kaya Maskini
 
Kama ni kweli basi huyo mkurugenzi aletwe jela hapa Arusha ajikwe tyakko lake.
Akitoka hapa ataheshimu hata kuku wake wa kisasa.
 
Tatizo hapo ni Ulemavu wa huyo Mtoto na sio Njaa kama inavyosemekana. Ni kweli amekufa kwa njaa lakini yupo aliyemuua ambaye alipaswa ampe Chakula na hakumpa.

Swali la Msingi: Kwanini hakumpa chakula Mtoto kwa wakati hata kupelekea kufariki kwa njaa?
 
Back
Top Bottom