Mama Mongella - Aghushi na Kutafuna Mamillioni Ya Pesa!

Apr 27, 2006
26,588
10,374
Mwenyewe Agoma Kuzungumza!

Rais wa Bunge la Afrika, Mama Getrude Mongella, anatuhumiwa kutenda makosa ya kukosa uaminifu, Wizi na utoaji ajira kinyume na taratibu za kazi yake:-

1. WIZI:- anatuhumiwa kutafuna Dola za US, 138,000 ambazo ni sawa na shillingi 180Millioni za Tanzania.

2. UAJIRI:- anatuhumiwa kuajiri ndugu zake kinyume na sheria za kazi yake, akiwemo mkwe wake, yaani mke wa mtoto wake.

Katika kikao cha AU kilichopita nchini Ghana, nchi za Afrika zilimuamuru mama huyo kurudisha hela hizo mara moja huku uchunguzi ukiwa unaendelea, kikao hicho pia kilihudhuriwa na Rais Kikwete.

Mama Mongella, anatuhumiwa kujilipa US/Dola 800, kwa siku akilifanyia kazi bunge hilo la Afrika, na huku akiwalipa US/Dola 400 kwa siku ndugu zake aliowaajiri huko AU, wakati pia akilipwa na bunge la Tanzania kwa kazi hiyo hiyo. Mkwe wake mama huyu tayari ameshaachishwa kazi na bunge hilo na wengine wako njiani kurudishwa tayari Tanzania.

Katibu wa Bunge la Tanzania, ndugu Foka, alithibitisha kupata habari hizo za tuhuma dhidi ya Mama Mongella, na amekiri kwamba ni kweli Bunge letu la Tanzania limekuwa likimlipa mama huyo fedha zote anazostahili akiwa analifanyia kazi bunge la Afrika, kwa mujibu wa makubaliano na bunge hilo la Afrika, ambalo liliwaomba mwanzoni wakati anaanza kuwa liwe linamlipa ili asilipwe na bunge hilo la AU.

Taarifa za uchunguzi tayari zimefanyika na SADC, ikishirikiana na kampuni ya KP GM ya Kenya, ambazo izmeshauri mama huyo kufukuzwa kazi na kurudisha mapesa hayo kwa AU, mara moja. Mbunge mmoja wa bunge hilo la AU, Ndugu Wanyancha,(Serengeti-CCM) amekubali kuwa kweli Mama anakabiliwa nashutuma nzito sana ambazo zitatukosesha urais huo kwa muda mrefu sana ujao, juhudi zote za kuzungumza naye kuhusu hiii sualazimakwama kutokana na kukataa kwake, mama huyo.


Source: Mwana-Halisi.
 
Kama tuhuma hizi ni kweli basi hii ni aibu kubwa, inawezekana hii yote inatokana na mazingira ya rushwa waliyokulia viongozi wetu; wanadhani kuwa huo ndio utaratibu duniani kote. Kuajiri ndugu zako ni namna moja ya rushwa.
 
Inasikitisha sana kwamba Tanzania inaelekea kuipiku kwa kasi naijeria katika utapeli ambao sasa tumefikia ngazi za kimataifa.

Shame on her.Hakujua huko hamna kulindana kama inavyofanyika na kuzoeleka hapa bongo?

This is going to cost us as a nation.
 
Kama uchunguzi umeshafanyika tayari na tuhuma zimethibitishwa kwa nini sheria isichukue mkondo wake kwa nafasi tu...
 
Kama hizo tuhuma ni za kweli basi hiyo itakuwa ni Big soo, sasa sijui hata status yake ya u-diplomat itakuwaje. Hii si aibu tu kwake bali kwa Taifa la Tanzania, maake kiongozi kama huyu kuanza U-TP ni balaa. Mwl. Nyerere akifufuka leo hii na kusikia hayo yaliyofanywa na huyo Mama (Kama ni Kweli), ataweza kutoa machozi. Jamani taasisi zingine si za kufanyia USANII, si BONGO jamani maana huko Bongo angefunikwa na Waheshimiwa wenzake.

Pole Mama kama hiyo soo ni ya KWELI.
 
Kama hizo tuhuma ni za kweli basi hiyo itakuwa ni Big soo, sasa sijui hata status yake ya u-diplomat itakuwaje. Hii si aibu tu kwake bali kwa Taifa la Tanzania, maake kiongozi kama huyu kuanza U-TP ni balaa. Mwl. Nyerere akifufuka leo hii na kusikia hayo yaliyofanywa na huyo Mama (Kama ni Kweli), ataweza kutoa machozi. Jamani taasisi zingine si za kufanyia USANII, si BONGO jamani maana huko Bongo angefunikwa na Waheshimiwa wenzake. Pole Mama kama hiyo soo ni ya KWELI.

Mnakumbuka nilisema. Mkaninanga Asha wa mipasho. kutuhumiwa ametuhumiwa kweli kabisa na anachunguzwa. Ndio maana ameogopa kabisa kujitokeza hadharani kukanusha. Sitashangaa akijinyonga au akaacha kabisa siasa. Imemuumiza sana na kumuaibisha. Tuhuma ameshatuhumiwa na AU wenyewe. Kama watabaini hana hatia hilo ni suala lingine. Lakini mpaka utuhumiwe na taasisi ya kimataifa kama hiyo lazima kutakuwa kuna ukweli fulani fulani. Kwani Mongella hajatoka Chama Cha Mafisadi? Ametuaibisha kabisa wanawake wenzake.

Asha
 
Mama Mongella, anatuhumiwa kujilipa US/Dola 800, kwa siku akilifanyia kazi bunge hilo la Afrika, na huku akiwalipa US/Dola 400 kwa siku ndugu zake aliowaajiri huko AU...
Hivi kumbe wao (AU) hawatambui kale ka'slogan' ketu kanakosema "ukimwelimisha mwanamke..."

Taarifa za uchunguzi tayari zimefanyika na SADC, ikishirikiana na kampuni ya KP GM ya Kenya, ambazo zimeshauri mama huyo kufukuzwa kazi na kurudisha mapesa hayo kwa AU, mara moja.
...naona kina mama nao wanaanza kuingia kwenye orodha ya mafisadi. Lakini hii ya Mongera utakuwa ushindi kwa Msekwa - kwi kwi kwi!
=================
 
if the above story is true then, it is ten steps behind to the women activist against women oppression in Tanzania and Africa at large.

women in Tanzania have always look upon her as an icon. nyimbo kuhusu wanawake walioibeba Tanzania zikiimbwa ni lazima atajwe.
 
...halafu alikuwa anautaka urais wa nchi!

Sasa pale Ikulu sijui ndio ingekuwaje kama angeupata,i'm sure yule mtoto wake ambaye ni DC Kigoma huko labda angempa ubosi wa PCB!

Jamani,hao ndio viongozi wetu...always drooling where theres $$$
 
Mama Migiro usiwachukie watanzania wote kujiepusha na balaa hili alilozua shoga yako. Kama kuna mtanzania na mbrazil wanafaa kwa sifa zote, usimwache mtanzania hata siku moja. Ila usichukue mtanzania asiyefaa eti mradi ni wa Ukerewe au Upareni.
 
if the above story is true then, it is ten steps behind to the women activist against women oppression in Tanzania and Africa at large.

women in Tanzania have always look upon her as an icon. nyimbo kuhusu wanawake walioibeba Tanzania zikiimbwa ni lazima atajwe.
 
Huyu mama hata huko nyuma mambo yake hayako wazi sana. Ukizoea kuiba, huendelea kuiba hata ukweeni. Aibu kubwa sana kwa nchi.

Hivi kweli kwa Afrika, mtu anataka dola 800 kwa siku? Afukuzwe tu na ikibidi hata apelekwe mahakamani. Afadhali tusiwe na rais
kuliko kuwa na rais kibaka.

Hizo ndio conflict of interest tulizokuwa tunaongelea, yaani hata aibu hana. Si ajabu hata hizo pesa za mkwe wake kiasi kazitia ndani.
 
kama tuhuma hizi ni kweli basi hii ni aibu kubwa,

inawezekana hii yote inatokana na mazingira ya rushwa waliyokulia viongozi wetu; wanadhani kuwa huo ndio utaratibu duniani kote. kuajiri ndugu zako ni namna moja ya rushwa.

Itakuwa ni malezi mazuri ya jembe na nyundo!
 
Nadhani zile kelele za kuwa na Rais mwanamke hapa Bongo sasa zimefikia tamati baada ya huyu mama aliyeonekana kuwa mstari wa mbele na kwamba labda angediriki kugombea urais amejichafulia CV yake ivi ivi. Lakini kwa Bongo lolote linaweza kutokea maana hata sielewi sisi wabongo tunapochagua viongozi huwa tunaangalia sifa zipi!!!
 
Kama ni za kweli..ni aibu, tena si ndogo. Jamani mwenye habari za ndani za huyu mama aziaanike hapa, maana tunaweza jua ni kwanini kafanya hivyo. Au ndo kaanza tu na kudakwa..mmh lakini hizi ni za mwizi ni arobaini. JF intelligence we need more data about this beijing icon.
 
Itakuwa ni malezi mazuri ya jembe na nyundo!

CCM Chama Cha Makomunisti.Unaona hilo jembe na nyundo vilivyokuwa positioned? Wameondoa sickle wakaweka jembe.


su.gif


tz&
 
duh, hii shida, Msekwa najua atacheka hadi fizi ya mwisho! Tulishasema correlation kati ya u-CCM na ufisadi is so strong and positive. Halafu inaonekana wale wanaCCM wa wakati wa Nyerere ufisadi wao haukujionyesha kwa kuwa hawakupata nafasi tu, ukiwapa nafasi kidogo wana-prove kwamba ni mafisadi wa kutupa. Si ajabu hata Kingunge naye ndio hivyo tena.

Safari yetu ya kupambana na ufisadi ni futile so long as tunaendelea kuikumbatia CCM!
 
Back
Top Bottom