Mama mkwe ni wazuri pale unapowaheshimu kama mama zenu wazazi else ni nyoka awataki ujinga!!

BASIASI

JF-Expert Member
Sep 20, 2010
9,735
5,003
Pengine ni ndoa nyingi zinalalama na matatizo ya wakwe
ni kweli kwa namna moja ama nyingine akuna aliezaliwa yuko right kila sehemu
ila naombaleo niweke wazi mama mkwe hana matatizo kabisa kabisa kama utampenda na kumheshimu kama mama yakomzazi

nimangalia watoto wengi hasa umri wetu wa kizazi cha jk wamekuwa baada ya kuolewa ama kuoa wanaona wazazi hawana maana tena na hili hutokea hata mzazi kuapa kuliko aende kwenye nyumba ya mwanae kusalimia bora akahudumie wale wezi wa segerea masaa matatu apate thawabu

ndugu zanguni si vyema tuoe na kuishi maisha ya kuogopana ama kutoelewana na wazazi wetu..ikifika ndoa ya aina hii nawaambia ndugu hata huko uendako tarajia moto..nasema moto nimeona wengi wakati ndoa ikianza kunoga wanafika kuwadharau wazazi wao lakini inapofika nyumba ya ndoa ikaanza kuiva kama ndoa mmoja anageuka na kuanza kutoa kshfa kumbe ndio maana umeshindwa kuelewana na mama yangu huna maana wewe sijui hata kwenu uliishije ..yanaibuka matusi mengi ambayo atuwezi kuyaweka hadharani kulinda watoto wanaoingia jamvini

dawa ya mama mkwe:
Yawezekana umekuwa na tatizo gumu la makelele ya mamakwe kwenye ndoa yako zipo dawa nyingi za kuondokana na matatizo kama haya
1..maombi
jitahdi kuongozwa na maombi kwenye ndoa yako sio mpaka kiwake ndio uanze kumuita mungu ooh god ni huyu kweli ni huyu kweli loh malaika watakujibu""si uliomba mwenyewe"" jitahdi mshikiriane kwenye maombi kuna wanandoa wanaishi kama mapaka na sio kwamba awapendani la hasha mama anaingi kitandani anajisalia moto baba akifika ndani nae anajisalia analala hapana hii sio hata shetani mnamkaribisha hata kama mna watoto wenu shikaneni pamoja mungu anapenda maombi ya watu walio nia moja

2..heshima
pengine hujui tatizo lako lakini mamamkwe awana matataizo kabisa kabisa wengi wao hata wakiwa wamekuchukia kama utawaonyesha heshima kama unavyomheshimu mama yako mzazi nakwambia akuna tatizo la mamamkwe kwenye ndoa yako..aijalishi ameongea nini msamehe mpende mpe heshima yake mpe anachostahili hata mkinunua nguo za wazazi mkumbuke uone kama atobadilika ..ukijifanya nundu ule laana inafwata watoto wenu na wewe unaingia kwenye harusi ya mwanao umenuna lakini ndio hivyo kumbe uliikaribisha mwenyewe

3)+ na akili yako

4=usiku mwema wote mungu awabariki muende kusali na kumshukuru kwa kuwalinda mpaka hapo mulipo soma wimbo uliobora 8:6/16
 
Ni tabia ya mtu tu, mama mwingine utakuta ana makelele tu hata kwa wanae, na makelele hayo hayawezi kumalizwa kwa maombi, zaidi hayo maombi yanakufanya uonekane unadeka au unanyanyasika hivyo badala ya kusolve utakuwa unajiongezea sononeko na kujinyanyasa! Mama wengi mbona wako safi tu, ni mtazamo hasi wa wanawake ndy unawaumiza, ujue hata wewe una mama, na pia una kaka ambaye ameoa, hvo ukisema mama wa mwenzako anakuchukia kumbuka pia na wewe una mama na una wifi!
 
kuna mama mkwe wazuri hawana kero lakini kuna mama mkwe hawafai, wakorofi wanapenda kuingilia ndoa za watoto wao, wengi wa mama mkwe wakorofi ni mama wa upande wa mwanaume.
 
Mimi nakubaliana kabisa na mtoa mada, mama mkwe wako kama unamheshimu atakupenda tu kama watoto zake.
 
hapo hakuna formula!

kumheshimu sio guarantee ya kupendwa na mkwe,kama mkwe ana ghubu hata umheshimu vipi imekula kwako. . .

Sema wanandoa waheshimu mama wa wenzi wao haijalishi mstaarabu au ana ghubu,hakuna ambaye anapenda mama yake asiheshimiwe, ukimsoma mkweo na kumchukulia jinsi alivyo haitokusumbua.
 
Mama mkwe anayezungumziwa hapa ni mama mzazi wa mume. Binti keshaolewa sasa mama wa mume anakuwa kikwazo cha maisha. Hii ipo sana na hata huyu mwali anyenyekee na kuheshimu kwa uwezo wake wote baadhi ya wamama wakwe hawabadiliki. Tene tatizo huwa kubwa zaidi iwapo hawa vijana waliooana wanakaa nyumba moja na huyo mama. Tuambiane ukweli.Kijana wa kiume kabla hajaoa anaishi vizuri sana na mamake na mama anampenda sana. Kijana atamnunulia mamake kitenge au kanga au zawadi yoyote anayoona itamfaa mamayake. Kijana akioa, mama anajihisi atawekwa pembeni kwani mapenzi ya kijana yatahamia kwa mkewe. Nilishaona kwenye nyumba moja, mama anakuwa na kisirani zaidi pale kijana wake wa kiume anapomletea mkewe zawadin ya nguo. Hiyo ndo siku macho ya mama mzazi yanakuwa mekundu na mashavu kumvimba. Anaanza hata uchonganishi. Jioni atamwita kijana wake pembeni na kumweleza jinsi mkewe alivyo mhuni. "Ulipoondoka, alikuja mtu akamchukua mkeo wakaenda baa ya jirani kunywa" atamwambia kijana wake. Sina haja ya kukuamnia kitatokea ninin hapo. Kwenye huu mfano niliouona uchonganishi wa kila aina ulifanywa na mama mkwe kwa mwali wake na ugomvi mkubwa ulizuka baina ya wana ndoa. Si kwamba mwali alikuwa na kiburi au kutomheshimu mama mkwe. Mama mkwe akisalimiwa na mwali wake ananyamaza hajibu salamu.Matatizo yalizidi sana mpaka hawa wawili wakaamua kuhama na kwenda kupanga nyumba mbali na kwa mama. Baada ya haspo waliishi kwa amani.
 
mama mkwe anayezungumziwa hapa ni mama mzazi wa mume. Binti keshaolewa sasa mama wa mume anakuwa kikwazo cha maisha. Hii ipo sana na hata huyu mwali anyenyekee na kuheshimu kwa uwezo wake wote baadhi ya wamama wakwe hawabadiliki. Tene tatizo huwa kubwa zaidi iwapo hawa vijana waliooana wanakaa nyumba moja na huyo mama. Tuambiane ukweli.kijana wa kiume kabla hajaoa anaishi vizuri sana na mamake na mama anampenda sana. Kijana atamnunulia mamake kitenge au kanga au zawadi yoyote anayoona itamfaa mamayake. Kijana akioa, mama anajihisi atawekwa pembeni kwani mapenzi ya kijana yatahamia kwa mkewe. Nilishaona kwenye nyumba moja, mama anakuwa na kisirani zaidi pale kijana wake wa kiume anapomletea mkewe zawadin ya nguo. Hiyo ndo siku macho ya mama mzazi yanakuwa mekundu na mashavu kumvimba. Anaanza hata uchonganishi. Jioni atamwita kijana wake pembeni na kumweleza jinsi mkewe alivyo mhuni. "ulipoondoka, alikuja mtu akamchukua mkeo wakaenda baa ya jirani kunywa" atamwambia kijana wake. Sina haja ya kukuamnia kitatokea ninin hapo. Kwenye huu mfano niliouona uchonganishi wa kila aina ulifanywa na mama mkwe kwa mwali wake na ugomvi mkubwa ulizuka baina ya wana ndoa. Si kwamba mwali alikuwa na kiburi au kutomheshimu mama mkwe. Mama mkwe akisalimiwa na mwali wake ananyamaza hajibu salamu.matatizo yalizidi sana mpaka hawa wawili wakaamua kuhama na kwenda kupanga nyumba mbali na kwa mama. Baada ya haspo waliishi kwa amani.

mkuu hygie
hilo jamaa lako ni famba nasikitika kukwambia lilikuwa limeona limeoa kumbe limeolewa na mama yake mzazi.....hiiiiiiiii mitabia ya kuoa unakaa na mama yako upumbavu mtupu unarudi kwenye fungate mama yako anajua kilichoendelea...kuna nyumba nyinmgine mlango wa baba na mama unafwatana unamchaoa mkeo analia usiku mama anaamka anaanza kupiga kelelee achenii upuuzi mnatupigia kelele umeoa umeolewa na familia yenu??embu tukue na hilo tatizo alilitaka mwenyewe ndio maana nimerudi kusema awana noma hawa ukiwajua tu...wewe hisi hata ningekuwa mimi nishazoewa unaniletea zawadi leo hii nyumba hiyo hiyoo hata kama ameoa anamletea mkewe huku naangalia nimekuwa zuzu tena nakuletea vijana wa hapo hapo mtaani na ntatafuta simu ya mkwe nisave namba nimwambie kama uamini piga hii namba uone anapokea nani....

Acheni ujinga ukioa kwenda kwenu katafute maisha hata chumba kimja unahisi wanaoanza kuishi tandale kwa mfuga mbwa tulipenda majukumu yalitushinda ati lazima mtofautishe maisha ya wazazi wenu na yenu kama privacy...hope narudia tena mamamkwe uko juu
 
Sikatai kuwa kuwaheshimu ni kitu cha muhimu, lakini dah......kuna mama wakwe wengine ni disaster by nature!!!
 
Mama mkwe ni mama wa mkeo au mumeo unaempenda sana.
Ana mapungufu kama mama yako pia, ukiona makosa nakubwa sana kafanya, basi wahi kwa mama yako kamuonye asimfanyie mkwewe, yani mke au mume wa nduguyo.
Mama mkwe anahitaji heshima toka kwa watoto kwa asilimia zote. Kama hujaweza kujenga urafiki, jiepushe na kutaka kumrekebisha.
Avoid, avoid, kumzodoa, kuropoka, kutokumtunza, kuwekeana kinyonyo etc.
What do you have to loose?
Mwache aliwazike uzeeni au awe huru na mwanae,
tatiizo ni ile mentality ya kushindana mnashindania nini hasa? Mko katika hali tofauti sana.
 
Back
Top Bottom