Mama mkwe hataki niolewe na mwanaye kisa mimi ni Mchaga

miss chuga

JF-Expert Member
Dec 25, 2019
303
651
Habari zenu wapendwa?

Mwenzenu na matatizo sielewi nichukue uamuzi gani naombeni mnishauri wapendwa, nilianza mahusiano na mkaka wa kimakuwa toka 2016 kiukweli ananipenda sana na Mimi nampenda na Mungu ametujalia mwaka Jana mwezi wa 12 kapeleka mahari kwetu akanivalisha na Pete ya uchumba.

Baada ya hapo wakualiana na wazazi harusi iwe mwezi wa 4 mwaka huu Ila baada ya muda mama yake akamwambia naomba harusi mfanye mwezi wa 7 nataka nijipange sherehe iwe kubwa tukamkubalia kupeleka hadi wa 7 Ila Cha kushangaza juzi kipindi wamekaa kwenye kikao Cha kuandaa kamati ya harusi mama mtu akasema harusi isogezwe tena iwe mwezi wa 10

Baada ya mwanae kumbana mama yake kuwa kwanini kila cku unapeleka mbele akamwambia sitaki uowe mwanamke wa kichaga ndomana nafanya hivi, kiukweli mwanae alichukia sana kuskia hiyo kauli akanipa mrejesho kuwa mama yake hataki anioe kisa mimi mchaga Ila kwakuwa nakupenda tumeshirikiana mambo mengi siwezi kukuacha tutafunga ndoa mwezi wa 8 bila hata ndugu zake kuwepo atasimamia shoo mwenyewe bila msaada wa ndugu zake nikamwitikia sawa.

Ila hapa nawaza usikute huu uamuzi ameuchukua sababu ya hasira nahisi Kama akitulia atanibadilikia asikilize ndugu zake aniache na kinachoniumiza zaidi ni kwamba nimetoka naye mbali kanipotezea muda na hivi kapeleka hadi mahari kwetu watu wanasubiri harusi.

Kama akinibadilikia sijui hii aibu tutaibebaje na familia yangu, nimechanganyikiwa mpaka nawaza sijui nimbebe tu mimba ili azidi kuwa na msimamo aogope kupoteza mke na mtoto!

Ila nakosa jibu huyu mama simuelewi kwanini ananifanyia hivi Kama alikuwa hataki niolewe na mwanae kwanini hakumzuia kipindi anapeleka mahari wakamsapoti apeleke, kinachoniumiza ni aibu kwetu mahari imeenda alafu ikitokea tukiachana kisa mama yake aibu itakuwa kubwa Bora hata angekuwa hajapeleka mahari.

Ndugu zangu naombeni ushauri wenu nifanyaje kulishinda hili jaribu lililopo mbele yangu, Ndugu zangu Bado sijawambia Kama Kuna huu mgogoro maana hata sijui watalipokeaje nachanganyikiwa Mimi jamani
 
Maamuzi anayo mumeo mtarajiwa(mchumba).

Ila angalia miaka 30 mbele, usipokubalika wewe ujue hata wanao, wajukuu wa mama mkwe wako hawatakubalika.

Kama amani hakuna usilazimishe, japo wanaume ni wachache ila bado wako wengi duniani.

Kama una roho ya kupambana ingia ulingoni olewa, ila usilazimishe sasa hivi halafu baada ya miaka 2 ukimbie ndoa kuwa mama mkwe sio... dalili umeziona mapemaaa.

Mapenzi yatakuumiza, ukiyapuuza uliyempenda sana pia unamsahau vilevile na anakuja mwingine anakava nafasi ya jamaa.

NB: Kiukweli nimesoma kichwa cha uzi tuu, uzi wenyewe sijausoma 😜😜
 
Kuna mambo huwa hayalazishwi. Mama na mtoto wana bound ya milele. Mchumba akitenda kinyume na matakwa ya mama ndoa yenu itakua na changamoto nyingi za upumuaji.

Ni afadhali mpate aibu ya kutolewa mahari na kutoolewa kuliko kuishi kwenye ndoa isiyo na amani. Ingekua uko kwenye ligue na mwanamke mwingine ningekishauri usife moyo lakini ligue na mzaa chema ni ngumu sana.
 
Mmmh wakati mahali inapelekwa mama si alikuwa anajua labda kuna mengine ameyasikia anajificha kwny kivuli cha kabila

Kuhusu mimba sio kigezo cha utaolewa wapo wengi walibeba mimba wakaishia kuwa single mother's kama ipo ipo siku hazigandi kuwa na subira uone huo mwezi wa 7 jamaa atafanya maamuzi aliongea au vipi
 
Pole Sana ndg; ila kwa muono wangu mimi huyo jamaa yako Kama atakuwa na msimamo juu yako hakuna kitakachoharibika..

Kaa nae chini myafanyie kazi Tena Kama Bimkubwa Ni msalisali Basi fanyeni mazungumzo na mchungaji wa kanisa lake au mtu yeyoye ambaye mnahisi anaweza kumskiliza..

Ila tatzo lenu wadada wa chuga wengi wenu mnakuwaga ma sistaduu Sana sometimes wew mwenyew unaweza kuwa kikwazo..
 
nakupenda tumeshirikiana mambo mengi siwezi kukuacha tutafunga ndoa mwez wa 8 bila hata ndugu zake kuwepo atasimamia shoo mwenyewe bila msaada wa ndugu zake nikamwitikia sawa,
Japo siungi mkono maneno ya mama mkwe wako ila mumeo hapo Red anataka Kufanya kosa la kiufundi ambal linaweza mghalimu huko mbele...Mshauriane pia after time asifanye maamuzi akiwa anaongozwa na Hisia (Emotions) badala ya Ufikiri (Reasoning).....Nadhani mama mkwe ana hoja za msingi ndio maana alikubali kwa muda then ikatokea hivo. Mumeo akae chini nae kwanza amueleze
wanasubiri harusi Kama akinibadilikia sijui hii aibu tutaibebaje na familia yangu nmechanganyikiwa mpaka nawaza sijui nimbebe tu mimba ili azidi kuwa na msimamo aogope kupoteza mke na mtoto Ila nakosa jibu huyu mama simuelewi kwanini ananifanyia hivi Kama alikuwa hataki niolewe na mwanae kwanini hakumzuia kipindi anapeleka mahari wakamsapoti apeleke kinachoniumiza ni aibu kwetu mahari imeenda alafu ikitokea tukiachana kisa mama yake aibu itakuwa kubwa Bora hata angekuwa hajapeleka mahari.
Tafadhali sana usifanye hivo, utatengeneza akina baba Diamond wengine wasio na ulazima. Don't force it.. If something is destined to be yours it will come, and stay with you forever.
Usibebe mimba ili akuoe au mama mkwe aukukubali You have your dignity, Let Nature handle the destiny.
Ndugu zangu naombeni ushauri wenu nifanyaje kulishinda hili jaribu lililopo mbele yangu, Ndugu zangu Bado sijawambia Kama Kuna huu mgogoro maana hata sijui watalipokeaje nachanganyikiwa Mimi jamani
Yeye aziunganishae nyoyo za watu wawili wapendanao pamoja alifanyie maamuzi jambo hili kadri ya yeye aonavyo inafaa.
Muachie Unayemuabudu jambo hili atalitatua. Usifosi mkuu✌️
 
Hivi ni kweli wanawake wa kichaga wanatabia za kutazama pesa tu kuliko upendo kwa wenza wao, nakumbuka ninipataga demu mchaga veta sasa marafiki wa chuo wakawa wananiambia nimeangukia, mtoto wa watu nilimuacha kimnya kimnya alihangaika kunitafuta harafu alikuwa na msimamo wa upendo kwangh mpaka leo hii namjutia ,kisa marafiki walonipa mastory ya kijinga kuhusu wachaga🙉🙉🙉🙉🙉🙉🙉
 
Pole sana dada,ndoa za kiafrika ndugu wananafasi kubwa sana,shemeji katoa kauli ya kishujaa sana,lakini ajue cost yake ni kubwa na wala haitaishia kwenye ndoa tu,mtakuja pata shida nyingine ndugu watasimama kidedea kuwa jamaa amalize mwenyewe kama alivyofanya katika ndoa.

Lakini mwisho wa siku mapenzi ni ya wawili mtachoamua fanyeni mkijua mtapambana na lolote mbele yenu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom