Mama Mgwhira asisitiza kwamba hajaachia Uenyekiti wa ACT Wazalendo hadi Juni 15

Aliyekuwa mwenyekiti wa ACT wazalendo Anna Mgwira amesema yeye hajapinga kuondolewa uenyekiti wa ACT wazalendo ila amepinga utaratibu uliotumika.

Hapingi utaratibu kwa ajili yake ila ni utaratibu unaotakiwa kuwa kwenye vyama vyote, kuwamteuliwa wa mkutano mkuu hutenguliwa na mkutano mkuu, mteuliwa wa halmashauri kuu pia hutenguliwa na halmashauri kuu na ACT wamefanya haraka mno na alikuwa ameshawaomba wakutane tarehe 15 lakini wakaharakisha

Amewashangaa waandishi wa habari kuchukua habari nusu na kuacha habari za muhimu kwa maendeleo

Chanzo: Millard Ayo

Kwa hiyo lile gongo la udi nilijua litanukia kama alivyosema Ayatollah, ila naona imekuwa kinyume chake, sijui lilikuwa limeeksipaya??
 
Wewe tulia huko uliko fanya kazi,huwezi kuwatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja,either uchague kusuka au kunyoa.
 
Hii ndio siasa ya kibongo yaaan inapasua kichwa vibaya sana duh wanasiasa wote ni wasaka tonge kumkumbuka mwananchi mpaka Siku ya uchaguzi anakupa buku tano utatubu miaka mitano na bahati mbaya wabongo wengi wao awaherewi huu mchezo
 
Mbona "umepanic". Kulikoni?
Kinachokufanya uone nimepanic ni kipi?

Hata chafya sijapiga bado.

Unataka nione kwamba akili yako ni ndogo sana kiasi kwamba pahala ambapo hata chafya sijapiga, umeona nimepanic.

Hujajibu maswali niliyouliza. Tunaenda kwa hoja hapa.

Angalau kama hutaki kujitambulisha kama guluguja.
 
Kinachokufanya uone nimepanic ni kipi?

Hata chafya sijapiga bado.

Unataka nione kwamba akili yako ni ndogo sana kiasi kwamba pahala ambapo hata chafya sijapiga, umeona nimepanic.

Hujajibu maswali niliyouliza. Tunaenda kwa hoja hapa.

Angalau kama hutaki kujitambulisha kama guluguja.
Kwanini CUF na sio Chadema. Kwani Lowasa alihamia CUF?
 
Kwa nini unzunguka mbuyu?
Hujajibu swali langu.

Lowassa anahusiana vipi na mimi au maneno niliyoyasema hapa?

Wewe, kwa kukataa kujibu swali la wazi na linaloeleweka kabisa, ndiye unayezunguka mbuyu.

Mbuyu ni swali langu.

Ili usizunguke mbuyu, unatakiwa kulijibu.

Swali lako ya kuniuliza "Kwa nini unazunguka mbuyu" ni jitihada zakobwewe kuzunguka mbuyu.

Lowassa anahusika vipi na mimi au maneno niliyoandika hapa?

Hujanijibu swali hili.
 
Hijajibu swali langu.

Lowassa anahusiana vipi na mimi au maneno niliyoyasema hapa?

Wewe, kwa kukataa kujibu swali la wazi na linaloeleweka kabisa, ndiye unayezunguka mbuyu.

Mbuyu ni swali langu.

Ili usizunguke mbuyu, unatakiwa kulijibu.

Swali lako ya kuniuliza "Kwa nini unazunguka mbuyu" ni jitihada zakobwewe kuzunguka mbuyu.

Lowassa anahusika vipi na mimi au maneno niliyoandika hapa?

Hujanijibu swali hili.
Ni sawa na kupoteza muda.
 
IMG_-fmunna.jpg

Huyo hapo akiwa kwenye 2nd Community Economic Empowerment Workshop in Dodoma,ashaanza kula posho za WORKSHOP
 
Ni sawa na kupoteza muda.
Kupoteza muda unatupotezea wewe uliyejitoa akili na unayeruka maswali yote unayoulizwa. Unanukuu maswali na kujibu maruweruwe.

Kati yangu ninayeuliza maswali yanayoeleweka na wewe unayejibu majibu yasiyoeleweka wala kujibu maswali niliyoyouliza, nani anapotrza muda?

Wewe ni guluguja unayefikiri kila anayehoji hizi habari ni CHADEMA na hivyo unaweza kumbana kwa maswali ya Lowassa.

Katika kujibiringita kwako kiguluguja haijawahi kutokea ufikiri kwamba mtu asiye CHADEMA wala kumuunga mkono Lowassa anaweza kuhohi suala hiki.

Yaani huo ndio udogo wa upeo wako.
 
MKUU wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amesema hajaachia ngazi yake ya uenyekiti wa Chama cha ACTWazalendo mpaka Juni 15 Kamati Kuu ya chama hicho itakapokaa na kujadiliana kuhusu suala hilo.

Akihojiwa na mwandishi wa habari hizi jana kabla ya kwenda mtamboni kuhusu nafasi yake kwenye chama kukaimiwa na Yeremia Kulwa mpaka Machi mwakani wakati wa uchaguzi mkuu wa chama hicho, Mkuu huyo wa mkoa alisema kwa sasa chama kimemweka kaimu na ni kitu cha kawaida pale mtu mwenye nyadhifa fulani anapokuwa nje ya ofisi.

Alisema, “Sijaacha Uenyekiti, kwa kawaida nikiwa mbali na ofisi au nikiwa nimesafiri, nafasi yangu imekuwa ikikaimiwa ili shughuli za chama ziendelee. “Kwa kuwa nipo Kilimanjaro na nitakuwa na majukumu mengi kwa kipindi hiki, ni sawa nafasi yangu kukaimiwa na mtu mwingine.”

Aidha, Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa leo ataanza kazi na shughuli ya kwanza itakuwa ni kufika ofisini na kusaini kitabu cha mahudhurio kisha atafanya kikao na kamati ya ulinzi ya mkoa huo.

Pia alisema atakutana na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) wa mkoa huo ili kufahamiana na kujua jinsi atatekeleza ilani ya chama hicho, kisha ataenda kuhani msiba wa Mbunge wa zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Philemon Ndesamburo aliyezikwa juzi mjini Moshi.

Baada ya kufanya hivyo atarejea ofisini na kuendelea na majukumu mengine yatakayokuwa mezani kwake. Kwa mujibu wa taarifa ya Kaimu Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Samson Mwigamba iliyotolewa jana, Kamati ya Uongozi (kwa mujibu wa Ibara za 29 (24) ya Katiba ya ACT Wazalendo) ilitangaza kumteua Yeremia Maganja kukaimu nafasi hiyo ya Mghwira mpaka uchaguzi mkuu utakapofanyika.

Chanzo: Mtanzania
Aendelee kubakia ACT awavuruge kama alivovuruga kura za UKAWA,,
 
Kupoteza muda unatupotezea wewe uliyejitoa akili na unayeruka maswali yote unayoulizwa. Unanukuu maswali na kujibu maruweruwe.

Kati yangu ninayeuliza maswali yanayoeleweka na wewe unayejibu majibu yasiyoeleweka wala kujibu maswali niliyoyouliza, nani anapotrza muda?

Wewe ni guluguja unayefikiri kila anayehoji hizi habari ni CHADEMA na hivyo unaweza kumbana kwa maswali ya Lowassa.

Katika kujibiringita kwako kiguluguja haijawahi kutokea ufikiri kwamba mtu asiye CHADEMA wala kumuunga mkono Lowassa anaweza kuhohi suala hiki.

Yaani huo ndio udogo wa upeo wako.
Duh, naona umeamua kuandika insha.
 
Back
Top Bottom