Boniphace Kichonge
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 1,606
- 1,956
Vifo vya watu 20 kwenye mkutano wa mtumishi Boniphace Mwamposa
Kwa mkuu wa mkoa Kilimanjaro Mama Mghwira .
Kauli yako kuwa kulikuwepo na utaratibu mzuri tu kwa watu kukanyaga mafuta ila vibaka waliharibu utaratibu kusababisha maafa yaliyopelekea vifo vya watu 20 haijakaa vema.
Sifahamu chanzo hasa cha vifo hivyo lakini kwa mtazamo wangu majibu yako ni mepesi mno kulinganisha na uzito wa tukio lenyewe.
Mama Mghwira huu ni msiba wa kitaifa na watu wana huzuni kubwa kwa kuwapoteza wapendwa wao.
Ungelitoa nafasi kwa vyombo vya ulinzi na usalama kufanya uchunguzi wa kina na kisha kutoa taarifa.
Taarifa ya uchunguzi huo kwa maoni yangu ingalitolewa na waziri wa mambo ya ndani ya nchi!
Pole sana mama mgwira ila kwa jambo hili natofautiana na wewe.
Mungu azipumzishe mahala pema roho za marehemu
Kwa mkuu wa mkoa Kilimanjaro Mama Mghwira .
Kauli yako kuwa kulikuwepo na utaratibu mzuri tu kwa watu kukanyaga mafuta ila vibaka waliharibu utaratibu kusababisha maafa yaliyopelekea vifo vya watu 20 haijakaa vema.
Sifahamu chanzo hasa cha vifo hivyo lakini kwa mtazamo wangu majibu yako ni mepesi mno kulinganisha na uzito wa tukio lenyewe.
Mama Mghwira huu ni msiba wa kitaifa na watu wana huzuni kubwa kwa kuwapoteza wapendwa wao.
Ungelitoa nafasi kwa vyombo vya ulinzi na usalama kufanya uchunguzi wa kina na kisha kutoa taarifa.
Taarifa ya uchunguzi huo kwa maoni yangu ingalitolewa na waziri wa mambo ya ndani ya nchi!
Pole sana mama mgwira ila kwa jambo hili natofautiana na wewe.
Mungu azipumzishe mahala pema roho za marehemu