JoJiPoJi
JF-Expert Member
- Aug 8, 2009
- 2,907
- 3,260
MJANE wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, ameibuka na kusema kuwa ufisadi umeliangamiza taifa, ndiyo maana maisha ya Watanzania yameendelea kuwa duni hata baada ya kujikomboa kutoka mikononi mwa wakoloni.
Mama Maria alisema hayo jana wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Huduma za Nishati na Ujasiriamali Endelevu - Machame (Machame COSEESE), uliofanyika wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro, ambapo Mwenyekiti wa makampuni ya IPP, Reginald Mengi, alikuwa mgeni rasmi.
Machame COSEESE, imeanzishwa na taasisi isiyokuwa ya kiserikali inayoshughulika na uendelezaji wa teknolojia za nishati endelevu na kuhifadhi mazingira (TaTeDO), wakishirikiana na taasisi inayojishughulisha na uundaji wa vikundi vya kijasiriamali kwa ajili ya kupunguza umaskini (VICOBA).
Huku akionekana mwenye afya njema, Mama Maria alisema siku zote huwa anajiuliza sababu ya umaskini wa Watanzania wakati nchi ina rasilimali za kutosha na hali ya hewa nzuri kwa kilimo na kubaini kuwa umaskini wa Watanzania umetokana na ufisadi.
Siku zote nimekuwa nikijiuliza, kwa nini Watanzania ni maskini wakati wenzetu hasa wale wanaopitiwa na mstari ule wa Ikweta, wanapata maendeleo haraka, hasa zile nchi zenye hali ya hewa nzuri? Tatizo letu ni ufisadi. Rushwa hii itaisha lini? alihoji Mama Maria Nyerere na kushangiliwa na umati wa wananchi wa Machame.
Mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, Dk. Norman Sigalla, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, mama huyo wa taifa alienda mbali kwa kusema kuwa unyonyaji unaofanywa na mafisadi hao ambao hakuwataja majina, umefanya baadhi ya watu kuwataja kwa majina na kufanya hivyo si kuwahukumu bali kutokana na uchungu.
Kwa mujibu wa Mama Maria, ufisadi umelifanya taifa la Tanzania kuendelea kuwa ombaomba wakati liko huru kutoka mikononi mwa wakoloni.
Wengine wanasema Tanzania ni maskini kutokana na kutawaliwa na wakoloni, mimi nafikiri si sahihi kusema umaskini wetu umetokana na kutawaliwa na wakoloni, hiyo isitumike kama sababu ya umaskini wetu, alisema Mama Maria.
Akizungumza kwa hisia kuhusu umaskini, Mama Maria alisema hivi sasa baadhi ya afya za Watanzania ni duni kutokana na kutokuwa na uhakika wa chakula.
Tunahitaji watoto wawe na afya, lishe nzuri kama watu na watoto wa hapa Machame ninavyowaona, nami mnisaidie niwe na afya nzuri. Kwa sasa afya yangu ni nzuri, umri wangu bado si mkubwa sana, natembea na mkongojo kwa sababu tu sina mazoezi, lakini ningekuwa na mazoezi nadhani afya yangu ingekuwa nzuri zaidi kwa sababu taifa linanitunza vizuri, alisema Mama Maria.
Mama huyo wa taifa alimmwagia sifa Mengi kwa kazi anazofanya na moyo wa kujitolea katika kutoa misaada mbalimbali kwa vikundi vya kijamii kwa ajili ya maendeleo yao.
Ukipata pesa, usikimbilie kwenda sehemu kama Zanzibar au sijui wapi kutafuta ukimwi, wape na hawa wengine ili wajikwamue na umaskini kama anavyofanya Mengi, alisema Mama Maria.
Kabla ya kuzungumza na wananchi wa Machame, Mama Maria aliweka shada la maua kwenye kaburi la Dk. Elbenezer Mwasha, ambaye alikuwa daktari wa Mwalimu Nyerere.
Kwa upande wake, Mengi ambaye alitoa hundi ya sh milioni 210 kwa ajili ya taasisi hiyo na watoto yatima na wenye ulemavu wa ngozi (albino), alisema adui mkubwa wa taifa kwa sasa ni ufisadi.
Alisema mafisadi Watanzania, wana roho ngumu, kwani wanatembea kifua mbele na wanapotajwa, wanakimbilia mahakamani.
Watu wakimkamata kibaka, wanampa kibano, lakini mafisadi ukipambana nao, wanakimbilia mahakamani, lakini tunamshukuru Rais Jakaya Kikwete, kinara wa mapambano hayo, ametoa uhuru wa vyombo vya habari kuibua mambo ya ufisadi, kwa sababu yeye si fisadi na ufisadi mwingi ulioibuliwa sasa, ulitokea kabla hajaingia madarakani, alisema Mengi.
Kuhusu ujasiriamali, Mengi ambaye aliwapongeza wananchi wa Machame kwa hatua hiyo, alisema tatizo la watu wengi ni kutojiamini, hasa wanapotaka kuingia kwenye biashara.
Mengi alitumia muda mwingi kueleza jinsi alivyoanza biashara katika mazingira magumu, alisema kilichomfanya afanikiwe hadi kufika mahala alipofika leo, ni kujiamini na kujiona kama anaweza, hata kama hakuwa na uwezo huo.
Akizungumza katika hafla hiyo iliyofana, Mkuu wa Wilaya ya Hai, Dk. Sigalla kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega, alisema Mengi si mkabila kwani shughuli anazozifanya kusaidia vikundi vya kijamii, viko nchi nzima.
Kama humpendi Mengi, basi zipende jitihada zake, lakini inawezekana vipi upende jitihada zake halafu mwenyewe usimpende? alihoji Dk. Sigalla.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa VICOBA nchini, Devota Likokola, ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), alisema kazi anazozifanya Mengi leo, ndizo alizozipigania Mwalimu Nyerere wakati wa uhai wake, kupigana na umaskini na kutetea hali za wanyonge.
Mbunge huyo ambaye alitamba kwamba VICOBA imepiga hatua katika kupambana na umaskini, alisema amedhamiria kupambana na umaskini na sasa taasisi hiyo imesambaa nchi nzima na kuwataka wananchi kujiunga, ili waweze kunufaika. Katika risala yao, wana vikundi vya Machame COSEESE, walisema lengo la kituo hicho cha kwanza na cha aina yake nchini, kina lenga kutoa huduma za sekta ambayo kwenye jamii haijapata msukumo wa kutosha. Kwa mujibu wa risala hiyo, wanachama wa vikundi hivyo wanajishughulisha na ujenzi wa majiko sanifu ya kuni majumbani na kwenye taasisi kama shule, uokaji kwa kutumia matanuri sanifu ya mkaa, ufungaji wa mitambo ya umeme wa jua, vitalu vya miti na shughuli nyingine mbalimbali za ujasiriamali.
Chanzo
Tanzania Daima
Mama Maria alisema hayo jana wakati wa uzinduzi wa Kituo cha Huduma za Nishati na Ujasiriamali Endelevu - Machame (Machame COSEESE), uliofanyika wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro, ambapo Mwenyekiti wa makampuni ya IPP, Reginald Mengi, alikuwa mgeni rasmi.
Machame COSEESE, imeanzishwa na taasisi isiyokuwa ya kiserikali inayoshughulika na uendelezaji wa teknolojia za nishati endelevu na kuhifadhi mazingira (TaTeDO), wakishirikiana na taasisi inayojishughulisha na uundaji wa vikundi vya kijasiriamali kwa ajili ya kupunguza umaskini (VICOBA).
Huku akionekana mwenye afya njema, Mama Maria alisema siku zote huwa anajiuliza sababu ya umaskini wa Watanzania wakati nchi ina rasilimali za kutosha na hali ya hewa nzuri kwa kilimo na kubaini kuwa umaskini wa Watanzania umetokana na ufisadi.
Siku zote nimekuwa nikijiuliza, kwa nini Watanzania ni maskini wakati wenzetu hasa wale wanaopitiwa na mstari ule wa Ikweta, wanapata maendeleo haraka, hasa zile nchi zenye hali ya hewa nzuri? Tatizo letu ni ufisadi. Rushwa hii itaisha lini? alihoji Mama Maria Nyerere na kushangiliwa na umati wa wananchi wa Machame.
Mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, Dk. Norman Sigalla, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, mama huyo wa taifa alienda mbali kwa kusema kuwa unyonyaji unaofanywa na mafisadi hao ambao hakuwataja majina, umefanya baadhi ya watu kuwataja kwa majina na kufanya hivyo si kuwahukumu bali kutokana na uchungu.
Kwa mujibu wa Mama Maria, ufisadi umelifanya taifa la Tanzania kuendelea kuwa ombaomba wakati liko huru kutoka mikononi mwa wakoloni.
Wengine wanasema Tanzania ni maskini kutokana na kutawaliwa na wakoloni, mimi nafikiri si sahihi kusema umaskini wetu umetokana na kutawaliwa na wakoloni, hiyo isitumike kama sababu ya umaskini wetu, alisema Mama Maria.
Akizungumza kwa hisia kuhusu umaskini, Mama Maria alisema hivi sasa baadhi ya afya za Watanzania ni duni kutokana na kutokuwa na uhakika wa chakula.
Tunahitaji watoto wawe na afya, lishe nzuri kama watu na watoto wa hapa Machame ninavyowaona, nami mnisaidie niwe na afya nzuri. Kwa sasa afya yangu ni nzuri, umri wangu bado si mkubwa sana, natembea na mkongojo kwa sababu tu sina mazoezi, lakini ningekuwa na mazoezi nadhani afya yangu ingekuwa nzuri zaidi kwa sababu taifa linanitunza vizuri, alisema Mama Maria.
Mama huyo wa taifa alimmwagia sifa Mengi kwa kazi anazofanya na moyo wa kujitolea katika kutoa misaada mbalimbali kwa vikundi vya kijamii kwa ajili ya maendeleo yao.
Ukipata pesa, usikimbilie kwenda sehemu kama Zanzibar au sijui wapi kutafuta ukimwi, wape na hawa wengine ili wajikwamue na umaskini kama anavyofanya Mengi, alisema Mama Maria.
Kabla ya kuzungumza na wananchi wa Machame, Mama Maria aliweka shada la maua kwenye kaburi la Dk. Elbenezer Mwasha, ambaye alikuwa daktari wa Mwalimu Nyerere.
Kwa upande wake, Mengi ambaye alitoa hundi ya sh milioni 210 kwa ajili ya taasisi hiyo na watoto yatima na wenye ulemavu wa ngozi (albino), alisema adui mkubwa wa taifa kwa sasa ni ufisadi.
Alisema mafisadi Watanzania, wana roho ngumu, kwani wanatembea kifua mbele na wanapotajwa, wanakimbilia mahakamani.
Watu wakimkamata kibaka, wanampa kibano, lakini mafisadi ukipambana nao, wanakimbilia mahakamani, lakini tunamshukuru Rais Jakaya Kikwete, kinara wa mapambano hayo, ametoa uhuru wa vyombo vya habari kuibua mambo ya ufisadi, kwa sababu yeye si fisadi na ufisadi mwingi ulioibuliwa sasa, ulitokea kabla hajaingia madarakani, alisema Mengi.
Kuhusu ujasiriamali, Mengi ambaye aliwapongeza wananchi wa Machame kwa hatua hiyo, alisema tatizo la watu wengi ni kutojiamini, hasa wanapotaka kuingia kwenye biashara.
Mengi alitumia muda mwingi kueleza jinsi alivyoanza biashara katika mazingira magumu, alisema kilichomfanya afanikiwe hadi kufika mahala alipofika leo, ni kujiamini na kujiona kama anaweza, hata kama hakuwa na uwezo huo.
Akizungumza katika hafla hiyo iliyofana, Mkuu wa Wilaya ya Hai, Dk. Sigalla kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega, alisema Mengi si mkabila kwani shughuli anazozifanya kusaidia vikundi vya kijamii, viko nchi nzima.
Kama humpendi Mengi, basi zipende jitihada zake, lakini inawezekana vipi upende jitihada zake halafu mwenyewe usimpende? alihoji Dk. Sigalla.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa VICOBA nchini, Devota Likokola, ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), alisema kazi anazozifanya Mengi leo, ndizo alizozipigania Mwalimu Nyerere wakati wa uhai wake, kupigana na umaskini na kutetea hali za wanyonge.
Mbunge huyo ambaye alitamba kwamba VICOBA imepiga hatua katika kupambana na umaskini, alisema amedhamiria kupambana na umaskini na sasa taasisi hiyo imesambaa nchi nzima na kuwataka wananchi kujiunga, ili waweze kunufaika. Katika risala yao, wana vikundi vya Machame COSEESE, walisema lengo la kituo hicho cha kwanza na cha aina yake nchini, kina lenga kutoa huduma za sekta ambayo kwenye jamii haijapata msukumo wa kutosha. Kwa mujibu wa risala hiyo, wanachama wa vikundi hivyo wanajishughulisha na ujenzi wa majiko sanifu ya kuni majumbani na kwenye taasisi kama shule, uokaji kwa kutumia matanuri sanifu ya mkaa, ufungaji wa mitambo ya umeme wa jua, vitalu vya miti na shughuli nyingine mbalimbali za ujasiriamali.
Chanzo
Tanzania Daima