Mama lishe, kuna soko kubwa la biashara mkiweza kusambaza chakula

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
Biashara ya chakula inauzika na ina uhakika kwasababu kila siku watu wanahitaji kula. Wateja wengi wanavutiwa na ladha ya chakula pamoja na mandhari ya eneo.

Katika maisha ya kila siku huku mtaani, wapo ambao hawana muda wa kupika nyumbani, wanatumia muda mrefu katika shughuli zao za kila siku na hurudi nyumbani usiku wanahitaji kupumzika ili kesho wawahi kwenye shughuli zao.

Wengine ni ma bachelor, shughuli ya kupika na kuosha vyombo kila siku ni ngumu kwao, hasa siku za mvua eti mkaka atoke akanunue dagaa na nyanya aje apike mboga na ugali!

Wengine wana wagonjwa hospitali na hawana muda wa kupika na kupeleka chakula hospital. Unaweza kupata order za lunch maofisini.

Mama lishe wakijiongeza tena kuwa na app, mteja analipia kabisa kwenye simu, unampigia simu mlangoni kwake atoke achukue chakula chake.

1621773386851.jpeg

 
Biashara ya chakula inauzika na ina uhakika kwasababu kila siku watu wanahitaji kula. Wateja wengi wanavutiwa na ladha ya chakula pamoja na mandhari ya eneo.......
Wazo zuri lakini sijui unalenga kuwapa elimu mama lishe wa level/ standard ipi. Maana linapokuja swala la usafi ni changamoto kubwa ya mama lishe wengi. Uki imagine mazingira ya mahali chakula kinapoandaliwa lazima njaa izime.
 
Wazo zuri lakini sijui unalenga kuwapa elimu mama lishe wa level/ standard ipi. Maana linapokuja swala la usafi ni changamoto kubwa ya mama lishe wengi. Uki imagine mazingira ya mahali chakula kinapoandaliwa lazima njaa izime.
Kama serikali ikiweka mkakati wa kupata elimu ya food hygiene kwenye vyuo vya VETA na bila cheti hicho huwezi kuendesha biashara itasaidia sana.
 
Kama serikali ikiweka mkakati wa kupata elimu ya food hygiene kwenye vyuo vya VETA na bila cheti hicho huwezi kuendesha biashara itasaidia sana.
Shida kubwa ni mitaji kwa upande wa mamalishe na sheria butu za mipango miji au halmashauri kuruhusu chakula kupikwa na kuuzwa ktk mazingira yasio faa. Kama waliweza kuwakazia watu wenye mabucha hili nalo linawezekana.
 
Shida kubwa ni mitaji kwa upande wa mamalishe na sheria butu za mipango miji au halmashauri kuruhusu chakula kupikwa na kuuzwa ktk mazingira yasio faa. Kama waliweza kuwakazia watu wenye mabucha hili nalo linawezekana.
Biashara ya chakula ina soko kubwa, wale wenye uwezo na sifa za kuendesha biashara hii, wanaweza kutoa ajira kwa wengine. Fikiria ajira kwa vijana wa boda boda ambao watasambaza vyakula, wapishi na waandaji.
 
Shida kubwa ni mitaji kwa upande wa mamalishe na sheria butu za mipango miji au halmashauri kuruhusu chakula kupikwa na kuuzwa ktk mazingira yasio faa. Kama waliweza kuwakazia watu wenye mabucha hili nalo linawezekana.
Mitaji ipi? Kwani wanapo uza Profit wanapeleka wapi?
 
Chamgamoto ya delivering ni nyumba nyingi kukosa address maalumu, yaani huyo msambazaji atahangaika sana kumpata huyo mtu akiweka oder.
 
Chamgamoto ya delivering ni nyumba nyingi kukosa address maalumu, yaani huyo msambazaji atahangaika sana kumpata huyo mtu akiweka oder.
Ukipewa jina la mtaa ukifika kwenye mtaa unaelekezwa nyumba yenye gate jeusi pembeni ya kanisa kata kushoto.
 
Kua 'mobile' ni gharama ( delivery fee, nk ),

Ku-maintain usafi ( hapa ni tatizo sugu mno) kwa mama lishe ni 'gharama nyingine'

Aki meet izo unakuta lunch peke yake inafika 7000/-

Usafi ni changamoto kubwa kubwa mno, niko tayari kupika/kula 'bokoboko' langu kuliko hawa mama ntilie wa uku 'Mvuti'
 
Naheshimu mawazo yako ila kwangu ni bora niende kula 1500 kwa mama ntilie mtaa wa pili kuliko kukaa geto niagize chakula ambacho ntaletewa na kugharamika 7000, kwasababu hyo 7000, imeizid hata 5000 yangu ambayo ndo bajeti ya kula na nauli ya kwenda kijiweni...

Wazo lako ni zuri sana huko masaki upanga oysterbay na sehemu wanakojenga washua kama ww, ila sisi huku mitaani kwetu bado sana!.

Nawasilisha.
 
Wazo zuri lakini sijui unalenga kuwapa elimu mama lishe wa level/ standard ipi. Maana linapokuja swala la usafi ni changamoto kubwa ya mama lishe wengi. Uki imagine mazingira ya mahali chakula kinapoandaliwa lazima njaa izime.
mazingira machafu sana. wengine wanakuwa na watoto wadogo mtu yuko anakuandalia chakula Mara dogo kajisaidia anatakiwa kusafishwa. Hata Kama wananawa ila hamu ya chakula inaisha muda huo huo.
 
Back
Top Bottom