Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,193
- 25,504
Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Yanga Mama Karume amewataka wanasiasa kutojibanza kwenye mpira kwa ajili ya maslahi yao binafsi. Amewakemea na kuwataka kutoutumia mpira kama ngazi zao za kusaka ngazi mbalimbali za uongozi.
Mama Karume, akiwa ni nembo nyingine ya Wazanzibari ya kutoacha kuusema ukweli popote walipo, hakutoa ujumbe huo kwa bahati mbaya. Katika meza yake alipokuwapo Mgeni Rasmi na hata Mgeni Maalum, Mama Karume alijionea 'mtu' akiwa amevaa fulana ikiandikwa mgongoni 'MAKONDA'.
Mama Karume hakuchelewesha. Alipopata tu nafasi akatuma ujumbe wake mkavu na wa moja kwa moja. Kumbe kuna watu walijiandaa kutafuta umaarufu wa kisiasa kwenye Shughuli ile ya Yanga. Ujumbe wa Mama Karume ukawafikia wahusika palepale.
Ninamuweka Mama Karume kwenye kundi la akina Mzee Moyo, Juma Duni Haji na Maalim Seif kama alama za Wasemakweli Wazanzibari.
Mama Karume, akiwa ni nembo nyingine ya Wazanzibari ya kutoacha kuusema ukweli popote walipo, hakutoa ujumbe huo kwa bahati mbaya. Katika meza yake alipokuwapo Mgeni Rasmi na hata Mgeni Maalum, Mama Karume alijionea 'mtu' akiwa amevaa fulana ikiandikwa mgongoni 'MAKONDA'.
Mama Karume hakuchelewesha. Alipopata tu nafasi akatuma ujumbe wake mkavu na wa moja kwa moja. Kumbe kuna watu walijiandaa kutafuta umaarufu wa kisiasa kwenye Shughuli ile ya Yanga. Ujumbe wa Mama Karume ukawafikia wahusika palepale.
Ninamuweka Mama Karume kwenye kundi la akina Mzee Moyo, Juma Duni Haji na Maalim Seif kama alama za Wasemakweli Wazanzibari.