Mama Kahaba!!!!!

Ligogoma

JF-Expert Member
Aug 27, 2010
3,503
6,376
Mimi ni kijana(mwanaume) na ni mtoto pekee kwa huyu mama.
Ni mama yangu mzazi na kanilea yeye mwenyewe bila baba, na nikimuuliza baba yangu ni nani hanijibu zaidi tunagombana tu!!!
Kanisomesha vizuri sana bila tabu yoyote wala msaada tena kwenye shule expensive sana though sikuwa najua kazi yake (huko utotoni).
Nimemaliza chuo wandugu!! Nimegundua kuwa kazi ya mama yangu kumbe ni UKAHABA na ndiyo kazi iliyonilea, kunivisha, kunisomesha na hata vijigari vya kupigia misele na pia kajenga nyumba nzuuri tunayoishi.
Sasa nina kazi nzuri tuu, na nilipogundua kuwa kazi ya mama ni ukahaba, niliongea na mtu mzima akaongee nae ili aachane na ukahaba ilishindikana, zaidi ya yote alimtukana sana na mie pia nikapata na matusi yangu kiasi.
Pia nikagundua kwanini haelewani na ndugu zake kama dada, kaka, wazazi wake na ndugu wengineo ni sababu ya kazi hiyo na hajali kuhusiana na hilo.
Nishaurini ndugu zangu nifanye nini, kwani kiukweli naona fedheha sana hata raha ya maisha haipo tena kwangu.
 
Mpeleke kwenye maombi ndugu ht km umefanikiwa kwa kazi yake, hapana ukahaba ht biblia inakataza yawezekana ana pepo la ngono.Na mm nitamwombea pia.
 
Mimi ni kijana(mwanaume) na ni mtoto pekee kwa huyu mama.
Ni mama yangu mzazi na kanilea yeye mwenyewe bila baba, na nikimuuliza baba yangu ni nani hanijibu zaidi tunagombana tu!!!
Kanisomesha vizuri sana bila tabu yoyote wala msaada tena kwenye shule expensive sana though sikuwa najua kazi yake (huko utotoni).
Nimemaliza chuo wandugu!! Nimegundua kuwa kazi ya mama yangu kumbe ni UKAHABA na ndiyo kazi iliyonilea, kunivisha, kunisomesha na hata vijigari vya kupigia misele na pia kajenga nyumba nzuuri tunayoishi.
Sasa nina kazi nzuri tuu, na nilipogundua kuwa kazi ya mama ni ukahaba, niliongea na mtu mzima akaongee nae ili aachane na ukahaba ilishindikana, zaidi ya yote alimtukana sana na mie pia nikapata na matusi yangu kiasi.
Pia nikagundua kwanini haelewani na ndugu zake kama dada, kaka, wazazi wake na ndugu wengineo ni sababu ya kazi hiyo na hajali kuhusiana na hilo.
Nishaurini ndugu zangu nifanye nini, kwani kiukweli naona fedheha sana hata raha ya maisha haipo tena kwangu.
 
Hapo sasa unahhitaji kusali sana na kuomba sana maana hataweza kuacha kamwe unless apate UKIMWI lakini hiyo kazi ukianza kuacha ni ngumu mimi kuna msichana alihama kwa mama yake kisa ni hicho alipata kazi nzuri kila akimweleza mama yake wapi ikabidi ahame akapange na nyumba wanayo nzuri tu. Hapo ni maombi tu hakuna kingine
 
It is tough man. Ataacha tu umri utakapo ruhusu, though. You also know why she wo'nt listen to you. Ni ile wanasema yai haliwezi kumfundisha kuku sijui.. It was the business which brought you in the word and made you what you are. Kumbadilisha sasa hivi sio rahisi labda kwa kufanyiwa counseling ya ajabu. Vumila tu .
 
Piga goti kwa mola wako na umuombee atasikiliza sala zako no matter how long it will take
 
Duh pole sana mkuu. Maji yameshamwagika hapo. Mimi naona we kaa mbali na mama yako kama hataki kukuelewa. Mpotezee tu.
 
Get a life man, mshukuru Kwa kufikisha hapo ulipo.....mwache na maisha yake, Kama hataki chapa lapa iwe unam-treat Kama mama Kwa mbalikama vipi...mbona umekaa nae miaka yote? Au tujiela unavyopata sasa ndo unaona maza hayupo sahihi?
 
Pole sana muombee mungu atamuonyesha njia ya kweli ..hasa ukizingatia haya mambo hajaanza jana .
 
Well, huwezi badili historia yako....ila unaweza kubadili maisha yako ya mbeleni....get a life and move!
 
1.usijitafutie laana kwa kutaka aishi maisha safi.
2.Mpende sana mama yako,nae atakupenda sana na kwa kufanya hivyo anaweza akabadilika.
3.kwa mungu hakuna kisichowezekana.
4.Mpe pesa za kutosha na matunzo manzuri...mwenyewe ataacha.
 
Kwanza kitendo cha mamako kujua kwamba na wewe unajua kwamba yeye ni kahaba si kizuri na kinaweza kukuharibia mahusiano yako na mamako. Kama ni mimi nisingethubutu kumshirikisha mtu juu ya hilo. Kwa kuwa una kazi yako nzuri na ya maana, jaribu kumuweka mamako karibu na umkeep busy kwa mambo mengine. Ukiweza hata msaidie kuwa na shughuli nyingine mbadala. Kama kipato chako kinalipa, unaweza hata kumsaidia kwa kumfungulia duka au shughuli yoyote itakayomfanya angalau ahamishe akili yake kuelekea huko. Tafadhari sana, epuka ushauri unaokutaka ukae mbali na mamako. Mzazi bwana, awe na atakavyokuwa kumkaushia kunaweza kukuweka pabaya sana. Mheshimu mpende, muweke karibu zaidi na kumsaidia kwa kumshirikisha katika vishughuli mbalimbali ambavyo vitamfanya akose muda wa kufanya hayo mengine. Pole sana na ninakutakia uvumilivu, busara na hekima katika kukabiliana na hilo.
 
Kumwacha mama yako si jambo la busara kwani hujaweza kujua kwa nini mama yako alijiingiza kwenye biashara ya ukahaba. Inaweza kuwa ni laana ambayo inaweza kwenda kizazi hata kizazi cha msingi ni kumlilia mungu wako na kukemea hizo laana na nguvu za giza katika maisha yako, huku ukizidi kumweka mama kwenye maombi ipo siku roho wa mungu atasema naye. Mkaribishe Yesu katika maisha yako utayashinda hakuna mungu asiloliweza amini hivyo.
 
Pole sana rafikini kweli hii hali lazima ikuweke kwenye wakati mgumu sana, nacho kushauri ni kwamba, usijaribu kutumiambinu za haraka haraka wala za nguvu ya aina yoyote,Unachotakiwa kukumbuka ni kwamba hata mama mwenyewe anajua anafanya makosa,na hakuna mwanadamu aliye tayari kukubali makosa, hata yeye hatokubali kwamba ana kosea na anaweza kutumia mafanikio aliyoyapa kama kielelezo cha kwa nini hawezi kuacha.Kumbuka swala hili halizungumziki, hasa baina yako na yeye, na pia kumbuka wote wanaofahamu kuhusu tabia hizo ama hawana dhamira ya kweli ya kumsaidia au wamekwisha kukata tamaa. Amefanya mambo hayo kwa Muda Mrefu sana na hawezi kuacha mara moja tu ghafla, hili hili litokee inahitajika nguvu ya lazima ya Kimungu.Nakushauri usali na kuliweka swala hili mbele za Mungu aingilie kati,
 
muombe kwanza mungu, funga kwa siku kadhaa , halafu mtoe mama outing kwa ajili ya chakula cha usiku, halafu mueleze linalokukera kwa utaratibu na unyenyekevu mkubwa sana , nadhani atakuelewa kuwa inakuuma rohoni. onesha masikitiko yako lkn kwa unyenyekevu mkubwa nadhani atajirekebisha tu kwani utakuwa umemtanguliza mungu mbele.
 
Pole ndio maisha , maisha yana siri nyingi sana, kuna siri nyingine ukijua zinatesa,
Mpende sana mama yako, usionyeshe tofauti yoyote kati ya sasa na kabla ya kujua kuwa mama yako ni kahaba.Kuwa naye karibu usiongee chochote juu ya maisha yake hayo , Ondoa uchungu moyoni mwako ,uwe huru , onyesho upendo sana, kila unapopata muda kuwa naye karibu usionyeshe hasira, Mtume mtu yuleyule akakuombee samahani na amweleze kuwa vyovyote alivyo unampenda na utampenda. Muombee sana huku ukizidisha upendo, bwana atafanya njia.
 
Hama mji,huwezi kumbadilisha mzazi. Kama huwezi funga domo,fumba macho.
 
Kwani hujafundishwa kuomba? au huamin kua MUNGU yupo na kwamba kwake yeye yote yanawezekana? Usimweleze mwanadamu shida zako mlilie MUNGU ask why haya yanatokea! Kumbuka MUNGU hafundishwi bali mshirikishe haja zko na kwa muda wake atajibu! Washirikishe viongozi wako wa dini na uokoke pia
 
Hii ni hali inayoumiza. Binafsi namfahamu mtu ambaye mama yake alikuwa kahaba wa enzi zile za Mwalimu, mama yule alikuwa anatembea na watu wakubwa kama wabunge, mawaziri na viongozi wa chama na serikali, na hata alizaa mtoto mmoja na kiongozi mmoja wa kitaifa wa enzi zile. Jumla yule mama alizaa watoto wanane, kila mmoja na babake, na wote hao baba vigogo wa chama na serikali. Lakini bado alikuwa anaonekana mrembo sana licha ya uzazi wote huo. Huyo jamaa ninayemfahamu alikuwa mtoto nadhani wa saba, na aliichukulia ile hali kawaida, yaani aliipokea na kusonga na maisha yake. Nakumbuka alikuwa anaaga kwa babu yake kuwa anaenda Dar kumwona dada yake mmoja ambaye ndiye mtoto wa yule aliyekuwa kiongozi wa kitaifa. Sasa hivi jamaa ana biashara nzuri tu kubwa, lakini lililonifanya niseme hiyo hali inaumiza ni ile tabia anayoonesha anapolewa. Ana club yake, akishakunywa whisky zake za kutosha huwa anatukana matusi ya nguoni, anatukana kwa majina watu wote waliozaa na mamake, matusi ya kutisha sana. Hii mimi nachukulia ni frustration inayotokana na hasira juu ya hali hiyo ambayo dhahiri haipendi.

Nakushauri mdogo wangu (au sijui mwanangu), stahimili, usigombane na yaliyopita hutabadili kitu. Jijengee heshima binafsi, itasaidia kumpunguzia mamako hiyo aibu, watasema mama kahaba lakini mwanae mzuri. Pengine inaweza kumsaidia kujirekebisha pia, japo nadhani itachukua muda mrefu.
 
Back
Top Bottom