Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Karibu sana mama, hapa ni TZ pia. Katikati ya jiji la Dar! Panaitwa Tandale sokoni, halafu ficha hiyo blackberry yako. Eneo hili watu hawachati katika facebook itakwenda na maji. Watu wengi wanakuja huku kwa sababu bidhaa zetu tunauza kwa bei nafuu sana, yaani bei ya kutupa. Maharagwe mbeya sh 2000 kwa kg haya ya Iringa sh1800. Mchele supa huu kilo ni sh 2100 kutoka Mbeya mama, huu wa Shinyanga kilo ni sh 1850. Kifuko cha njegere hizo, zimo mia humo utapata kwa buku. Aha kitunguu swaumu kimoja ni sh 300 ......mbona unaondoka tena mama? Bado naendelea kutaja bei!