Mama huyu ufukweni Ocean Road ana kazi gani?

Wanajamii tuangalie jinsi tunavyoweza kumsaidia huyu mama kama kuna mtu yuko tayari tuwasiliane ili tupange cha kufanya ili tuweze kumrudisha kwenye msitari japo kwa asilimia chache email yangu ni oldmoshi@gmail.com au tunaweza kuwasiliana kupitia mada hii kuona jinsi tunavyoweza kukutana kati kati ya jiji na kufanikisha mengine

Huyu Mama haitaji msaada "material": Kwa maoni yangu nadhani anahitaji ushauri nasaha: Ukisoma ile article iliyondikwa na Gazeti la Mwananchi ni kwamba huyu Mama alitendewa ubaya na ndugu wa mme baada ya mme kufariki, and so, it seems, she gave up since then. Na the only choice was "to run away from the society": Watu wote hawaamini!

Kwahiyo, I would suggest, kama kuna madaktari washauri hapa, wanaweza kumfikia in a possible conducive way/manner, na taratibu wakamuweka kwenye "rehab" and thereafter misaada material inaweza kuwa na maana kwake!
 
Wanajamii tuangalie jinsi tunavyoweza kumsaidia huyu mama kama kuna mtu yuko tayari tuwasiliane ili tupange cha kufanya ili tuweze kumrudisha kwenye msitari japo kwa asilimia chache email yangu ni oldmoshi@gmail.com au tunaweza kuwasiliana kupitia mada hii kuona jinsi tunavyoweza kukutana kati kati ya jiji na kufanikisha mengine

Wazo la maana sana, wajibu ni wetu sote. Mlioko mjini jaribuni kufuatilia muone kama yuko tayari kusaidiwa. Naona misheni namba moja iwe watoto-tuwasaidie waende shule. Muenendo mzima uwekwe hapa ili na sisi tulio mashambani tuone namna gani tunawezakusaidia hata yunifomu, nina imani hawa watoto wana fyucha nzuri kama tukiwawezesha (forget about their wicked mother). Tanzania hii ni wengi walokatishwa tamaa na ccm (nyie watu wa morogoro mnamjua Mzee Ally Ally?)
 
Sasa ana kichanga kipyaaaaaaa.
Sijui kazaa na nani?
Halafu sijui hilo tendo walilifanyeje maana yule mama kila aendako huongozana na kundi la wanawe.

Duh kuna baadhi ya wanaume hawana huruma kweli kweli unazaa nae harafu unashindwa kumsaidia loh
 
Kwanini msiwasiliane na ustawi wa jamii[whatever it is]??maanake hata ukitaka ku-sponsor hao watoto naamini lazima upitie huko au jumuia nyingine kama hizo......
 
Mimi nipo tofauti kidogo,, kwasababu mtoas mada kaomba kujua Yule mama anafanyya nini,, hata mimi huwa najiuliza the sama Question lakini sijapata jib Mpaka leo hii.. mimi ninachoomba kwa wale ambao wapo karibu na members walio Selikalini muwazpdoe basi maana mi naona kama hana akili timam vile,, na kuhusu watoto ndo kitu kinaniuma sana maana wanapata shida wasiyo stahili kabisaaaa

kama inawezekana basi si Jamaa wa ustawi wa jamii wamshughulikie? au wawachukue watoto wakawatunze since ewanahitaji kusoma na kuenjoy na watoto wenzao ili kubadilisha uwezo wa kufikiri..

Mimi huwa nasema Mtu anapo ingia Majukumuni Selikalini huwa na Displine nzuri sana na anawajibika ile mbaya, lakini kadiri sikuzinapozidi kuisha Majukum speed ya kazi inapungua mpaka inafikia Zero.. naongea hivi kani kukaa kwake pale mimi nailaum Selikali tu!! kwani they know what to do but they dont like to show their Reactions tena kwa makusudi mazima..

hii inachosha sana ni AFAZALI TUSIWE NA SELIKALI TU, maana hata sioni uwajibikaji wakee:disapointed:

Kwa sababu mama huyu anakaa pale so serikali haifanyi kazi? je serikali ikimsaidia huyu mama utasema ndio serikali ipo kazini?
Anyway...ila maelezo kuhusu huyu mama yanajichanganya sana
1) Huonekana pale masaa fulani tu kwa siku akiwa na wanae waliovaa vema na wana afya nzuri....nachelea kusema kuwa bila shaka kuna mtu au watu wanaomsapoti huyu mama kwa sababu kama angekuwa hali chakula nadhani tusingemwona kila siku pale
2) Huyu mama alikuwa mwalimu miaka ya 70s lakini mpaka leo bado ana uwezo wa kunyonyesha mtoto tehe tehe hii pia ni kali
3) Ninajua social network zinaelekea kufa hapa kwetu lakini bado hainiingii akili kabisa kuamini kuwa hana ndugu kabisa baada ya kufiwa na mumewe!! kama wapo ...je wanajisikiaje na hali hiyo au nao wanangoja serikali ije imnusuru?
Sidhani kama ni attitude nzuri kufikiria kuwa serikali ina majukumu 100% ya matatizo ya aina hii....nina amini kuwa jamii ina jukumu kubwa zaidi ya kufanya katika kunusuru hali hii wakiwemo wababa wa watoto hao.
mix with yours
 
Hivi tujiulize Wizara y unayohusika na usatwi wa jamii kazi yake nini, Maofisa ustawi wa jamii mikooni na wilayani kazi zao nini? Na inawezekana wahusika na wanaofanya kazi kwenye vitengo husika wapo lakini wanamchukulia huyo mama akam sisi wapita njia tunavyomchukulia.

Kuna watu ambao serikalini ngazi ya wilaya na mkoa wanalipwa na nadhani kazi zao inabidi wazunguke kwenye mashule wawasadie watoto na wanafunzi kisaikolojia. au watoe mwongozo kwa walimu kutambua watoto wenye matatizo na kuyaripoti kwao, Viongozi wa mitaa kuripoti familia zenye migogoro na kutishia ustawi wa watoto.Walitakiwa wawe wameshamuona na kumdadisi huyu mama na watu wake wa karibu. Wanaweza wasiwe hata na Rekodi yake

Our society is breaking na kuna watu hawafanyi kazi zao. Watu wanafanya kazi kwa mazoea hakuna anayekuja na Idea za kusaidia watu kama huyu mama kumrudisha japo katika hali yake ya kawaida.

Anayejua number ya kiofisi ya ofisa ustawi wa jamii ilala anipe nimpigie nimuulize kama hii itakuwa ni breaking news kwake au ni jambo la kawaida na hawana cha kufanya?
 
Wasiliana na Gazeti la Mwananchi watakupa "details zote" za huyo Mama:

Pale hana kazi: alikuwa Mwalimu wa Shule za Msingi miaka ya 70 katikati, unfortunately MME wake wa ndoa alifariki late 70s na baada ya hapo maisha yakaenda mrama! Hapo alipo anadai "mafao" yake ya ualimu takribani sh 11m lakini alishawahi kulipwa laki 7 tu!

Kila mtoto aliyenae pale yupo na baba tofauti tofauti: As of late amejifungua mtoto wa 5!

Mkuu baba Enoc,
Ukiongelea miaka ya 70 ni zaidi ya miaka 30! Kama ni hivyo angeshakuwa na watoto wakubwa zaidi ya hao tunaowaona akiongozana nao...na hata mwenyewe anavyoonekana hazidi miaka 40 .... na ndio inaelezea kuendelea kwake kuzaa hadi sasa ana mtoto anayenyonya bado.
 
Wanajamii tuangalie jinsi tunavyoweza kumsaidia huyu mama kama kuna mtu yuko tayari tuwasiliane ili tupange cha kufanya ili tuweze kumrudisha kwenye msitari japo kwa asilimia chache email yangu ni oldmoshi@gmail.com au tunaweza kuwasiliana kupitia mada hii kuona jinsi tunavyoweza kukutana kati kati ya jiji na kufanikisha mengine

Mama anahitaji msaada kweli lakini inabidi wahusika ambao ni watu wa usatwi wa jamii ndo watoe tamko hili. wakati tumnamsaidia mama mimi naomba wanapenda tuunganise nguvu za kuwasukuma ustawi wa jamii wa wilaya au mkoa wamefanya nini kujua tatizo na kumsaidia. wanafanya nini kuwasaidia watu kama hawa?

Kuna baba mmoja nae ilikuwa anajipnaga yeye na watoto wake kuwa omba omba kwa style ya ulokole.wanaimba na kushika biblia. Nadhani ilichukua zaidi ya miezi wakati sehemu alizokuwa anafanya vituko vyake wahusika lazima walikuwa wanamuona.

Ni wakati wa kuanza kuwaamsha usingizini watu waliozea kufanya kazi kwenye madesk tu na kwa mazoea. wakati kazi zao zinahitaji wawe field.
 
Hivi tunajifanya kumuonea huruma kwa vile anakaa Ocean Road? mbona wakina mama wenye watoto wachanga na wenye umri wa kwenda shule wako kibao katikati ya jiji wakiomba omba! Na bila shaka wengi zaidi wako huko kwenye miji mingine na vijijini. Huyu mama hajamkera mtu. Mwacheni aendelee na maisha yake badala ya kumsimanga kwa kuuliza maswali yasiyostahili. Ati kazaa na nani! Inakuhusu nini? Kama unataka kumsaidia fanya hivyo kwa kumheshimu na si kwa kujiona bora kuliko yeye. Tutamsaidia huyu mama kwa kusimama kidete na wanawake wote ambao wanadhulumiwa haki zao. Tutamsaidia huyu mama kama tutasimama kidete pamoja na wale wote ambao waajiri na waliokuwa waajiri wananyima haki zao. Haya machozi ya mamba hayatatufikisha mbali.
Amandla......
 
naombeni nami nitoe yangu machache......mimi humwita mama huyu "MAMA ERICK" Ni mwenyeji wa kigoma ambaye kidogo nadiriki kusema juu hakujatimia.....kuhusu kipi kilichomsibu......mama huyu unapozungumza naye kwa nyakati tofauti huweza kukupa majibu tofautti kwa ufasaha mkubwa na huzuni kuu.....mimi binafsi ameshanisimulia hadithi tatu tofauti kuhusu maisha yake na kilichomsibu mpaka kuwa hapo...LIARS SHOULD HAVE GOOD MEMORY.......kulala , kuhusu sehemu ya kulala inategemea umekujaje.....leo atakwambia ametupiwa mizigo yake hotelini na hawajala toka jana kesho atakwambia huwa analala BP PETREOL STATION NEAR NYUMBA YA SANAA (which is true), keshokutwa atakwambia baba watoto amefariki na ndugu wa mume wamemfukuza....YAANI ITATEGEMEA UMEKUJAJE.......KISHA MZINGA! ...UNA ELFU KUMI HAPO YA KARIBU....!
 
Ni thahiri huyo mama ana akili timamu,yote anayofanya yako nje uwezo wake kiakili.Tatizo liko kwa hawa wanaomzaliasha halafu wanakimbia. Kati ya wanawake wote dar mpaka machangu wameona huyu mama ndiyo wameona kipoozeo chao.kuondokana na hili tatizo ni kuanza “NAME AND SHAME” wat u wanaotembea na huyu mama na pia watoto wadogo wa shule. Picha zao zikiwekwa kwenye tvs ,magazeti na majina yao kutangazwa kwenye radio itasadia kutatua hili tatizo wengine unaweza kukuta ni viongozi serikalini na wana familia.

Hivi mtu anaye mfanya mwanamke kama huyu hawezi kuwa sex offender?
 
Usishangae hao watoto baba zao ni wa Upanga, Masaki, Mikocheni, Mbezi na hata wengine wako hapa JF kama si binamu zao. Nadhani kuna watu wanafanya ngono/wanabaka wanawake wa aina hiyo kwa ajili yakufanikisha mambo wanayoyaamini wao wenyewe na imani zao
 
Wasiliana na Gazeti la Mwananchi watakupa "details zote" za huyo Mama:

Pale hana kazi: alikuwa Mwalimu wa Shule za Msingi miaka ya 70 katikati, unfortunately MME wake wa ndoa alifariki late 70s na baada ya hapo maisha yakaenda mrama! Hapo alipo anadai "mafao" yake ya ualimu takribani sh 11m lak


miaka ya 70,mpaka leo ni zaidi ya miaka 40 tangu kaacha ualimu wake jumliasha umri kabla hajaanza ualimu ni zaidi ya 70!!! mbona haonekani kuwa na umri huo?? sijui labda!!!!
 
mama huyu kwa maelezo yake hupenda (kumradhi)dogo dogo, beach boys ndo baba wa watoto....na ana lugha tatanishi wakati wa usiku....she offers herself to that if you need....! ....."WE RAFIKI YAKE MICHAEL(that baby boy ambaye mimi humuita erick)USIKU WOTE HUU UNATOKA WAPI, AU UNATAFUTA MTU WA KUKULIWAZA,NAJUA USHAGOMBANA NA MDOGO WANGU.....BASI USIANGAIKE JUST COME TO ME HALAFU HIYO ULIYOTAKA WAPA HAO NIWATUNZIE WANAO" alinambia.....!
 
jamani jamani, unapotaka kumasaidia binadamu mwenzako usianze kumchunguza, sijui yuko hivi au yukoo vile, wewe msaidie na wala usiseme mbona wengine hawamsaidii.

mie naanimi yule mama hapendi kukaa pale, wala kuzalishwa kila wakati na midume isiyokuwa na huruma hata kwa malaika wale.

kama umeguswa kama binadamu mwenzako, ni vema mikakati iliyosemwa hapo juu ikaanza ili nae aweze kukaa mahali salama na malaika zake.

masikini huyo mtoto mdogo Dhu!
 
dont think wanaume wanambaka anyway.....nadhani wanatembea nae kwa makubaliano fulani tatizo linakuja anapopata mimba may be wanakuwa hawako shua kama hiyo mimba ina mhusu yeye au lah...pia kama hao wanaume ni watu wa maana 'km wa jf au masaki' wanaogopa stigma itayofuata baada ya kujulikana walitembea na mwanamke ambaye kama hazimtoshi hivi....ukute wanachofanya ni kumpatia hela za matumizi ya kulisha watoto huku wakiwa wamejificha.....
HIVI HUWA ANAZALIA HOSPITALI GANI? NA ZILE SIKU ZA MWANZO ZA KUJIFUNGUA NANI ANA MTAKE CARE.....mimi nadhani tuna lack information za kweli za huyu mama. Anyway in simbo nzuri lets think on wanawake wengi wanaotelekezwa wakiwa na akili timamu/vichaa!
mix with yours
 
''mama huyu kwa maelezo yake hupenda (kumradhi)dogo dogo, beach boys ndo baba wa watoto....na ana lugha tatanishi wakati wa usiku....she offers herself to that if you need....! ....."WE RAFIKI YAKE MICHAEL(that baby boy ambaye mimi humuita erick)USIKU WOTE HUU UNATOKA WAPI, AU UNATAFUTA MTU WA KUKULIWAZA,NAJUA USHAGOMBANA NA MDOGO WANGU.....BASI USIANGAIKE JUST COME TO ME HALAFU HIYO ULIYOTAKA WAPA HAO NIWATUNZIE WANAO" alinambia.....![QUOTE -mahesabu]

Kweli mjini shule nimeamini
 
Huyu mama keshaongelewa sana na bado hakuna anaejali. yaweza kuwa ni mto wa system yuko kazini huyo
 
jamani jamani, unapotaka kumasaidia binadamu mwenzako usianze kumchunguza, sijui yuko hivi au yukoo vile, wewe msaidie na wala usiseme mbona wengine hawamsaidii.

mie naanimi yule mama hapendi kukaa pale, wala kuzalishwa kila wakati na midume isiyokuwa na huruma hata kwa malaika wale.

kama umeguswa kama binadamu mwenzako, ni vema mikakati iliyosemwa hapo juu ikaanza ili nae aweze kukaa mahali salama na malaika zake.

masikini huyo mtoto mdogo Dhu!
Wewe kama una ndugu yako kafukuzwa kwenye nyumba kwa kushidwa kulipa kodi ya pango utamsaidia kulipa bila kujua kwanini alishindwa kulipa na ikiwezeka kumsadia kuondokana na hilo tatizo siku zijazo? hauwezi kutibu maradhi bila kujua chanzo cha maradhi.

Huyu mama hata humpe nyumba na pesa bado anaweza kurudi hapo hapo barabarani. Ni vizuri kumwelewa kwa undani zaidi ili uweze kumwondoa kwenye hilo tatizo
 
dont think wanaume wanambaka anyway.....nadhani wanatembea nae kwa makubaliano fulani tatizo linakuja anapopata mimba may be wanakuwa hawako shua kama hiyo mimba ina mhusu yeye au lah...pia kama hao wanaume ni watu wa maana 'km wa jf au masaki' wanaogopa stigma itayofuata baada ya kujulikana walitembea na mwanamke ambaye kama hazimtoshi hivi....ukute wanachofanya ni kumpatia hela za matumizi ya kulisha watoto huku wakiwa wamejificha.....
HIVI HUWA ANAZALIA HOSPITALI GANI? NA ZILE SIKU ZA MWANZO ZA KUJIFUNGUA NANI ANA MTAKE CARE.....mimi nadhani tuna lack information za kweli za huyu mama. Anyway in simbo nzuri lets think on wanawake wengi wanaotelekezwa wakiwa na akili timamu/vichaa!
mix with yours
Sisi wanaume kusema hauko sure kama mtoto mi wakwako ni kutafuta sababu ya kukimbia responsibilities,kama hauna uhakika msaidie mpaka hatakapo jifungua ukafanye Paternity tests kama mtoto si wa kwako unalaza na kama ni wakwako unasadia, Vinginevyo ni kujaribu kukimbia gharama au Stigma.

Kwa sababu watu wengi wanaogopa stigma ndio njia nzuri ya kuondokana na hili tatizo.Media kama GlobalPublishers wenye weledi wa kupata picha mbali mbali za matukio ya siri wakiamua kulivalia njuga kwa kuweka picha za wanao tembea na huyu mama kwenye magazeti na ustawi wa jamii kuwashinikiza walio mzalisha kuchangia kwenye matumizi itakuwa ndio mwisho wa hili tatizo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom