Katika baadhi ya mabango ya CCM nimeona moja ambalo linaonyesha jinsi rais alivyo mtu wa watu, baadhi ya mabango yanaonyesha rais akiingia katika nyumba za vikongwe pia akikutana na baadhi ya makundi mbalimbali ya watu wenye ulemavu n.k. huenda amewatatulia shida zao kwa kiasi kikubwa ndiyo maana mabango hayo yaewekwa ili watanzania tumfahamu zaidi rais wetu jinsi alivyo karibu na watu hususan wale wenye matatizo.
Naamini hivyo ndivyo alivyo rais wetu pia ndivyo alivyomgombea wa CCM. Kwa wale ambao wanapita barabara ya ocean road au nyuma ya Hospitali ya ocean road watakubaliana na mimi kuwa kuna mama pamoja na watoto wake watano ambaye anahitaji huruma. Mama huyo hayo yamekuwa makazi yake ya kudumu yeye na watoto wake watano ambapo naamini hata hao watoto amewapatia akiwa eneo hilo hilo. mvua na jua na kila hatari zimemzunguka mama huyu na watoto wake watano. Eneo la ocean road ni eneo ambalo mheshimiwa rais anapita kila siku na ninaimani mama huyu anamuona, shida ambayo mama huyu na watoto wake watano ni kubwa ambayo inastahili huruma. Niliposoma mabango haya ambayo yanaonyesha huruma rais aliyonayo kwa watanzania nikasukumwa kuuliza kwamba huruma hizo kwanini zisimuone mama huyu na watoto wake watano? mama huyu yuko jirani sana na Ikulu ni vipi asisaidiwe?
Ukiachilia mbali rais, kuna hii taasisi ya mke wa rais iitwacho WAMA ambapo kila kukichwa tunaona misaada mbalimbali inatolewa na waandishi wa habari wamealikwa kushuhudia misaada ikitolewa ni dhambi kwa taasisi kama WAMA ikitoa msaada kwa watu wenye matatizo maalumu kama mama huyu na watoto wake watano? watotohawa ambao mama huyu analala nao nje nani anawalinda dhidi ya vitendo vya ubakaji na udhalilishaji?
Nakubaliana na ukweli kuwa sio mama huyu tu hapa jijini mwenye matatizo wapo wengi, lakini kwa maisha ambayo mama huyu ambaye nimemzungumzia yanasikitisha sana na anahitaji kusaidiwa. Mama huyu kila nikimuona amekuwa akiniharibia siku yangu kwa uchungu na huruma zinazouzigira moyo wangu. hivyo kwakuwa rais inaonyesha anawajali watanzania basi aanze kwa jirani yake huyu ambaye nafikiri ameamua kuishi karibu na Ikulu ili iwe rahisi kwa rais kumuona na kumsaidia, kama kampeni zimezidia basi atoe maagizo kwa wizara inayohusika na watoto au manispaa ambazo kwa pamoja zingechukua hatua lakini zimelala usingizi na inavyoelekea tatizo la mama huyu hawajui kuwa linawahusu.
Naamini hivyo ndivyo alivyo rais wetu pia ndivyo alivyomgombea wa CCM. Kwa wale ambao wanapita barabara ya ocean road au nyuma ya Hospitali ya ocean road watakubaliana na mimi kuwa kuna mama pamoja na watoto wake watano ambaye anahitaji huruma. Mama huyo hayo yamekuwa makazi yake ya kudumu yeye na watoto wake watano ambapo naamini hata hao watoto amewapatia akiwa eneo hilo hilo. mvua na jua na kila hatari zimemzunguka mama huyu na watoto wake watano. Eneo la ocean road ni eneo ambalo mheshimiwa rais anapita kila siku na ninaimani mama huyu anamuona, shida ambayo mama huyu na watoto wake watano ni kubwa ambayo inastahili huruma. Niliposoma mabango haya ambayo yanaonyesha huruma rais aliyonayo kwa watanzania nikasukumwa kuuliza kwamba huruma hizo kwanini zisimuone mama huyu na watoto wake watano? mama huyu yuko jirani sana na Ikulu ni vipi asisaidiwe?
Ukiachilia mbali rais, kuna hii taasisi ya mke wa rais iitwacho WAMA ambapo kila kukichwa tunaona misaada mbalimbali inatolewa na waandishi wa habari wamealikwa kushuhudia misaada ikitolewa ni dhambi kwa taasisi kama WAMA ikitoa msaada kwa watu wenye matatizo maalumu kama mama huyu na watoto wake watano? watotohawa ambao mama huyu analala nao nje nani anawalinda dhidi ya vitendo vya ubakaji na udhalilishaji?
Nakubaliana na ukweli kuwa sio mama huyu tu hapa jijini mwenye matatizo wapo wengi, lakini kwa maisha ambayo mama huyu ambaye nimemzungumzia yanasikitisha sana na anahitaji kusaidiwa. Mama huyu kila nikimuona amekuwa akiniharibia siku yangu kwa uchungu na huruma zinazouzigira moyo wangu. hivyo kwakuwa rais inaonyesha anawajali watanzania basi aanze kwa jirani yake huyu ambaye nafikiri ameamua kuishi karibu na Ikulu ili iwe rahisi kwa rais kumuona na kumsaidia, kama kampeni zimezidia basi atoe maagizo kwa wizara inayohusika na watoto au manispaa ambazo kwa pamoja zingechukua hatua lakini zimelala usingizi na inavyoelekea tatizo la mama huyu hawajui kuwa linawahusu.