Mama Apigania Mtoto wake wa Kiume Kubadili Jinsia

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,268
33,040


3604398.jpg

Georgie Smith mtoto wa kiume anayepigania kubadili jinsia kuwa mwanamke Tuesday, November 24, 2009 6:22 AM
Mama mmoja nchini Uingereza amewashangaza watu wengi kwa kupigania mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka 14 afanyiwe operesheni ya kubadilisha jinsia yake akidai amezaliwa katika umbile la kiume kimakosa. Mtoto wa mama huyo aliyejulikana kwa jina la Georgie Smith inadaiwa alitaka kuwa mwanamke tangia alipokuwa na umri wa miaka miwili.

Kitengo kinachosimamia huduma za afya nchini Uingereza (NHS) kimemtaka Georgie kusubiri hadi atakapovuka atakapofikisha umri wa miaka 18 ndipo aanze matibabu ya kubadilisha jinsia yake kuwa mwanamke.

"Nina umri wa kutosha kujua nini ninataka, nataka kuwa mwanamke", alisisitiza Georgie.

Mama yake Georgie, Carole mwenye umri wa miaka 41, aliilamu NHS kwa kuzuia matibabu ya kubadilisha jinsia ya mwanae mpaka atakapevuka kwani kwa kusubiria mpaka wakati huo mwili wake utakuwa umejijenga na kumfanya aonekane kama mwanaume.

Carole ambaye ni mama wa watoto watatu alisema kuwa Georgie alitaka kuwa mwanamke tangia alipokuwa na umri wa miaka miwili na aliwahi kujaribu kujiua mara mbili akipinga kuendelea kuwa mwanaume.

Alipokuwa na umri wa miaka minane alikiri mbele ya mama yake kuwa anataka kuwa mwanamke kama mtangazaji wa kipindi cha watoto katika luninga Tracy Beaker.

Kutokana na tabia yake ya kujipodoa na kuvaa nguo za kike, Georgie alikuwa akisumbuliwa na wakati mwingine kuzomewa na wanafunzi wenzake tangia alipokuwa shule ya msingi na alipoingia sekondari alikataliwa kuvaa nguo za kike na kumfanya awe anavaa nguo za kiume lakini akiendelea kujipodoa kama mwanamke.

Carole anasema kuwa aliwahi kufikiria kumpeleka Georgie Marekani kuanza matibabu ya kubadilisha jinsia yake lakini hana uwezo wa kulipa gharama za matibabu zinazokadiriwa kufikia dola 30,000.

Miezi michache iliyopita wanafunzi wawili wa kiume wa shule mbili tofauti za kusini mwa Uingereza walirudi shuleni toka likizo wakiwa wamebadilisha jinsia zao kuwa wanawake na kusabisha mjadala mkubwa kuhusiana na kuongezeka kwa idadi ya wavulana wanaotaka kubadili jinsia kuwa wanawake.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3604398&&Cat=2
 
haya, huu uhuru huu unatucost sana jamani.dunia inakoelekea sijui tu.
 
Anaona mama yake anafaidi kwa babake hivyo nae anahitaji ile kitu roho iko muruwa!
 

Headline:

Lad aged 14 in NHS sex change plea
Synopsis:

A BOY was last night backed by his mum as he begged to begin sex change treatment on the NHS - at the age of just FOURTEEN.

Georgie Smith, who dresses as a girl and wears make-up, insisted: "I'm old enough to know what I want. What I want is to be a girl."

Mum Carole, 41, blasted health chiefs for slapping a ban on youngsters taking sex change drugs until after puberty.

She said it meant that by the time her son is old enough to have an op he will never really look like a woman.

Carole wants Georgie to be given hormone blockers now to stop him turning into a man.

She said: "With his puberty suspended, he wouldn't grow to six foot or have big hands."

The mum-of-three said her boy had wanted to be a girl since the age of two - and had twice attempted suicide after realising he was in the "wrong" body.

School bullies began targeting him at age eight - branding him a "freak".

Georgie - not his real name because The Sun has agreed to protect his identity - asked his Dorset secondary school to let him wear girls' uniform. But he was barred - so he now wears make-up and bangles with the boys' version of the uniform.

Publish date: 23 November 2009
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom