Superbug
JF-Expert Member
- Jan 31, 2018
- 12,383
- 30,836
Kwenye kipindi Cha TBC muda huu mdahalo wa uongozi mama Anna Makinda anasema yeye alikuwa na wenzake 20 ambao ni wapinzani bungeni na anasema walikuwa ni self made opposition. Na walikuwa wakali mpaka Nyerere aliahirisha Safari yake ya Ruvuma akafika bungeni akamwambia Cleopa David Msuya hawa wabunge wa mrengo wa upinzani ndio tunaoutaka, kwahiyo Nyerere aliona umuhimu wa upinzani. Vipi nyie CCM wa Leo kwanini mmeuwa upinzani? Kwa maoni ya mwalimu nyie CCM Leo mnafanya vibaya.
=========
Mama Anna Makinda: Mshahara wa Bunge ulikuwa 345, mshahara wa auditors kama sisi ulikuwa 1600. Nilipata tabu kufanya maamuzi, ikabidi nikubali kubaki Bunge na mshahara wa 345. Watu wakashangaa zaidi, huyu nae kichaa! Ameenda huko, Auditors hawaendagi huko! Lakini nilipata fahari kwa sababu nilikuwa naweza ile kamati yetu ya Bunge, wajumbe 12 na mtoto mdogo nilikuwa mimi na ninayejua masomo hayo kwahiyo nilifanya kazi very actively katika ile kamati.
Siku Mwalimu anamtuma mheshimiwa Butiku aje wanifate mimi niende kwa Mwalimu, mimi namwambia Butiku, mimi sijui Mwalimu anakaaga wapi! Huyu ananiuliza hujui Mwalimu anakaaga Msasani! Ikabidi anipe gari kutoka Ikulu yeye mwenyewe kunipeleka Msasani.
Kufika kule, Mwalimu anafika, eeeh Anna nataka utusaidie serikalini, kama nilivyosema Mwalimu hazoeleki lakini rahisi kumuelewa. Nikasema mbona mimi nafanya kazi kubwa sana, wakati ule decentralization ndio imeanza, watu walikuwa hawawezi kuweka vitabu vizuri, kwahiyo tukasema hao hatuwezi kuwapeleka kusoma lakini unaweza kuwafundisha on the field nini kilichokuwa kinatakiwa, kwahiyo tulikuwa na kaprogram. Nasema mbona nafanya, nakusaidia, mwalimu hakunielewa.
Nimerudi naendelea na mambo yangu, baada ya saa mbili naitwa tena, Anna umeshafanya uamuzi? Akasema mimi ni Rais, nenda tu. Usiku natangazwa kwenye redio eti mimi ni waziri.
Wakati wa Ubunge wetu, mimi nilikuwa 'notorious'. Katika wabunge waliotengeneza upinzani wa kujifanyia wenyewe, sisi tulifanya. Tulikuwa tunasema 'Self made opposition'. Tulikuwa wakali kweli kuliko hata wabunge hawa. Mimi nilikuwa nawaambia nyie hamna lolote, sisi tulikuwa tunafanya kazi ya opposition kwelikweli wala hatukutumwa na mtu.
Mpaka Mwalimu alikuwa na ziara yake Ruvuma, akafika mpaka bungeni, waziri mkuu alikuwa mheshimiwa Msuya, anasema 'Cleopa we want self made opposition'
Tukiwa chama kimoja mtabweteka, sasa hivi inakuja ile point hawa wako chama kimoja, anasema msipokuwa na kitu kama hiki, nyinyi mnabweteka. We need that group ya self, tulikuwa watu kama 20 hivi, sasa sisi ndio tunazinduka, kumbe kulikuwa kuna tatizo!
Tumewanyanyasa kwelikweli na ile sugar scandal, nikasema hapa shughuli kweli, waziri mkuu akawa Sokoine. Mimi niliingia uwaziri wakati hali ya uchumi mwaka 83 ilikuwa ni mbaya sana.
Kwahiyo kazi moja mimi ilikuwa kuratibu upatikanaji wa vitu mbalimbali na kuangalia upungufu maana ulikuwa upungufu wa everything almost.
Siku moja niko kanisani usiku ikaletwa gari, Sokoine alikuwa anakuita saa yoyote, ukienda unawakuta kina Butiku wako kikao full na majenerali wote hapohapo, naingia pale usiku hata sijaelewa.
Waziri mkuu ananiambia utakuwa mwenyekiti wa mali za wahujumu uchumi, kwanza zimetoka wapi hizo mali? (Anacheka).
Kwahiyo tumemsaidia sana Mwalimu, ilikuwa kipindi kigumu kwasababu kulikuwa na upungufu wa bidhaa karibu zote, walioweza kohodhi mali walihodhi, nchi ilikuwa hali ngumu, ukitaka sukari lazima foleni, unga hakuna, chochote hamna, mafuta hakuna, hela za kigeni hakuna. Tulishiriki mpaka kugawa hela za benki kuu.
=========
Mama Anna Makinda: Mshahara wa Bunge ulikuwa 345, mshahara wa auditors kama sisi ulikuwa 1600. Nilipata tabu kufanya maamuzi, ikabidi nikubali kubaki Bunge na mshahara wa 345. Watu wakashangaa zaidi, huyu nae kichaa! Ameenda huko, Auditors hawaendagi huko! Lakini nilipata fahari kwa sababu nilikuwa naweza ile kamati yetu ya Bunge, wajumbe 12 na mtoto mdogo nilikuwa mimi na ninayejua masomo hayo kwahiyo nilifanya kazi very actively katika ile kamati.
Siku Mwalimu anamtuma mheshimiwa Butiku aje wanifate mimi niende kwa Mwalimu, mimi namwambia Butiku, mimi sijui Mwalimu anakaaga wapi! Huyu ananiuliza hujui Mwalimu anakaaga Msasani! Ikabidi anipe gari kutoka Ikulu yeye mwenyewe kunipeleka Msasani.
Kufika kule, Mwalimu anafika, eeeh Anna nataka utusaidie serikalini, kama nilivyosema Mwalimu hazoeleki lakini rahisi kumuelewa. Nikasema mbona mimi nafanya kazi kubwa sana, wakati ule decentralization ndio imeanza, watu walikuwa hawawezi kuweka vitabu vizuri, kwahiyo tukasema hao hatuwezi kuwapeleka kusoma lakini unaweza kuwafundisha on the field nini kilichokuwa kinatakiwa, kwahiyo tulikuwa na kaprogram. Nasema mbona nafanya, nakusaidia, mwalimu hakunielewa.
Nimerudi naendelea na mambo yangu, baada ya saa mbili naitwa tena, Anna umeshafanya uamuzi? Akasema mimi ni Rais, nenda tu. Usiku natangazwa kwenye redio eti mimi ni waziri.
Wakati wa Ubunge wetu, mimi nilikuwa 'notorious'. Katika wabunge waliotengeneza upinzani wa kujifanyia wenyewe, sisi tulifanya. Tulikuwa tunasema 'Self made opposition'. Tulikuwa wakali kweli kuliko hata wabunge hawa. Mimi nilikuwa nawaambia nyie hamna lolote, sisi tulikuwa tunafanya kazi ya opposition kwelikweli wala hatukutumwa na mtu.
Mpaka Mwalimu alikuwa na ziara yake Ruvuma, akafika mpaka bungeni, waziri mkuu alikuwa mheshimiwa Msuya, anasema 'Cleopa we want self made opposition'
Tukiwa chama kimoja mtabweteka, sasa hivi inakuja ile point hawa wako chama kimoja, anasema msipokuwa na kitu kama hiki, nyinyi mnabweteka. We need that group ya self, tulikuwa watu kama 20 hivi, sasa sisi ndio tunazinduka, kumbe kulikuwa kuna tatizo!
Tumewanyanyasa kwelikweli na ile sugar scandal, nikasema hapa shughuli kweli, waziri mkuu akawa Sokoine. Mimi niliingia uwaziri wakati hali ya uchumi mwaka 83 ilikuwa ni mbaya sana.
Kwahiyo kazi moja mimi ilikuwa kuratibu upatikanaji wa vitu mbalimbali na kuangalia upungufu maana ulikuwa upungufu wa everything almost.
Siku moja niko kanisani usiku ikaletwa gari, Sokoine alikuwa anakuita saa yoyote, ukienda unawakuta kina Butiku wako kikao full na majenerali wote hapohapo, naingia pale usiku hata sijaelewa.
Waziri mkuu ananiambia utakuwa mwenyekiti wa mali za wahujumu uchumi, kwanza zimetoka wapi hizo mali? (Anacheka).
Kwahiyo tumemsaidia sana Mwalimu, ilikuwa kipindi kigumu kwasababu kulikuwa na upungufu wa bidhaa karibu zote, walioweza kohodhi mali walihodhi, nchi ilikuwa hali ngumu, ukitaka sukari lazima foleni, unga hakuna, chochote hamna, mafuta hakuna, hela za kigeni hakuna. Tulishiriki mpaka kugawa hela za benki kuu.