Kama kweli tunataka kuendeleza kilimo haya mambo tunatakiwa tuyaangalie kwa uangalifu. Haiwezekani mkulima alime kwa juhudi zake zote, leoa anataka kuuza matunda ya kilimo chake ili ajipatie kipato umwambia hapa nchi itakuwa na njaa, hivyo sivyo.
Ili kukifanya kilimo kivutie wengi ni lazima kuwafanya wao fanya kilimo waonekane wanamabadiliko fulani katika hali zao za maisha. Haiwezekani watu wanalima miaka nenda miaka rudi hawana mabadiliko maisha yao yako vile vile, hali hii haitawavutia vijana kufanya kilimo. Wafanyakazi wanapopata mishahara yao hakuna mtu anayewapangia watumie vipi mapato yao, kwa nini wakulima.
Suluhi la tatizo hili ni sarekali kuongeza akiba ya chakula, ili kupambana na upungufu utakao jitokeza.
Kisha kuwaruhusu wakulima kuuza mazao yao bila bunguza, kipato watakacho kipata kitakuwa motisha kwa wao kuongeza juhudi, pia kuifanya sekta hiyo kuwavutia watu wengi zaidi haswa vijana.