Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kwanza, mdogo wangu alinilalamikia kuwa hawalali usiku kwani kuna malori yanapita usiku wa manane huko Kunduchi yakiwa yamebeba michanga. Tatizo ni kuwa malori haya hupita katika cover of darkness na kuharibu sana barabara na madaraja. Nikamuambia kwanini asifuatilie kwa viongozi wa mtaa pale nyumbani? baada ya kufuatilia akakuta anaambiwa na viongozi kuwa "aliache" suala hilo kwani malori au biashara ni ya mbunge mmoja wa CCM ambaye ni maarufu kwa mambo ya sanaa sanaaa!
Tukiwa tunafikiria nini cha kufanya kutoka maeneo ya Mbezi Beach nako kisa ni hicho hicho. Mdogo alikuwa anashare yanayotokea huko Kunduchi na rafiki yake ambaye naye akasema kule kwao malori hayo yanaletwa kwenye nyumba za uraiani ambapo yanapakua mchanga huo ambao kwa maelezo yake unadaiwa kuwa unaletwa kutoka "Shinyanga" a.k.a kwenye migodi..
Baada ya kupewa taarifa hizo nikaanza kuuliza ni nyumba gani zinazopokea mchanga huo na ni kina nani wanaruhusu mambo hayo kufanyika tena kwa kificho jawabu lake limenitisha. Kumbe watu wenyewe hata huwezi kuwapeleka polisi au kulalamika kwani ndio wenye wenyewe kupitia proxies wao.
Sasa watu kama hawa tunawashughulikiaje? maana kama hadi mchanga wetu ni dili na watu wetu wenyewe kwa tamaa ya fedha wanashiriki kuuza basi sisi yawezekana ni taifa la mazezeta kupita yote yaliyowahi kuwepo duniani - kama yamewahi kuwepo mengine. Au tunaongozwa na magenius wawekezaji!
Tukiwa tunafikiria nini cha kufanya kutoka maeneo ya Mbezi Beach nako kisa ni hicho hicho. Mdogo alikuwa anashare yanayotokea huko Kunduchi na rafiki yake ambaye naye akasema kule kwao malori hayo yanaletwa kwenye nyumba za uraiani ambapo yanapakua mchanga huo ambao kwa maelezo yake unadaiwa kuwa unaletwa kutoka "Shinyanga" a.k.a kwenye migodi..
Baada ya kupewa taarifa hizo nikaanza kuuliza ni nyumba gani zinazopokea mchanga huo na ni kina nani wanaruhusu mambo hayo kufanyika tena kwa kificho jawabu lake limenitisha. Kumbe watu wenyewe hata huwezi kuwapeleka polisi au kulalamika kwani ndio wenye wenyewe kupitia proxies wao.
Sasa watu kama hawa tunawashughulikiaje? maana kama hadi mchanga wetu ni dili na watu wetu wenyewe kwa tamaa ya fedha wanashiriki kuuza basi sisi yawezekana ni taifa la mazezeta kupita yote yaliyowahi kuwepo duniani - kama yamewahi kuwepo mengine. Au tunaongozwa na magenius wawekezaji!