Intelligence Justice
JF-Expert Member
- Oct 23, 2020
- 3,036
- 3,479
Wakuu,
Mjadala unawekwa mezani kuhusu fursa za kiuchumi kutokana na rasilimali asili zilizoko Singida
1. Safu za mlima Sekenke hadi Makutupora ina mkanda wa madini ya Dhahabu. Wajerumani walivuna sana madini hayo na jinsi ya usafirishaji wake ilikuwa wanatumia mitaro ya zege.
2. Zao la Vitunguu ni moja la mazao la aina ya viungo kwenye chakula
3. Zao la korosho kwa kulingana na mazingira ya ustawi wake ni fursa ya kiuchumi kwa kuwa matumizi yake ni mtambuka (mafuta, kitafunwa, kimiminika cha alikoholi)
4. Miti asili ya Mihama inayofanana na minazi ambayo inaishi sio chini ya miaka 300
5. Maziwa yenye uhusiano wa kiasili (Singida na Kindai) moja lina maji chumvi jingine lina maji mchanyiko baridi na magadi yanafaa sana kwa uwekezaji wa kitalii, mapumziko na utafiti;
6. Miamba ya mawe iliyobebana kwa nguvu za asili bila kuanguka yanafaa kwa uwekezaji wa utalii
7. Zao la Alizeti ambapo mazao hayo yanawakilisha upendo na kudumisha uzao wenye furaha-mazao yake yanatumika utengenezaji wa mafuta, makapi/mashudu yake yanatumika kwa ajili ya kulisha mifugo
8. Upatikanaji wa ndege asili wa Kware na Kanga kwa wingi
9. Nyuki, asali na nta
10. Mazao ya karanga, njugu mawe, kunde, na ubuyu (kwa juisi, mafuta na sabuni)
Rasilimali nilizoainisha hapo juu ambazo zinapatikana kwa wingi huko Singida ni fursa pekee kwa watu na serikali kiuchumi na maendeleo
Mjadala unawekwa mezani kuhusu fursa za kiuchumi kutokana na rasilimali asili zilizoko Singida
1. Safu za mlima Sekenke hadi Makutupora ina mkanda wa madini ya Dhahabu. Wajerumani walivuna sana madini hayo na jinsi ya usafirishaji wake ilikuwa wanatumia mitaro ya zege.
2. Zao la Vitunguu ni moja la mazao la aina ya viungo kwenye chakula
3. Zao la korosho kwa kulingana na mazingira ya ustawi wake ni fursa ya kiuchumi kwa kuwa matumizi yake ni mtambuka (mafuta, kitafunwa, kimiminika cha alikoholi)
4. Miti asili ya Mihama inayofanana na minazi ambayo inaishi sio chini ya miaka 300
5. Maziwa yenye uhusiano wa kiasili (Singida na Kindai) moja lina maji chumvi jingine lina maji mchanyiko baridi na magadi yanafaa sana kwa uwekezaji wa kitalii, mapumziko na utafiti;
6. Miamba ya mawe iliyobebana kwa nguvu za asili bila kuanguka yanafaa kwa uwekezaji wa utalii
7. Zao la Alizeti ambapo mazao hayo yanawakilisha upendo na kudumisha uzao wenye furaha-mazao yake yanatumika utengenezaji wa mafuta, makapi/mashudu yake yanatumika kwa ajili ya kulisha mifugo
8. Upatikanaji wa ndege asili wa Kware na Kanga kwa wingi
9. Nyuki, asali na nta
10. Mazao ya karanga, njugu mawe, kunde, na ubuyu (kwa juisi, mafuta na sabuni)
Rasilimali nilizoainisha hapo juu ambazo zinapatikana kwa wingi huko Singida ni fursa pekee kwa watu na serikali kiuchumi na maendeleo