Malezi ya wazazi wa siku hizi na dosari zake!

Hahahaha hahahahahahahah kwenye kukafinya sasa jamani wewe...... Ila mtoto mwenye matusi jamani hapendezi lol..... Mtoto anamwambia mamake "pumbavu" mama mtu anakenua meno tu aiseeee... Yaani hapo namzibua domo lake na kofi moja hilo lazima aumwe homa...... Mimi huwa hawaniachii watoto kabisaaaaaaa sababu ni mwendo wa makofi tu hakuna kipya
Umeolewa kweli? Wewe ndio aina ya kina mama zetu waliobaki wachache dunian...njoo tukiendeleze kizazi bora......isije unaweza kwa watoto wa wenzio tu...wa kwako huwezi...?

Mimi nmekaanza haka katoto kangu kadogo hivi hivi kakiwa na miez nane..naona kamezidi mazoea kudeka na kulia lia kwingi...sipendi ujinga...
 
Ila huu uzi umenikumbusha katoto ka Dada angu ..kale katoto kamelelewa ovyo kabisa..lilitokea tukio kama ilo la msiba tuko msibani katoto kanamwambia mama ake waondoke..mama ake anakaambia subiri tuzike tutaondoka mtoto acha acharuke anamvuta mama ake nguo yani ili mradi amkere wanyanyuke waondoke..yule dada baada ya kuona kero zimezidi akampiga kale katoto kofi .

Kakaanza kujiliza kanabembelezwa kanazidisha sauti mama ake akawa kama anamnon'goneza katoto si kakaropoka "toka hapa ndio maana baba anakupigaga"

Aibu niliona mimi
Hahahahahahhahaha unaona sasa mpaka mtoto anakosa adabu sababu ya kumchekeachekea.... Hapo akilia tu unamwangalia kwa jicho fulani hivi hahahahaha sura umeikunja mtoto anajua mmmh hapa sipo kidogo anaingiwa woga.....
 
Nikufundishe, mtoto akiwa less than 5 years mama ni muhimu sana ila baba unatakiwa kuanza kukaonesha kuwa huna utani hasa kakikosea. Baada ya hapo hasa katika kuvunja ungo uwepo wako ni muhimu. Maana anamuona mama kama mwanamke mwenzie na anataka kuwa na opposite sex. Hapo ndipo mibaba mipuuzi inaweza kutenda upuuzi. Na mtoto wakike kama hajaanza kujamiiana utamuona alivyo free na baba ila akipata boyfriend anakuwa mita 500 na baba. Uzoefu muhimu
Boss ni mzazi mwenyewe tu sisi tumelelewa na mzee pamoja na maza tena home mzee Alikuwa hajui kupiga wala kugombeza mtoto na haongeagi tu.... Ila maza alitunyoosha kweli kweli tena mnoo akikutuma umekataa stiki, umesusa kula fimbo, ukiomba kitu kwa mtu akijua tu kipigo, umetumwa sehemu umechelewa kurudi fimbo,yaani kama vitani vile dingi hana huo Muda maza anakalisha watoto wa kiume jikoni mzee anawaka kwa nini!, maza anamwambia mimi ndiye niliyezaa we subiri tu nifundishe watoto, aseee yaani maza katuburuza kweli kweli hakuna mtoto mtukutu kati yetu.... Yaani ni adabu mwanzo mwisho.... Mimi nasema mama ndiye zaidi kwenye malezi sababu nimeyaona sijahadithiwa...
 
Umeolewa kweli? Wewe ndio aina ya kina mama zetu waliobaki wachache dunian...njoo tukiendeleze kizazi bora......isije unaweza kwa watoto wa wenzio tu...wa kwako huwezi...?

Mimi nmekaanza haka katoto kangu kadogo hivi hivi kakiwa na miez nane..naona kamezidi mazoea kudeka na kulia lia kwingi...sipendi ujinga...
Sijaolewa na sina mtoto ila nilivyolelewa na mamangu ndivyo nitakavyomlea mwanangu.... Yaani nampitisha mulemule
 
Na ndivyo tulivyolelewa wengi wetu..
Acha tu Kuna siku nilijifanya sitaki kupika maza wala hakunijibu kaingia jikoni kapika chakula chake tu.... Kakaa mbele yangu... Yeye na mdogo wangu wanakula, akanambia weka vidole vyako humu uone nitakachokufanya utashinda njaa leo, weee wakamaliza chote nilikaa na njaa jioni nilikimbilia jikoni mwenyew kupika sijawahi teena kugoma kupika
 
Siku hizi wazazi wanawapenda watoto kama property sio kama human beings. Saa nyingine inabidi kuwa tough kidogo ili mtoto awe kama binadamu wengine
Hayo malezi ya kufuga watoto sio mazuri...mtoto anaelekezwa Do's and Donts mapema sana na kadri anavyokuwa. Na muda wa kumshape mtoto seriously ni from 6-12 years ukizembea hapo atakuja kuwa kituko tu badae.

Jukumu la kufanya hayo ni la wote baba na mama.
 
Boss ni mzazi mwenyewe tu sisi tumelelewa na mzee pamoja na maza tena home mzee Alikuwa hajui kupiga wala kugombeza mtoto na haongeagi tu.... Ila maza alitunyoosha kweli kweli tena mnoo akikutuma umekataa stiki, umesusa kula fimbo, ukiomba kitu kwa mtu akijua tu kipigo, umetumwa sehemu umechelewa kurudi fimbo,yaani kama vitani vile dingi hana huo Muda maza anakalisha watoto wa kiume jikoni mzee anawaka kwa nini!, maza anamwambia mimi ndiye niliyezaa we subiri tu nifundishe watoto, aseee yaani maza katuburuza kweli kweli hakuna mtoto mtukutu kati yetu.... Yaani ni adabu mwanzo mwisho.... Mimi nasema mama ndiye zaidi kwenye malezi sababu nimeyaona sijahadithiwa...
Mwambie haka kadada @meeya kanatuletea uzungu hapa...nani kasema malezi ni baba...

Msingi wa kwanza na mwalim wa kwanza wa mtoto ni mama...hata kama mama hupati ushirikiano wa kutosha kutoka kwa baba...haihalalishi kutotekeleza wajibu wako kwa watoto wako...
 
Acha tu Kuna siku nilijifanya sitaki kupika maza wala hakunijibu kaingia jikoni kapika chakula chake tu.... Kakaa mbele yangu... Yeye na mdogo wangu wanakula, akanambia weka vidole vyako humu uone nitakachokufanya utashinda njaa leo, weee wakamaliza chote nilikaa na njaa jioni nilikimbilia jikoni mwenyew kupika sijawahi teena kugoma kupika
Yaani bonge la mama...huyo mama yupo nimletee mwanangu anisaidie kumnyoosha kabla hajaanza kupinda...?
 
Hahahahahaha hongera kwa maza ako

Nakumbuka bi mkubwa ilikuwa akipika kitu sikipendi nikisusa tu kosaaa nachezea kipigo nakalishwa kwenye sahani na lazima Nile,,,,, ila Nampa pongezi sababu mpaka sasa hakuna mwenye jeuri ya kuinua bakuli lake kumjibu bi mkubwa akiongea na tena tukimvuruga kama tupo karibu nae vibao tunachapwa
hahah mama yako ni typically mama wa kiafrika. Hawapendagi utoto ila cha ajabu wewe utamlea mtoto kizembe utadhani huelewi nini kinatakiwa😅😄😃
 
Yaani bonge la mama...huyo mama yupo nimletee mwanangu anisaidie kumnyoosha kabla hajaanza kupinda...?
Utahisi anamwonea bi mkubwa achagui mtoto wa kunyoosha yeyote anaekaa nae ataishi atakavyotaka yeye
 
Back
Top Bottom