Malezi ya wazazi wa siku hizi na dosari zake!

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
10,561
19,054
Jumapili iliyopita nilihudhuria kwenye msiba wa ndugu wa rafiki yangu, Miongoni mwa waombolezaji alikua dada mmoja mwenye miaka kama 26-30, alikuwa na mwanae wa kama miaka minne hivi

Sijui ilikuaje lakini mara yule dogo akaanza kulia na kisha kumvurumishia ngumi na mateke mama yake. Mama mtu akabakia kusema tu " Brian stooop banaa". Mpaka mama mmoja alipokuja akamwambia hiyo ni aibu mwanao hata kama ni mdogo unamuachia akupige hivyo hebu ingieni kule chumbani mkabembelezane

Watoto wote wadogo sio ajabu kuwa na utundu lakini utundu mwingine nahisi kama ni wa kukosa adabu na unaendekezwa na wazazi hasa wakike.

Nimewahi kushuhudia mtoto wa chini ya miaka mitano akiipasua simu ya mama yake kwa makusudi kwa kuibamiza chini na mama mtu anasema "mmmh leo sijui kakasirika nini huyu!" halafu akaanza kumbembeleza!

Kuna mtoto wa shangazi yangu aliwahi kumtupia usoni mfuko wa chips mama yake baada ya kugundua alicholetewa sio alichomuagiza wakati anaenda kazini!

Hapo kwenye msiba baada ya tukio la huyo mama na mtoto watu walisema mengi sana kuhusu dosari za kimalezi za wazazi wa kike wa siku hizi. Kuna mzee mmoja akawa anasema dunia inavokwenda huko baadae hayo mapenzi ya mama na mwana yanaweza kufikia hatua ya aibu zaidi hata mama "kumuonjesha" mwanae atakapo balehe

Sina hakika kama haya mambo ya kudekeza watoto kiasi hiki yalikuwepo zamani ila nahisi mengine ni kuwapotosha watoto kwa kuwapa malezi yasiyofaa.
 
usimnyime mtoto kipigo
Hata kama kupiga unaona vibaya kuna option ya kufinya,unamuita chemba,kama kwenye gari au nje ya pale kidogo,unamfinya sana sehemu tofauti tofauti ili ikusaidie angalau kupunguza hasira kidogo ,maana ukimuanzishia kipigo unaweza mletea madhara,watoto wetu wa Kiswahili ukiwalea kizungu wana misbehave mara mbili yake...
 
Hata kama kupiga unaona vibaya kuna option ya kufinya,unamuita chemba,kama kwenye gari au nje ya pale kidogo,unamfinya sana sehemu tofauti tofauti ili ikusaidie angalau kupunguza hasira kidogo ,maana ukimuanzishia kipigo unaweza mletea madhara,watoto wetu wa Kiswahili ukiwalea kizungu wana misbehave mara mbili yake...
Kuna community zingine kama wahindi na hata wazungu huwa hawawapigi watoto lakini the way wanavyokwenda nao mtoto anafata vile mzazi anavyotaka kutokana na culture yao, watoto wa kizungu tunavyo waona mienendo yao ni kutokana na utamaduni wa jamii nzima, tatizo ni sisi waswahili tunaotaka kuiga, na mchanganyiko wa uzungu na uswahili unatoa tabia ya ajabu
 
Mara nying huwaga kwa sababu asilimia kuwa ya wana wake hao wanalea watoto wenywe labda jukumu la baba mzazi ni kutoa hela ya malezi tu lakin sio kukaa na mtoto wakati wote (mama na baba kulea mtoto kwa pamoja) sasa pale mama anapokuwa yeye mwenywe anakuwa anamlea mtoto kwa upole na ukarimu lakin angekuwepo baba wakati huo lazima mtoto angenyooka.
kwani katika maisha ya mtoto siku zote kuna pande mbili ambapo mzazi moja ni makali wa kumrekebisha mtoto (kichapo) na upande mwingine ni kulea mtoto kuwa mpole (emotional )
 
Wazazi wa kike wanachangia sana malezi mabovu kwa watoto. Tutamlaumu baba mtu ila kuna kipindi akiingilia kati ataambulia kauli "leba nilikua mwenyewe na manesi usinitesee mtoto" "haukunisaidia kupush" "huujui uchungu na maumivu ya kujifungua"

Akina mama wa siku hizi wanadekeza vibaya. Na zile kiss za mdomo uchafu mtupu
 
Wazazi wa kike wanachangia sana malezi mabovu kwa watoto. Tutamlaumu baba mtu ila kuna kipindi akiingilia kati ataambulia kauli "leba nilikua mwenyewe na manesi usinitesee mtoto" "haukunisaidia kupush" "huujui uchungu na maumivu ya kujifungua"

Akina mama wa siku hizi wanadekeza vibaya. Na zile kiss za mdomo uchafu mtupu
Nakazia hapa..... Kuna jirani yangu ana mtoto hapa wa miaka kama mitano hivi toto halielewi lile jamani anamtukana mama yake mama nae anacheka tu, akimtuma kitu hataki yaani anamjibu mamake atakavyo.... Ukiona mtoto huyo anachapwa basi na babake sio mamake


Nilimuuliza siku moja ( mama nonino) malezi gani haya unampa mtoto? Anajichekesha tu hana cha kujibu... Kwakweli wamama ndio wanaoweza kunyoosha watoto au kulemaza watoto sababu Muda mwingi wanashinda nao wao....
 
Unakuta Mama anamwambia mwanae; "Subiri baba yako arudi nimwambie ulichokifanya" hapo unakua umesha mjengea mtoto imani kua kumbe wewe si lolote kwake bali amuogope na kumuheshimu Baba yake tu!

Mtoto anapokosea chukua hatua wewe mwenyewe na sio kujionyesha kwake kua wewe huwezi kumfanya lolote!

Mtoto usimregezee sana wala kumkazia sana.
 
Huu ni ukweli mchungu wanawake wengi hawataki kuukubali. Kisingizio cha usingo maza hakina mashiko. Malezi ya mtoto yanaanzia kwa mama kwanza

Huyo mama jirani aombe sana yasije mpata kama ya yule mama aliyetukanwa na mwanae matusi ya nguon mpaka akafariki kwa mshtuko
Nakazia hapa..... Kuna jirani yangu ana mtoto hapa wa miaka kama mitano hivi toto halielewi lile jamani anamtukana mama yake mama nae anacheka tu, akimtuma kitu hataki yaani anamjibu mamake atakavyo.... Ukiona mtoto huyo anachapwa basi na babake sio mamake


Nilimuuliza siku moja ( mama nonino) malezi gani haya unampa mtoto? Anajichekesha tu hana cha kujibu... Kwakweli wamama ndio wanaoweza kunyoosha watoto au kulemaza watoto sababu Muda mwingi wanashinda nao wao....
 
Huu ni ukweli mchungu wanawake wengi hawataki kuukubali. Kisingizio cha usingo maza hakina mashiko. Malezi ya mtoto yanaanzia kwa mama kwanza

Huyo mama jirani aombe sana yasije mpata kama ya yule mama aliyetukanwa na mwanae matusi ya nguon mpaka akafariki kwa mshtuko
Kunakoelekea atatukanwa tu...
 
36 Reactions
Reply
Back
Top Bottom