Malezi ya Watoto Njiti: Utunzaji wa aina ya Kangaruu wa Mama kwa Mtoto

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
1601470757187.png

Utunzaji wa aina ya Kangaruu wa Mama kwa Mtoto (UKM) ni njia ya utunzaji iliyopewa jina kwa kurejelea jinsi kangaruu wanavyowatunza ndama wao. Njia hii imetambulika kuwa bora sana katika kuwatunza watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini. Njia hii huhusisha kumshika mtoto huku mwili wake ukiguzana na wa mama mchana na usiku. Mtu mwingine anaweza kuchukua nafasi ya mama iwapo hawezi kumshika namna hii wakati wote.

Utafiti unaonyesha kuwa njia ya UKM inapotumika, husaidia kudhibiti kima cha mdundo wa moyo na kupumua kwa watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini. Njia hii pia husaidia kupunguza maambukizi na kumwezesha mtoto kuongeza uzani ifaavyo. Njia hii humsaidia mama kwa kuzidisha utoleshaji wa maziwa, na pia kufanikisha kunyonyesha bila kutumia vyakula vya ziada.

Utaratibu wa UKM

Baada ya ya kumwelezea mama kuhusu utaratibu wa UKM (ama mhudumu mwingine kufanya hivyo) unafaa kufuata hatua zilizopeanwa katika jedwali 8.1
Matayarisho ya UKM
  • Hakikisha kuwa chumba ni safi na chenye kiwangojoto mwafaka.
  • Hakikisha kuwa mama yuko faraghani hivi kwamba anaweza kufungua sehemu ya mbele ya nguo yake na kutoa matiti yake.
  • Mshauri mama aketi au kuegemea barabara.
  • Mvue mtoto nguo zote kwa utaratibu isipokuwa chepeo, nepi na sokisi.
  • Mlaze mtoto tambarare, huku akimtaza mama kwa hali ya uwimawima na kutandazika katikati mwa matiti ya mama, mwili wake ukiguzana na wa mama.
  • Geuza kichwa cha mtoto upande mmoja ili kufungua njia za kupumua. Mweke mtoto katika hali hii kwa saa 24 kila siku, isipokuwa kwa vipindi vifupi vya mapumziko.
  • Mfunike mtoto kwa shuka au gauni la mama, umfunge kwa blanketi ya ziada, kisha umvishe chepeo kichwani.
  • Mnyonyeshe mtoto mara kadhaa, angalau mara 8 -12 kila siku.
pnc_session8_fig4.jpg

Mchoro 8.4
Mtoto na Mama wanaweza kulala panoja wakati wa UKM.

Mhakikishie mama kuwa mtoto anaweza kupokea utunzaji muhimu wa kila siku, ikiwa ni pamoja na kunyonyesha, wakati wa UKM. Mtoto huondolewa kutoka hali ya kuguzana na mama wakati wa kumbadilisha nepi, usafi wa jumla wa kimwili, utunzaji wa kitovu na uchunguzi wakati wa ziara. Mama anahitaji kulala kitandani siku 3 - 5 tu za kwanza baada ya kuzaa. Hali ya mtoto inapokuwa dhabiti, mama anaweza kutembea na kufanya kazi zake za kawaida huku mtoto akiwa katika UKM, na wanaweza kulala pamoja usiku wakifuata njia ya UKM.

Kubaini kama mtoto yuko salama katika UKM

Katika kila ziara ya baada ya kuzaa unafaa:
  • Kukadiria kima cha kupumua cha mtoto, ukihakikisha kuwa hapumui kwa kasi sana.
  • Kuhakikisha kuwa mtoto analishwa vyema.
  • Kupima kiwangojoto cha mwili cha mtoto kwapani, ukihakikisha kuwa ni cha kawaida.
  • Kama mtoto yuko salama, Kuidhibitishia familia, iwapo mtoto yuko salama, lakini uwaarifu watafute msaada wako punde wanapokumbwa na tatizo lolote.
Kumshauri mama na familia kuhusu umuhimu wa UKM

Njia ya UKM inaweza kuonekana kama njia isiyo ya kawaida ya kumtunza mtoto. Kwa hivyo, ni muhimu kuchukua muda unapomshauri mama, baba na familia kuhusuvipengele vya njia hii na manufaa yake. Mama (na familia) wanapaswa kushawishika na kukubali kutumia njia hii kwa siku nyingi mfululizo. Baba na watu wengine wa familia pia wanapaswa kuwa tayari kutoa usaidizi wa kimwili na kihisia kwa mama anapotumia njia ya UKM

Umuhimu wa UKM ni nini?

Kunyonyesha: UKM huimarisha kima cha unyonyeshaji na muda wa kunyonyesha.
  • Udhibiti wa joto mwilini: kuguzana kwa muda mrefu kwa mwili wa mama na mwanawe aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula wa ujauzito/aliye na uzani wa chini husaidia kudhibiti kiwango cha joto mwilini mwa mtoto na pia kupunguza hipothemia.
  • Kuongezeka kwa uzani mapema: watoto wembamba huongeza uzani wakitumia UKM kuliko wakitumia utunzaji wa kawaida baada ya kuzaliwa
  • Vifo kupunguka: watoto wanaotumia huduma hii ya UKM wanapumua kwa ubora zaidi na uwezekano kukoma kupumua ni wa kima cha chini. Njia hii pia humkinga mtoto dhidi ya maambukizi.
Kwa kweli inaweza kuwa vigumu kwa kina mama wote kutumia UKM. Kwa hivyo, ni sharti uhakikishe kuwa mama hana matatizo au maradhi yoyote yanayoashiria kuwa anakosa nguvu za kutumia njia hii bila kusaidiwa. Ikiwa anakumbwa na matatizo haya, unapaswa kubaini kama baba au jamaa yeyote wa familia anaweza kushirikiana na mama kutoa utunzaji huu au kumtunza mtoto kwa njia hii wakati wote iwapo mama anaugua. Hatimaye, kina mama ambao wameweza kutoa utunzaji huu kikamilifu wana ujasiri mwingi mbali na kuridhika kuwa wanaweza kuwafanyia jambo spesheli watoto wao.

8.5.4 UKM inafaa kufanywa kwa muda gani?

Ikiwa mama na mtoto wanaridhika kutumia njia hii, inafaa kueendelezwa kwa kipindi kirefu kama inavyowezekana au mpaka mtoto ahitimu muhula wa kuzaliwa (wiki 40) ama mpaka mtoto apate uzani wa gramu 2,500. Iwapo mtoto ana uzani unaozidi gramu 1 800 na kiwango chake cha jotomwili ni dhabiti, hana matatizo yoyote ya kupumua na ananyonya vizuri, anaweza kulishwa kupitia UKM kabla ya wiki 40. Mtoto anapotosheka na UKM humdhiirishia mama yake kupitia, kugaagaa, kuchezacheza, kuondoa miguu na mikono yake kutoka kwenye nguo zilizomfunika na kulia hadi afunuliwe.

Hatimaye, ukifuata maagizo haya na kuwasaidia familia zako kutunza watoto wao waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula au waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini kama ilivyoelezwa katika Kipindi hiki, ni hakika kuwa utaokoa maisha ya watoto wengi wachanga. Kunalo jambo muhimu kuliko hili?

Muhtasari ya Kipindi cha 8

Katika Kipindi cha 8 umejifunza kuwa:
  1. Watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na wale wenye uzani wa chini wamo katika hatari ya kufa kufuatia maambukizi, matatizo ya kupumua na hipothemia kwa kuwa hawajakomaa.
  2. Punde tu wanapozaliwa ni muhimu kuainisha watoto waliozaliwa kabla ya kuhitimu muhula na wale waliozaliwa wakiwa na uzani wa chini kulingana na umri wao wa ujauzito na uzani wao wa kuzaliwa, na kupendekeza rufaa kwa wale waliozaliwa wakiwa na umri wa ujauzito wa chini mno na wale walio na uzani wa chini sana.
  3. Unaweza kumshauri mama kikamilifu kuhusu namna ya kumnyonyesha mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula na waliyezaliwa akiwa na uzani wa chini, ikiwemo kumlisha baada ya kila saa mbili. Unafaa pia kumfunza jinsi ya kujikamua na namna ya kumnywesha mtoto kwa kikombe ikiwa mtoto hawezi kunyonya vyema kwa kuwa hajakomaa.
  4. Unaweza kumfunza mama na familia yake jinsi ya kutoa Utunzaji wa aina ya Kangaroo ya Mama kwa Mtoto (UKM) na kuwaelezea manufaa ya njia hii, ambayo ni pamoja na kuendeleza kunyonyesha, kudhibiti jotomwili la mtoto, kuongeza uzani mapema, kupumua vyema zaidi na upungufu wa kima cha maambukizi.
  5. UKM huendelezwa usiku na mchana hadi mtoto aliyezaliwa kabla ya kuhitimu muhula anapofikisha umri wa wiki 40 au mtoto aliyezaliwa akiwa na uzani wa chini anapofikisha angalau gramu 1,800. Mama atahitaji usaidizi zaidi ili kukabiliana na changamoto za UMK.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom