Malezi ya sasa bado siyaelewi

Balvejmumt

JF-Expert Member
Aug 10, 2015
2,149
2,784
Habarini wakuu,

Mimi si mwandishi mzuri lakini naomba tusaidiane katika hili.

Naomba nianze na visa kama viwili nilivyokutana navyo siku za karibuni

Wiki mbili zilizopita,

Wakati nipo mapumziko ya kimatembezi baada ya kuihudumia jamii yangu kwenye masuala ya kitabibu ndipo nilipo kutana na hili tukio la kwanza. Ambapo niliitwa na Bibi ambaye Yuko jirani na taasisi ninayoifanyia kazi ambaye alikuwa akiambatana na kijana wake (mjukuu wa kiume) age ni kama 17-19 hivi ,sababu zilizompelekea Bibi huyo kuniita ni kunifanyia utambulisho kwa mjukuu wake huyo wa kiume ambaye mara nyingi alikuwa akija ofisini huniambia anamjukuu wake anasomea Udaktari, nilisalimiana naye na swali la kwanza nilimuuliza unasoma chuo gani? Namna alivyofungua mdomo Tu na kuanza kuzungumza huku akirembua na namna alivyosimama kulinipa wasi wasi mkubwa wa jinsia yake.

Alinijibu kuwa Yuko A-level kwenye combination ya science akipambana nayo huko.

Baada ya Hilo jibu, nikaona ngoja niende maana sioni cha muhimu nilimsihi tu apambane katika elimu na dhamira aliyo nayo

Kisa cha Pili ni hivi majuzi,

Alikuja msichana age 23-27 hivi akiwa na mtoto wa kiume age ni 2.5 hivi

Niwapo katika majukumu yangu nina katabia fulani baada ya kunielezea kilichokutoa nyumbani huwa na tabia ya kuunganisha au kujaribu kutizama tatizo lako usikute limechangiwa na tabia tulizo nazo kwenye jamii.

Baada ya kujua tatizo la mtoto nilianza kumtizama na kumfanyia uchunguzi nikagundua katika moja ya vidole vya mikono mtoto kapakwa rangi, sikuhangaika kumuuliza mama kulikoni?

Nilimuuliza baada ya kugundua mikono yote na miguu imepakwa rangi, nikamuuliza kwa upole mama imekuwaje mtoto wa kiume kupakwa rangi mikononi na miguuni tena yote? Akanieleza kuwa wenzie ndio walio mpaka, ikabidi niwe mkali kidogo kwenye kuhoji ndipo nilipo gundua ni Mama ndiye kafanya hiyo kazi ya kumpaka mtoto rangi mikononi na miguuni.

Kwanini nimeleta hii mada kwenu?

Nimeileta baada ya kuwaza na kujiuliza hawa watoto wote wawili yule wa kwanza na huyu wa pili ijapokuwa ni mdogo wote wanalelewa na mzazi mmoja (single parent) nikiwa na maana wanalelewa na mama pekee lakini maadili na ukuzwaji uko sahihi? Hasa linapokuja suala la mtoto wa kiume kulelewa kwenye maadili au muundo wa jinsia ya kike?

Mimi ni miongoni mwa vijana wa kale tuliolelewa na mzazi mmoja (mzazi wa kike) lakini hatukuwa hivyo kama tuonavyo katika makuzi ya kizazi hiki cha sasa kinacholelewa na vijana age 27-45 . .. Simaanishi wote hapana.

Najiuliza tunaenda kuwa na kizazi cha aina gani baada ya miaka 50? Je, ni jukumu la nani kuhakikisha haya madhila ninayo yawaza kipindi kijacho ni Nani wakulaumiwa?

Bado sielewi!

Balvejmumt

2022
 
Mkuu ulichukua uamuzi gani wa kumuelimisha huyo binti kwa kumpaka rangi mwanae wa kiume?
Ungeanza na huyo kwanza coz alikua mbele yako.
 
Utasikia wanasema tunaenda na wakati, utandawazi mara ndio fashion ya siku hizi

Wazazi simamieni majukumu yenu ya kimalezi kwa usahihi msije mkalea watoto wasio na maadili
 
Mashoga walikuwepo hata miaka 3000 iliyopita na wataendelea kuwepo.
Na sasa media zinatumika kuupromote ushoga
 
Mashoga walikuwepo hata miaka 3000 iliyopita na wataendelea kuwepo.
Na sasa media zinatumika kuupromote ushoga
Unataka kusema nini hapa?

But hili tatizo linaendelea kukua,haimaanishi kua mashoga kuwepo toka zamani basi jitihada za kuielimisha jamii ubaya wa ushoga zisifanyike, hata wezi wapo toka kitambo ila haimaanishi kusiwe na jitihada za kupambana na wezi.
 
Hawa single mothers wanaweza kuwa na madhaifu yao lakini haipaswi kusahau kuwa hawakujizalisha wenyewe. Kuna kundi kubwa pia la wanaume wameyaacha majukumu yao tena wengine kwa makusudi kwa kulinda ndoa zao au tu kutokuwa tayari kuyavaa majukumu ya kuwa "Baba" wakiamini ipo siku "mbegu" zao zitawatafuta

Pia hawa single mothers bado wana makaka na baba zao ambao wote walifaa kuwa na jukumu la kuwa male figures kwa ndugu yao. Wanaposhindwa au kuacha kuwa, nani wa kulaumiwa

Hata hao watoto wanapokuja kuharibikiwa huwa wanaharibiwa na wanaume kama mimi au wewe. Kwa hiyo wanaume hatuwezi kuepuka lawama ya hili suala

msiwatumie kama scapegoats, we are not dead wakati haya yakitendeka, tunatazama na tunashiriki kulikuza aidha directly au indirectly
 
kuna mmoja alibeba ujauzito akitamani kupata mtoto wa kike, akaja jifungua wa kiume, basi akawa na mchezo wa kumvisha nguo za kike, anampaka wanja anamvalisha magauni siku naenda namkuta na hiyo hali nikamwambia tu unamfundisha mtoto kuikataa jinsia yake mapema sana, na hizo tabia za kishoga ndio hua zingine zinaanza kwa style hio shukuru hicho ulichoruzukiwa ndicho unacho stahiki
 
Kuna jamaa alipanga nyumba ninayopanga, pale tuko wanachuo tu kwahiyo tabia hazina tofauti sana. Yeye sasa miezi yake kama minne ya kukaa pale hajawahi kuleta demu, kuongea nae hata kwa simu, kuonesha dalili zozote za kuwa na encounter na mwanamke. Yani wengine tunavusha, usiku tunakaa nje tupunge upepo tuongeale nao, wanatutembelea, ukikaa kidogo unasikia huyu analalamika demu fulani kamfanyaje sijui.

Sasa huyo jamaa yuko busy na wanaume mara wako kwenye photoshoot ya kuvaa suti, mara wamevaa manguo ya kung'aa, nywele katia dawa za kulainisha kama Wahindi. Mimi nina wasiwasi nae na kwa sasa kahamia Sinza kwetu kahama.

Alafu wazazi wanashindwa vipi kuwatambua mbona dalili zinakuwepo. Kuna mmoja nilikuwa naye A level huyo anachonga nyusi na anapaka wanja, ana yale mafuta ya kulainisha na kung'arisha lips. Sasa huyu mzazi wake haoni?

Kuna dogo mwingine O level yeye alikuwa anakaa na wadada pekee. Anajilainisha kwenye kuongea na movements alafu ni "designer" na anapamba mademu wakijiandaa na zile sherehe za shule. Yani asipokuwepo wanalalamika wanaona hawatopendeza wakati dogo mwenyewe alikuwa form 2. Huyu anageuzwa tangu darasa la sita alikosomea uko shule maarufu Mwanza. Sasa wazazi wake hawakuona hobbies za mtoto na lifestyle yake?

Kuna lecturer flani Dodoma nilimsaidia kitu kwenye kuongea nae akanambia nafanana na mwanae. Akanambia ana watoto wanne wote wa kiume, huyo wa mwisho ninaefanana nae walijua ni wa kike wakampa na jina kabla. Akazaliwa wa kiume ila "bahati nzuri lile jina linatumika hata kwa mtoto wa kiume". Alafu akanambia anacheka eti ana tabia chache za kike.

Mzazi unamuita mtoto wa kiume Gift na wahuni wanamuita "Gee"
 
Utasikia wanasema tunaenda na wakati, utandawazi mara ndio fashion ya siku hizi

Wazazi simamieni majukumu yenu ya kimalezi kwa usahihi msije mkalea watoto wasio na maadili
Nakumbuka mmoja wa ma Ex wangu aliwahi kuniambia.... Hata kama atakuwa na mtoto anataka amlee mwenyewe....

Jamii yetu inabidi ikubali kuwa wazazi wote wa pande zote mbili wanajukumu la kulea watoto au mtoto waliompata baada ya uzinifu
 
Back
Top Bottom