Malezi Mabovu..... Kosa la Wazazi au Jamii

VoiceOfReason

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
5,194
1,355
Siku hizi imekuwa ni kawaida kuwalaumu wazazi / mlezi pindi mtoto anapokosa maadili, tukiangalia vizuri hata kama mzazi atakuwa anajua kulea kiasi gani mazingira yanachangia sana kumuharibu mtoto (we dont live in a vaccuum kwahiyo kama hata wako hajaoza wa jirani anaweza changia wako akaoza)

  • Zamani mtoto alikuwa sio wa fulani, ni wa jamii nzima kwahiyo popote anapokosa mtu yoyote alikuwa anamuadhibu (sasa people dont care)
  • Watu wazima wamekosa maadili sio role models (ufisadi mwanzo mwisho hakuna heshima)
  • Hivi serikali imeshindwa kuwachukua hao watoto wa mitaani wote na kuwaweka centre yenye ulinzi mkali ili wasitoroke na kuwapa elimu.... (this is a time bomb hivi hawa watoto ambao hawana elimu) wakija kuwa wakubwa watafanya nini.., hivi hatuoni au upeo wetu ni mfupi....? if you ask me hili ni janga kubwa its a time bomb
Kwahiyo bila kurudi kwenye maadili yetu ya zamani.., kwamba watoto ni wetu wote na sio mtoto wa fulani hiki kizazi na kinachofuata kitakuwa cha watu wa ajabu sana, na kamwe mzazi hawezi kulea mtoto peke yake bila msaada wa jamii....,

"We must learn to live together as brothers or perish together as fools. Martin Luther "

Probably Babu na Baba Zetu ndio walikuwa walezi bora..., We are failing our Kids who will fail theirs, and I dont want to even think two generations from now.... Na hili sio la kwamba fulani kasema.... even though I dont have kids right now, lakini mimi wewe na yule we are all responsible for this.... I CHALLENGE ANYONE TO TELL ME OTHERWISE...
 
Voice wewe acha tu Mtoto wa jamii?? Umpate wapi siku hizi??

Dear jana mie nimechoka wakati narudi kazini naingia getini hivi kuna watoto wa jirani nao walikuwa wanashushwa na school bus sasa kwenda home housegirl katoka sijui kaenda sokoni au wapi sielewi maana wamegonga geti halijafunguliwa dah nilichokisikia toka kwa mtoto yule sikuamini mpaka leo nanukuu " Leo niko na stress zangu na dada ananiongezea" Nilichoka mind you huyo ni mtoto wa nursery school wala si primary kwa mtindo tunaelekea wapi??
 
Voice wewe acha tu Mtoto wa jamii?? Umpate wapi siku hizi??

Dear jana mie nimechoka wakati narudi kazini naingia getini hivi kuna watoto wa jirani nao walikuwa wanashushwa na school bus sasa kwenda home housegirl katoka sijui kaenda sokoni au wapi sielewi maana wamegonga geti halijafunguliwa dah nilichokisikia toka kwa mtoto yule sikuamini mpaka leo nanukuu " Leo niko na stress zangu na dada ananiongezea" Nilichoka mind you huyo ni mtoto wa nursery school wala si primary kwa mtindo tunaelekea wapi??
Kweli kabisa.... hapo kama jamii ingebidi wewe uwaweke sawa..., huyo dada awazabe vibao na mzazi wao akija nae awakemee..., lakini sasa ukimgusa tu mtoto utaambiwa zaa wa kwako... lakini ubaya ni kwamba hata watoto wako hizi tabia za hao watoto zinawa-affect kwa njia moja au nyingine..., hivi kuna njia yoyote ya kuweza kuepuka hili janga au its too late
 
Hakuna mtoto wajamii cku hizi. jamii yenyewe imeingiliwa na akina this no wazazi wanashindwa hata kuwonya watoto wao kwani wamejiengua kwa kushindwa kuwasialiana.

Mzazi kanumba lugha haipandi mtoto mwingereza utawasiiana naye vp?

Jamii imechanganikiwa kwa kifupi, hakuna chorus, kiitikio ziro
 
Hakuna mtoto wajamii cku hizi. jamii yenyewe imeingiliwa na akina this no wazazi wanashindwa hata kuwonya watoto wao kwani wamejiengua kwa kushindwa kuwasialiana.

Mzazi kanumba lugha haipandi mtoto mwingereza utawasiiana naye vp?

Jamii imechanganikiwa kwa kifupi, hakuna chorus, kiitikio ziro

Lakini je unakubaliana na mimi kwamba haya makosa ni yangu mimi, wewe na yeye kwa namna moja au nyingine?
 
kuna siku niliongelea hili jambo hapa ni kama watu wanaamini malezi ya mtoto ni ya mzazi pekee umeshawahi jiuliza muda gani unautumia kwa ajili ya mibangaizo ya maisha.na hawa watoto tunawaachia kina nani tusipokubali wakanywe na kulelewa na hawa tunaowaacha karibu yao.
jamii yetu nayo imejaaa uozo, mkubwa kwa mdogo ni kuomba hekima ya Mungu tu.
 
Kinachosikitisha ni kwamba hapa tulipofika ni vigumu kujirudi sababu hata wazazi wa sasa ndio hao baadhi malezi yao yalikuwa yaleyale ambayo ndio wanatoa sahizi..., kuna jambo moja ambalo nilikuwa najisifia kwamba sisi tunalo na western countries hawana "MAADILI MEMA" lakini sahizi hata hilo hatuna..., kwa kweli sasa sioni kitu cha kujivunia ni uozo mtupu....
 
Nakubaliana na wewe kwamba its a time bomb....hawa watoto tulipaswa tuwajibike kwao wote.....mtoto wa mwenzio ni wa kwako...matokeo ya huu ubinafsi wa kulea/kuelekeza wale walio wetu ni mabaya sana,kwakuwa hao watoto wa mitaani wakiwa wakubwa wataishi na watoto wetu ambao wana elimu na maisha mazuri pengine....wale wa mitaani watakuwa mizigo na taabu kwao....ndo haya mambo ya majambazi,wauaji,jamii iliyojaa frustrations na tension na ndiko wanakotoka watu wasiohofia hata kufa,wanajitoa muhanga as hawaoni thamani ya maisha.....ni jukumu letu sote kubadili hali hii,kwa manufaa yetu na ya kizazi kijacho.....tukishindwa tumeshindwa wote kama jamii na madhara yatakuwa kwetu kama jamii as tunaishi nao.
 
huwezi amini ni majuzi tu nilishuhudia kisa mtoto kaiba pesa kwa jirani jirani akenda kushtaki kwa mzazi badala ya yule mama kushukuru akaingia ndani kwa hasira akalipa ile hela halafu huku nyuma akaanza kumbembeleza mtoto na huyu ni msomi ana uelewa mzuri mtu wa mambo kwa kweli ilinisikitisha embu fikiria kizazi kinachozunguka hawa watoto wetu tunaotaka wawe na maadili mema kitakuwaje kama wazazi wenyewe hatukubali kukemea.

Nakubaliana na wewe kwamba its a time bomb....hawa watoto tulipaswa tuwajibike kwao wote.....mtoto wa mwenzio ni wa kwako...matokeo ya huu ubinafsi wa kulea/kuelekeza wale walio wetu ni mabaya sana,kwakuwa hao watoto wa mitaani wakiwa wakubwa wataishi na watoto wetu ambao wana elimu na maisha mazuri pengine....wale wa mitaani watakuwa mizigo na taabu kwao....ndo haya mambo ya majambazi,wauaji,jamii iliyojaa frustrations na tension na ndiko wanakotoka watu wasiohofia hata kufa,wanajitoa muhanga as hawaoni thamani ya maisha.....ni jukumu letu sote kubadili hali hii,kwa manufaa yetu na ya kizazi kijacho.....tukishindwa tumeshindwa wote kama jamii na madhara yatakuwa kwetu kama jamii as tunaishi nao.
 
Kwa watoto waliochini ya mzazi flani kuharibika ni udhaifu wa huyo mzazi, wazazi wengine wanajifanya kuleta uzungu kwenye malezi kitu ambacho sio kabisa kwa mazingira yetu.(watoto hutofautiana tabia regardless wanasoma shule mmoja).During the holidays watoto wa ndugu husafiri kuja kwetu na kila mmoja anakatabia kake ila siku za kwanza nawacharaza mpaka wanakaa on line.KWA WATOTO WA MITAANI nakiri ni udhaifu wa jamii kwa ujumla kwenye malezi.
 
Kwenye ulimwengu wa leo kumkemea/kanya mtoto wa mwenzio ni kosa zaidi ya alichofanya huyo mtoto!Wale ambao malezi yamewashinda ukifanya hivyo wanaona kama unawakosoa na hawataki!Kwahiyo kosa sio langu wala lako..ni la mzazi asiyetaka mtu mwingine asaidie kumrekebisha mwanae!Binafsi kama sio mtu wa karibu nakaa mbali kwasababu hata nikijaribu najua itanirudia!Worse mtu mwingine anaweza kuona mtoto wake amekosea kweli..ila kwasababu mtu baki ndo amekua wa kwanza kumuonya atareward lile kosa!
 
Kwa watoto waliochini ya mzazi flani kuharibika ni udhaifu wa huyo mzazi, wazazi wengine wanajifanya kuleta uzungu kwenye malezi kitu ambacho sio kabisa kwa mazingira yetu.(watoto hutofautiana tabia regardless wanasoma shule mmoja).During the holidays watoto wa ndugu husafiri kuja kwetu na kila mmoja anakatabia kake ila siku za kwanza nawacharaza mpaka wanakaa on line.KWA WATOTO WA MITAANI nakiri ni udhaifu wa jamii kwa ujumla kwenye malezi.

Je mzazi katika masaa 24 anakaa na mwanae masaa mangapi? kumbuka kuna shule, kucheza n.k. Hata ukiwa mzazi mwenye maadili kiasi gani kama jamii iliyokuzunguka yote imeoza ni rahisi kwa watoto kubeba tabia chafu kutoka nje...., na huwezi ukawa na full control sababu environment inachangia sana kwenye maadili ya mtoto...., kwahiyo mimi huwa sio mwepesi kuwalaumu mzazi mwenye mtoto sometimes mtoto anapotoka hata kama mzazi akiwa safi kiasi gani. Ingebidi kila mtu awe mlezi..., mtoto wako akija kwangu mimi inabidi nimfunze, akiwa shule mwalimu amfunze na tukiwa mitaani tukiona upuuzi inabidi tuukemee bila kuoneana aibu..., Lakini haiko hivyo sababu jamii sasa haikubali mwingine akemee mtoto wa mwingine..., kwahiyo collectively kama jamaa we have failed our children
 
Kwenye ulimwengu wa leo kumkemea/kanya mtoto wa mwenzio ni kosa zaidi ya alichofanya huyo mtoto!Wale ambao malezi yamewashinda ukifanya hivyo wanaona kama unawakosoa na hawataki!Kwahiyo kosa sio langu wala lako..ni la mzazi asiyetaka mtu mwingine asaidie kumrekebisha mwanae!Binafsi kama sio mtu wa karibu nakaa mbali kwasababu hata nikijaribu najua itanirudia!Worse mtu mwingine anaweza kuona mtoto wake amekosea kweli..ila kwasababu mtu baki ndo amekua wa kwanza kumuonya atareward lile kosa!

Kosa ni letu sababu tumeacha hii kasumba iingie bila kufanya chochote wala kukemea....., hata tukiona meli ina tundu na inazama.., ingawa hakuna mtu ambae kazi yake ni kuziba tundu, lakini sababu wote tumekaa tu na kuangalia maji yanaingia..., boti itakapozama wakati tunatapapa..., we will all be the ones to blame, kwamba kwanini hakuna aliyechukua initiave ya kuziba matundu
 
Jamii na mazingira kwa ujumla ndio yana nafasi kubwa ya kumuharibu mtoto kuliko wazazi.
Binafsi nimelelewa na mzazi mmoja na ni mzazi aliyekuwa busy sana. Kutoka asubuhi kurudi usiku, hakuwa hata na muda wa kuangalia madaftari wala kunichunga chunga zaidi ya kuhakikisha nimepata mahitaji yangu muhimu.
Ila mazingira niliyoishi yalikuwa poa na jamii iliyonizunguka haikuwa na tabia za ajabu ajabu.
Nafikiri jamii ingekuwa mbaya ningeharibikiwa.
 
Jamii na mazingira kwa ujumla ndio yana nafasi kubwa ya kumuharibu mtoto kuliko wazazi.
Binafsi nimelelewa na mzazi mmoja na ni mzazi aliyekuwa busy sana. Kutoka asubuhi kurudi usiku, hakuwa hata na muda wa kuangalia madaftari wala kunichunga chunga zaidi ya kuhakikisha nimepata mahitaji yangu muhimu.
Ila mazingira niliyoishi yalikuwa poa na jamii iliyonizunguka haikuwa na tabia za ajabu ajabu.
Nafikiri jamii ingekuwa mbaya ningeharibikiwa.

Kweli kabisa, hatuwezi kumumlaumu mzazi / mlezi pekee

Ingekuwa hivyo basi watoto wengi ambao walikuwa geti kali au wazazi wao ni wachungaji wangekuwa malaika....,

Na je wale ambao watoto wapo boarding school ? mzazi pia alaumiwe...

Kweli Hus ni kwamba nchi yetu imepoteza dira na hatujui tunakokwenda anymore
 
Back
Top Bottom