Malecela na Lowassa - Njia mbili tofauti?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Kama kuna kiongozi katika CCM ambaye kwa haki angeweza kulia na kulalamika mbele ya wananchi na kuandaa waandishi wa habari wamsafishe na kujijenga upya ni Mhe. S. J. Malecela (Mtera - CCM). Mzee Malecela ni moja wa wa viongozi ambao siyo tu wameitumikia Tanzania kwa muda mrefu lakini pia amewahi kushika nafasi nyingi za juu ukiwemo Uweziri wa Mambo ya Nje na juu kabisa ni Uwaziri Mkuu. Kwenye chama alifikia kuwa Makamu wa Mwenyekiti Taifa (Bara) kwa muda mrefu tu.

Hata hivyo mara kadhaa katika njia yake ya kisiasa amejikuta akikutana na kila aina ya magogo na mahandaki ambayo mengine aliweza kuyahamisha lakini mengine alikubali yamemzidi kimo, au kwa hekima akayapa ushindi wa kimkakati.

Mojawapo ya matukio ambayo yanakumbukwa sana na kugongana kwake na Mwalimu Nyerere ambako inadaiwa kulichangia kwa kiasi kikubwa kuvuruga nafasi yake ya kuwa mgombea wa CCM mwaka 1995. Chochote kilichotokea na licha ya uwezo wake wa kumwambia Nyerere ukweli pasipo haya Malecela hakuwahi kusimama na kumshambulia Nyerere au kwa namna yoyote ile kumfanya awe duni mbele ya wananchi. Alikubali kushindwa mbele ya Nyerere lakini aliendelea kulitumikia Taifa lake na wapiga kura wake.

Na hata baadaye tena alipojaribu kupata nafasi ya kumrithi Mkapa na licha ya madai kuwa alimzunguka Mkapa na kutangaza nia yake ya kugombea bado aliamini ana mvuto mkubwa kwa chama. Mvuto huo ambao unadaiwa ni wa kweli na si wa masikhara nusura umpatie ushindi kwenye mchakato wa kutafuta mgombea. NI mpaka pale Mkapa alipofanya kile kinachoitwa "Mizengwe" ndipo jina la Malecela likachomolewa na majina mengine yakapita.

Kitendo cha jina lake kuenguliwa na kunyimwa nafasi ya kuletwa kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa (ambako inadaiwa alikuwa na nguvu sana) siyo tu kilimuumiza lakini kilimkera hasa. Hata hivyo kwa mara nyingine hakusimama hadharani au kwa wapiga kura wake (ambao walimchagua kwa zaidi ya asilimia 90) kuanza kulalamika kuwa "alionewa na hakupewa nafasi ya kusikilizwa". Alikubali na kuendelea na nafasi yake hadi pale alipokuwa tayari kuachia Umakamu na kubakia mbunge wa kawaida. Na kwa hakika baada ya kuzidiwa kete na mtandao, Malecela hakusimama kuanza kuonesha upinzani wa wazi dhidi ya Kikwete. Hadharani mara zote amekuwa akimuonesha heshima ambayo sitashangaa itazawadiwa muda si mrefu.

Ninafahamu, pembeni ambako akiwa na marafiki, ndugu na watu wa karibu ana maneno hasi ambayo anaweza kuyaelezea kuhusu kuenguliwa kwake na matukio ambayo anajua si ya haki. Hata hivyo hajaingia kwenye rekodi kusema mambo hayo na wananchi wakayasikia. Yeye kwa hakika ni kada mzuri wa chama kwa uzuri na kwa ubaya.

Hata hivyo, kwa upande wa Lowassa hilo ni kinyume naye. Matukio yaliyofuatia kujiuzulu kwake yamethibitisha kitu kimoja; Lowassa anaamini kuwa anastahili kuwa kiongozi wa ngazi za juu na ya kuwa hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kumzuia na yuko tayari kufanya lolote lile kujijengea jukwaa la kujisafisha.

Lowassa siyo tu ameamua kujisafisha lakini ni wazi kabisa ameamua kuchallenge siyo tu nguvu ya Rais bali pia chama chake na kwa hakika Bunge la Jamhuri ya Muungano. Kwa mtu mwenye jazba kama Lowassa neno hekima na busara viko mbali naye na hisia za kisasi na kustahili zinamuongoza.

Ni kwa sababu hiyo kabla ya kutumiwa ujumbe hivi juzi, ujumbe uliokuwa loud and clear alikuwa ameaanda mkakati wa "full throttle" wa kuchallenge maamuzi ya Bunge, ukimya wa Rais kumtetea n.k Na zaidi alifikia uamuzi huo baada ya kuamua kutomjulisha Rais kuwa anaenda kujiuzulu hadi pale Rais aliposikia kwenye TV kama Watanzania wengine.

Kitendo chake kile kilikuwa na lengo la kumtangazia Rais Kikwete kuwa "urafiki" wao umefikia kikomo na kwa vile JK hakuweza kumtetea kwenye CCM na kwa vile licha ya JK kukataa kuingilia kati ripoti ya Mwakyembe na kukataa kuiona kabla, ni wazi kuwa EL anaamini kabisa kuwa kuanguka kwake kisiasa kumehusishwa kabisa na maamuzi ya kutofanya lolote ya JK.

Lowassa siyo tu anataka kurudi katika uongozi bali pia anaandaa kisasi; kisasi ambacho kitaonekana zaidi siku zijazo ambapo Rais Kikwete anatarajiwa kufanya mabadiliko makubwa ya wakuu wa mikoa na wilaya akizingatia kile kinachofanyika Kyela kuhusu Mwakyembe.

Siyo hivyo tu, mkakati wa Agenda 21 sasa hivi ni kupitia Bungeni ambapo baadhi ya wajumbe wa Kamati Teule ambao na wenyewe walipata mikopo toka Benki Kuu hata kama ni ya halali kiasi gani wamewekwa kwenye shabaha ambapo na wenyewe watatajwa kuhusika na "ufisadi". Lengo ni "mmetuchafua, tutawachafua". Mbinu hii ya Kibunge itaonekana siyo kwenye kikao kijacho tu bali kile cha bajeti pia ambapo msishangae kuona Kamati Teule inaundwa kuhusu BoT ili iende kunasa wengine.

Hivyo, ni wazi kuwa licha ya wanasiasa hawa wawili kukabiliwa na mitikisiko mikubwa ya kisiasa ambayo imetishia maisha yao ya kisiasa, ni wazi kuwa wameamua kufuata njia mbili tofauti njia ambazo zimemfanya Malecela kuendelea kuwa mzee anayeshimika ndani ya CCM na Lowassa kuwa ishara ya kuangaliwa na jina la kutolewa mfano!

Endapo Lowassa hataweza kukaa chini na kutulia busara na hekima katika kushughulikia mgongano wake na JK ajue kabisa kuwa anajitengenezea mazingira siyo tu ya kukataliwa na wana CCM wenzake bali pia kuonekana mbele ya wananchi kama adui wa Rais. Sidhani kama anataka hilo la pili kwani licha ya matatizo mengi yaliyopo Tanzania watu wengi bado wanamhusudu na kumheshimu Rais Kikwete (licha ya madhaifu yake mengi ya kiuongozi)kama Rais Halali wa Jamhuri yetu.
 
Thanks Mwanakijiji,

Na baada ya kujua haya ndiyo maana nimeamua kuungana na wale wenye lengo la kupambana na Lowasa kwa yale yote anayotaka kuleta Tanzania - ukianza na haya madai ya ukabila - chuki dhidi ya watu wa monduli!
 
Mwanakijiji,

..kama mtu ametuhumiwa hadharani basi ni vizuri akajibu tuhuma hizo hadharani. binafsi sioni tatizo liko wapi hapo.

..wanaotaka kumtetea Lowassa wana uhuru sawa, na wale wanaotaka kumpinga. naamini katika busara za Watanzania kwamba wana uwezo wa kuchambua pumba na mchele.

..sasa kuhusu hilo la harakati za wabunge wa CCM "kuchafuana," huo ni utamaduni wa siku nyingi ndani ya CCM.
 
Kuna somo kubwa la uvumilivu katika siasa lipatikanalo kutoka kwa Mzee malecela, hawa wanasiasa mambo-leo EL and the like wanatakiwa wakachote elimu ile.

Thankx Mwakjj for this good analysis...
 
Masatu,

..unajua haya mambo ya kuvumilia ndiyo yametupatia Uraisi wa Kikwete-Lowassa. fuatilia tangu 1995 utajua kwamba tulikuwa tunachagua Kikwete-Lowassa au Lowassa-Kikwete.

..hawa wawili kwa kweli ndiyo wali-perfect mbinu za kuchafuana ndani ya CCM. kama the likes of Salim Salim,John Malecela, Frederick Sumaye,..wangeachana na hii habari ya "uvumilivu" na kuamua ku-expose mbinu chafu, na wahusika wake wakuu, tusingefika hapa tulipo leo hii.

..binafsi napendekeza kwa wana-CCM na Watanzania kwa ujumla kukataa hizi siasa za kuchafuana. tushindanishe hoja na siyo majungu.
 
issue ya El na mzee Malecela ni tofauti.Mambo ya Mzee Malecela yalikuwa ya siri ndani ya vikao vyao vya CCM.Ndicho hicho hata El alijaribu kuki advocate kwenye utetezi wake-yaani mambo ya richmond wangeyamaliza kisirisiri kama ambavyo huwa wanafanya wakiwa na 'nyeti' ndani ya chama!Kwahiyo Mzee Malecela pamoja na hekima yake,lakini pia ilikuwa rahisi kwake kuwa mvumilivu.Lakini kubwa,EL yeye ana tuhuma za ubadhilifu wa fedha ya uma,tofauti na Mzee Malecela ambaye kukosana kwake na Nyerere kulianza pale aliposhirikiana na G55 kuupitisha muswada wa serikali 3,kitu ambacho kilikuwa rahisi hata baadaye kwa Malecela kuja kusimama na 'kujitakasa' na watu wakakupa support,kama angehitajika kufanya hivyo.El inabidi awe na kazi ya ziada ya kuhakikisha political clout yake inarudi kwa sababu habari zake zimezagaa kiasi kwamba hata watoto wadogo wanafahamu.Kwahiyo ni lazima aanze mapema wakati issue bado iko motomoto,vinginevyo akichelewa ndiyo yatakuwa kama yale ya Sumaye.
Kwahiyo yeye si mjinga,anajua anachofanya!
 
Kuna somo kubwa la uvumilivu katika siasa lipatikanalo kutoka kwa Mzee malecela, hawa wanasiasa mambo-leo EL and the like wanatakiwa wakachote elimu ile.

Thankx Mwakjj for this good analysis...

This is in no way on defense of Lowassa.

Kuna uvumilivu na woga, na tofauti ni kubwa sana. Mtu ye yote ambaye ni principled anaweza kuwa mvumilivu lakini siyo mwoga.

Mwoga hana principles. Kwa anayeona kuwa Malecela ni mvumilivu itabidi atushawishi kama yuko principled na si mwoga.

Malecela ni mfano wa viongozi/wanasiasa wengi wa 60s wenye mtazamo wa 'funika kombe mwanaharamu apite', na kwao uongozi ni zawadi. Atakubali hata uenyekiti wa kitongoji maadamu aambiwe tu 'kateuliwa' na Rais.

Give me Lowassa, Sokoine, Mwakyembe, Kasaka, Zitto, Slaa anytime of the day kuliko akina Malecela, Kingunge, Mzindakaya, Mungai, Mwandosya, Mudhihir, and the like hata wawe wavumilivu vipi.

Malecela angewavimbia Nyerere na Mwinyi may be ingetuepusha na IPTL/ANBEM/Kiwira/EPA. Malecela angemvimbia Mkapa may be ingetuepusha na Kikwete_usanii.com/Richmonduli/Buzwagi na more EPA.

Funika kombe mwanaharamu apite wakati watoto wetu watajutia for the next 50 years.

Please Mwanakijiji, you are better than that.

Acha Lowassa amvimbie Kikwete, may be something will happen...
 
This is in no way on defense of Lowassa.

Kuna uvumilivu na woga, na tofauti ni kubwa sana. Mtu ye yote ambaye ni principled anaweza kuwa mvumilivu lakini siyo mwoga.

Mwoga hana principles. Kwa anayeona kuwa Malecela ni mvumilivu itabidi atushawishi kama yuko principled na si mwoga.

Malecela ni mfano wa viongozi/wanasiasa wengi wa 60s wenye mtazamo wa 'funika kombe mwanaharamu apite', na kwao uongozi ni zawadi. Atakubali hata uenyekiti wa kitongoji maadamu aambiwe tu 'kateuliwa' na Rais.

Give me Lowassa, Sokoine, Mwakyembe, Kasaka, Zitto, Slaa anytime of the day kuliko akina Malecela, Kingunge, Mzindakaya, Mungai, Mwandosya, Mudhihir, and the like hata wawe wavumilivu vipi.

Malecela angewavimbia Nyerere na Mwinyi may be ingetuepusha na IPTL/ANBEM/Kiwira/EPA. Malecela angemvimbia Mkapa may be ingetuepusha na Kikwete_usanii.com/Richmonduli/Buzwagi na more EPA.

Funika kombe mwanaharamu apite wakati watoto wetu watajutia for the next 50 years.

Please Mwanakijiji, you are better than that.

Acha Lowassa amvimbie Kikwete, may be something will happen...


Kiungani,

Labda ungetuwekea wazi una maana gani unaposema "angevimba" kama ni kuwa kung'ang'anizi hebu turudi nyuma tujikumbushe kidogo.

1995 Scenario

Hapa kamanda alikuwa Mwalimu mwenyewe na ali lisimamia jambo hili kwenye vikao vya chama hususan NEC ikawa ama Malecela apite au Mwalimu asuse! the answer is/was obvious....
swali: kuvimba gani ambapo Malecela kungemsaidia hapa? ung'ang'anizi wa aina yeyote ungemwacha na choice 2 tu ama watangaze wamekata jina lake au aseme mwenyewe kuwa kajitoa, rejea yaliyomkuta Dr Gharib Bilali pale white house 2005 alipong'ang'ania kugombea urais dhidi ya Amani. Choice ya tatu ambayo angechukua ingemmaliza kabisa kisiasa ni kwenda upinzani sina haja ya kulieleza hilo ni self explanatory.


2005 scenario.

Malecela kakatwa kwenye CC kamati kabla hata kufika NEC, kama ilivyokuwa 1995. Ikumbukwe kuwa CC hawapigi kura pale kuna kitu kinaitwa "vigezo" au kwa jina rahisi "mizengwe" wanakwambia tu jina lako halijapitishwa.

Baada ya kukatwa Malecela "akavimba" kama ulivyo suggest na aka appeal kwenye NEC. Mzindakaya alisimama kidete kudai iweje mtu aliekuwa waziri mkuu na makamu wa Mwenyekiti jina lake likatwe kimizengwe? this time around Mkapa akasimama kidete kummaliza kuna hadithi ndefu hapa kidogo let make it short.

Je Kiungani kwa mujibu wa scenario hizo juu unadhani "kuvimba" kwa aina gani kungemsaidia Malecela?

Tunapozungumzia uvumilivu tuna maana baada ya yote hayo wala mzee hakususa wala kupayuka kwenye vyombo vya habari eti "hajapewa nafasi ya kusikilizwa" bali alishiriki kikamilifu kwenye kampeni

Kwenye siasa mkuu kuna wakati unawekwa kwenye kona unatulia mwenyewe. Waulize wahanga wa "kuvimba" Seif, Komando, Mrema, Kasaka, Guninita etc
 
Wait a minute; JokaKuu ana hoja sana.

Kadri ninavyofuatilia huu mjadala sipati picha hasa kinachogomba ni kipi. Kwa mfano kuna watu wanaopinga Lowasa asihoji maamuzi ya bunge nje ya bunge, tena hapa wapo hata wanasheria ambao kwa muda mrefu tunafikiri wamebobea katika hii nyanja. Lakini hapa tuna-display unafiki wa hali ya juu. Ni juzi tu hapa tulikemea kwa nguvu zetu zote kitendo cha bunge kukemea watu kuhoji uamuzi wake wa kumfungia Zitto. Tena kila aina ya mwanasheria katika ile nchi akamtetea Zitto na wale waliokuwa wanalisema bunge. Na tukahitimisha kwamba, tena kwa hapa JF chini ya uongozi wa MKJJ, kwamba bunge lilikuwa linajaribu kuziba uhuru wa watu wa kutoa maoni yao. Sasa nauliza, huyu Lowasa pamoja na matatizo yaliyompata hana uhuru wa kutoa maoni, kilio, na dukuduku zake popote pale iwe ni ndani na nje ya bunge? Inawezekana tusipende yale anayoyasema Lowasa, lakini kamwe hatuna haki ya kujaribu kumnyamazishe asiseme, nami naseme wale wote wanaotaka kumnyamazisha Lowasa asitumie uhuru wake walegee kwa jina la JF.

Msingi wa demokrasia ni kukubaliana kutokubaliana. Sasa kama kuna watu wameamua kumtetea Lowasa wasionekane wanafiki au wasaliti. Huu mtindo wa kuwekea lable ndio unaotufanya watanzania tuwe makondooo kwa sababu kuna watu wanaogopa kutoa maoni kwa kuogopa kuonekana wanafiki au wasaliti au sio wazalendo. Tuwe huru kutetea hoja zetu bila kuitana majina, hii ndio maana ya ustaraabu.
 
Wait a minute; JokaKuu ana hoja sana.

Kadri ninavyofuatilia huu mjadala sipati picha hasa kinachogomba ni kipi. Kwa mfano kuna watu wanaopinga Lowasa asihoji maamuzi ya bunge nje ya bunge, tena hapa wapo hata wanasheria ambao kwa muda mrefu tunafikiri wamebobea katika hii nyanja. Lakini hapa tuna-display unafiki wa hali ya juu. Ni juzi tu hapa tulikemea kwa nguvu zetu zote kitendo cha bunge kukemea watu kuhoji uamuzi wake wa kumfungia Zitto. Tena kila aina ya mwanasheria katika ile nchi akamtetea Zitto na wale waliokuwa wanalisema bunge. Na tukahitimisha kwamba, tena kwa hapa JF chini ya uongozi wa MKJJ, kwamba bunge lilikuwa linajaribu kuziba uhuru wa watu wa kutoa maoni yao. Sasa nauliza, huyu Lowasa pamoja na matatizo yaliyompata hana uhuru wa kutoa maoni, kilio, na dukuduku zake popote pale iwe ni ndani na nje ya bunge? Inawezekana tusipende yale anayoyasema Lowasa, lakini kamwe hatuna haki ya kujaribu kumnyamazishe asiseme, nami naseme wale wote wanaotaka kumnyamazisha Lowasa asitumie uhuru wake walegee kwa jina la JF.

Msingi wa demokrasia ni kukubaliana kutokubaliana. Sasa kama kuna watu wameamua kumtetea Lowasa wasionekane wanafiki au wasaliti. Huu mtindo wa kuwekea lable ndio unaotufanya watanzania tuwe makondooo kwa sababu kuna watu wanaogopa kutoa maoni kwa kuogopa kuonekana wanafiki au wasaliti au sio wazalendo. Tuwe huru kutetea hoja zetu bila kuitana majina, hii ndio maana ya ustaraabu.

Na hii ndio demokrasia, uhuru wa maoni. Lakini hofu ya wengi ni matumizi mabaya ya networks ambazo mtu kama Lowassa anazo, ambayo yanaweza kutumika kupindisha ukweli ili mwishowe mkosa aonekane ndiye shujaa, na wale tuliowaona mashujaa wapewe label ya uhaini! Ileile ya label, tunaziogopa(zikiwa mbaya) na tunazipenda pia (zikiwa nzuri). Kitu kinachotufanya tuwe on the alert Lowassa anapoongea ni yale anayoyasema, jinsi anavyoyasema, mazingira anakoyasemea na kile kinachoonekana kwa wengi kama lengo ovu nyuma ya jitihada hizo za kujitakasa. Kila mtu atoe maoni yake bila kuogopa label, lakini mtu akitoa utetezi wa kipotoshaji ajibiwe na ikiwezekana hatua zaidi ya hapo ichukuliwe.
 
Sasa nauliza, huyu Lowasa pamoja na matatizo yaliyompata hana uhuru wa kutoa maoni, kilio, na dukuduku zake popote pale iwe ni ndani na nje ya bunge?


Mkuu wangu Kitila,

Heshima mbele, Lowassa ana haki zote za kudai haki zake, lakini aende kuzidai at the right place, na at the right time, kwanza angeanza na bungeni ambako angeweza kuanzisha mjadala mzito sana kuhusiana na fate yake, pili angekwenda NEC na kutoa malalamiko yake, halafu angeenda cc, sasa huko kote wasingemsikiliza basi a ngeingia mahakamani, ndipo angefanya anayoyafanya sasa,

Tatizo la anayoyafanya sasa ni kwamba anaitumia siasa kushindana na bunge na sheria, matokeo ni kuleta mgawanyiko kwa jamii, we do not need what he is doing now, taifa lingenuifaika sana kama angeenda kwenye sheria, angalau ingetupatia respect kwa the rule of law, au politically anayoyafanya sasa angeyafanya akiwa upinzani, then angetusaidia taifa sana, kwa sababu Kitila ndugu yangu the big picture the man analilia tumbo lake, sio taifa jaribu kuangalia vizuri kilio chake na wenziwe,

Mambo ya kina malecela kunyamaza ni mambo ya ccm sio ya taifa, yeye aliumizwa ndani ya ccm, we should not care a bit about ccm na mambo yao ya ndani, lakini Lowassa ameumizwa na taifa kupitia bunge na sheria, sasa kwa nini asiende kwenye sheria au kwa nini hakusimama kidete bungeni na hao marafiki zake? Hakuna anyemkataza kupiga kelele za haki, lakini ni lazima aambiwe kuwa anzipigia kwenye the wrong place, angezipigia kwenye sheria na wenziwe wakamsaidia huko mimi ningemsifia sana,

kesi ya Zitto na hii ya Lowassa, hazifafanani kabisaaaa kisheria, Zitto alipigiwa kura za wabunge kumsimamisha bunge, Lowassa alikimbia ripoti ya kamati ya bunge kabla ya kupigiwa kura na bunge, sasa unazilinganishaje hizi mkuu? Kwa kweli ni waste of our valid national's time kujadili hii ishu ya Lowassa, kwa sababu in the end inatusaidia kutugawa as jamii, maana sasa hata hapa JF tumfikia hatua ya kuanza kuvutana mashati na hata kudai eti ni ishu ya haki ya Lowassa, give me a break! haki inapatikana kwa kulikimbia bunge na kwenda kuwalaghai wananchi wa Monduli? Haki ameshindwa kusimamia ndani ya bunge ataipata kwenye magazeti yetu uchwara?

Please do not get me started....!
 
WaTanzania wote SI wabunge,ila wabunge wote NI waTanzania.Pia wabunge wote SI Mawaziri wakuu ila Waziri mkuu NI mbunge.Kwa hiyo jinsi ya kulalamika kwa mbunge na aliyekuwa Waziri mkuu ni vitu 2 tofauti sana.Kuna sheria zinazowazuia na kuwatofautisha.Unafikiri ulinzi anaopewa PM hata kama akistaafu ni kwa ajili ya roho yake???

Kwa hiyo Lowassa anatakiwa aelewe nafasi aliyokuwa amefikia na miiko ya nafasi hiyo katika jamii.Anavyobwabwaja anaonyesha jinsi gani alivyo na ustaarabu wa kukopa.Naamini angekuwa ni yeye ndo amechafuliwa kama alivyomshafua Salim wakati wa Kampeni 2005 basi leo tusingekuwa tunaongea hivi.Lazima angevaa Sime yake kuzunguka mtaani kutafuta wabaya wake.

Malechela kwa hili huwezi kumlinganisha na bwana mdogo Lowassa.Kwa kweli Malechela alionyesha na anaonyesha ukomavu wake KISIASA.Lowassa nakushauli uende ukale tuition ya bule kule mtera ila vizia mama kilango akiwa hayupo,vinginevyo atakutimua kama utaenda na pumba zako hizo.Hongera Malechela na Lowassa una kazi.Ziiiiiiii
 
ndugu zangu,

..kuna hali ya kuamini kwamba Bunge liko juu ya wananchi. Bunge ni mali ya wananchi--viongozi na wasio viongozi.

..si makosa kuzungumzia uamuzi wowote ule wa Bunge, au kupingana nao mitaani. leo hii tukimzuia Lowassa kufanya hivyo, kesho yanaweza kumkuta mwananchi wa kawaida.

..Lowassa analalamika wakati Bunge limeshafanya uamuzi wa kupitisha Ripoti ya Mwakyembe. Hii si sawa na kuzungumzia suala lililoko mbele ya Mahakama. Lowassa alieleza kinyongo chake ndani ya Bunge, ana haki ya kueleza kinyongo chake nje ya Bunge.

..Hii si mara ya kwanza uamuzi wa Bunge kupingwa nje ya vikao vya Bunge. Sote tunakumbuka jinsi Baba wa Taifa alivyopinga Azimio la kuundwa kwa serikali ya Tanganyika. Tena aliandika mpaka Utenzi, na kitabu. Je, alikuwa akifanya makosa? sidhani.

..pia naomba tuelewane hapa kwamba yanayotokea ndani ya vyama vya siasa yanatuhusu Watanzania wote. Vyama vya siasa vinapokea mabilioni ya ruzuku kutokana na kodi yetu wananchi.

..Yaliyomtokea Malecela ndani ya vikao vya CCM yanalihusu Taifa zima. Suala lililokuwa mbele ya vikao vya CCM lilikuwa uteuzi wa mgombea Uraisi wa Tanzania. Maamuzi ya vikao vile yana athari kwa Taifa. Yanatuhusu Watanzania wote.

..Naamini katika busara ya Watanzania ktk ujumla wetu. We can be fooled for sometime but not all the time. Sina wasiwasi na wananchi wa Monduli kwamba at the end of the day watang'amua kwamba Lowassa.
 
Quote: Spika Sitta


Spika wa Bunge, Bw. Samuel Sitta, juzi alikaririwa kwenye vyombo vya habari kusikitishwa na baadhi ya watu waliotajwa kwenye Kamati ya Bunge iliyochunguza sakata hilo, kuendelea kujisafisha kwenye vyombo vya habari na kuipakazia kamati hiyo.

Bw. Sitta alikaririwa akisema hatua ya kujibu maamuzi yaliyofikiwa na chombo halali kilichoundwa na Bunge ni kinyume na sheria.

Alikaririwa akisema kuwa ni kinyume cha sheria kwa mtu yeyote ambaye anaona hakutendewa haki na maamuzi ya Bunge au kamati zake, kulalamika nje ya Bunge.

Alifafanua kuwa Mbunge anapaswa kulalamika ndani ya Bunge na mwananchi mwingine anatakiwa kuiandikia Kamati ya Bunge kulalamika.

Alisema hayo ni kwa mujibu wa Sheria Haki, Mamlaka na Madaraka ya Bunge namba 3 ya mwaka 1988.

Mkuu Joka,

Heshima mbele, nafikiri haya maneno ya Spika ni mazito sana mkuu on this ishu.
 
ndugu zangu,

..kuna hali ya kuamini kwamba Bunge liko juu ya wananchi. Bunge ni mali ya wananchi--viongozi na wasio viongozi.

..si makosa kuzungumzia uamuzi wowote ule wa Bunge, au kupingana nao mitaani. leo hii tukimzuia Lowassa kufanya hivyo, kesho yanaweza kumkuta mwananchi wa kawaida.

..Lowassa analalamika wakati Bunge limeshafanya uamuzi wa kupitisha Ripoti ya Mwakyembe. Hii si sawa na kuzungumzia suala lililoko mbele ya Mahakama. Lowassa alieleza kinyongo chake ndani ya Bunge, ana haki ya kueleza kinyongo chake nje ya Bunge.

..Hii si mara ya kwanza uamuzi wa Bunge kupingwa nje ya vikao vya Bunge. Sote tunakumbuka jinsi Baba wa Taifa alivyopinga Azimio la kuundwa kwa serikali ya Tanganyika. Tena aliandika mpaka Utenzi, na kitabu. Je, alikuwa akifanya makosa? sidhani.

..pia naomba tuelewane hapa kwamba yanayotokea ndani ya vyama vya siasa yanatuhusu Watanzania wote. Vyama vya siasa vinapokea mabilioni ya ruzuku kutokana na kodi yetu wananchi.

..Yaliyomtokea Malecela ndani ya vikao vya CCM yanalihusu Taifa zima. Suala lililokuwa mbele ya vikao vya CCM lilikuwa uteuzi wa mgombea Uraisi wa Tanzania. Maamuzi ya vikao vile yana athari kwa Taifa. Yanatuhusu Watanzania wote.

..Naamini katika busara ya Watanzania ktk ujumla wetu. We can be fooled for sometime but not all the time. Sina wasiwasi na wananchi wa Monduli kwamba at the end of the day watang'amua kwamba Lowassa.


.....Kwamba EL ni mw*z* na j*mb*z*. (F*SAD*)
 
Wait a minute; JokaKuu ana hoja sana.

Kadri ninavyofuatilia huu mjadala sipati picha hasa kinachogomba ni kipi. Kwa mfano kuna watu wanaopinga Lowasa asihoji maamuzi ya bunge nje ya bunge, tena hapa wapo hata wanasheria ambao kwa muda mrefu tunafikiri wamebobea katika hii nyanja. Lakini hapa tuna-display unafiki wa hali ya juu. Ni juzi tu hapa tulikemea kwa nguvu zetu zote kitendo cha bunge kukemea watu kuhoji uamuzi wake wa kumfungia Zitto. Tena kila aina ya mwanasheria katika ile nchi akamtetea Zitto na wale waliokuwa wanalisema bunge. Na tukahitimisha kwamba, tena kwa hapa JF chini ya uongozi wa MKJJ, kwamba bunge lilikuwa linajaribu kuziba uhuru wa watu wa kutoa maoni yao. Sasa nauliza, huyu Lowasa pamoja na matatizo yaliyompata hana uhuru wa kutoa maoni, kilio, na dukuduku zake popote pale iwe ni ndani na nje ya bunge? Inawezekana tusipende yale anayoyasema Lowasa, lakini kamwe hatuna haki ya kujaribu kumnyamazishe asiseme, nami naseme wale wote wanaotaka kumnyamazisha Lowasa asitumie uhuru wake walegee kwa jina la JF.

Msingi wa demokrasia ni kukubaliana kutokubaliana. Sasa kama kuna watu wameamua kumtetea Lowasa wasionekane wanafiki au wasaliti. Huu mtindo wa kuwekea lable ndio unaotufanya watanzania tuwe makondooo kwa sababu kuna watu wanaogopa kutoa maoni kwa kuogopa kuonekana wanafiki au wasaliti au sio wazalendo. Tuwe huru kutetea hoja zetu bila kuitana majina, hii ndio maana ya ustaraabu.

Kitila,
Tatizo sio kumziba mdomo Lowasa asizungumze nje ya Bunge. Tatizo hapa ni kujisafisha yeye binafsi kwa gharama ya kamati na kulishushia hadhi Bunge. Kwenda kuwaambia watu nje ya Bunge kuwa kamati ya Mwakyembe haikumtendea haki kwa kutojumlisha ushahidi wake wa barua ni uongo na dhihaka dhidi ya Bunge: kwa babu kuu moja barua anayoizungumzia aliitoa kwa spika tarehe 28/01/2008 wakati ripoti ya Mwakyembe ilikabidhiwa kwa spika tarehe 31/12/2007. Hivyo basi kama tunakubaliana kumpa uhuru Lowasa wa kueneza propaganda za kisanii kwa jinsi hii na kwa kisingizio cha demokrasia, basi naamini kabisa demokrasia kwa maana hiyo hapo juu haina maana.
 
Quote: Spika Sitta




Mkuu Joka,

Heshima mbele, nafikiri haya maneno ya Spika ni mazito sana mkuu on this ishu.

Haya maneno Sita amekuwa akiyasema kila wakati watu wakihoji maamuzi ya bunge, hajaanza leo. Alisema wakati wa Malima, akasema wakati wa Zitto, sasa sioni kwa nini yawe ni maneno mazito kwa sasa na wakati tuliyaona kuwa ni mepesi huko nyuma. I hate what Lowasa is saying but I will defend his right to say it (nimetumia maneno ya mtu fulani, simkumbuki!). Freedom of expression is the cardinal principle of democracy. Sasa hatuwezi tukawa tunataka uhuru wa kujieleza kwa yale tunayotaka kuyasikia tu. Mtikila amekuwa akiropoka mambo kibao miaka yote, lakini tume-defend haki yake ya kuropoka. Lazima tu-defend haki ya Lowasa ya kuropoka. Tumjibu kwa hoja katika yale anayoyasema lakini asizuiwe kuyasema,tukimzuia sisi ndio tutakuwa dhaifu na siyo yeye. Hata hao wananchi wa Monduli hawataacha kutompenda Lowasa kwa kuzuiwa kuongea, wataacha kumfuata kwa kusikiliza hoja za upande mwingine zikitolewa. So far hakuna mtu yeyote, nje na na hapa katika JF, aliyekwishatoa sababu za msingi kwa nini kamati ya Mwakyembe haikumhoji Lowasa. Hii hoja ni muhimu ikajibiwa once and for all. Vitisho havitasaidia kutupa ukweli wa mambo.
 
Mkuu Kitila,

Unayo strong argument, wasi wasi wetu na anayoyafanya Lowassa, ni kwamba anafikia mahali anatugawa as a nation maana sasa tunaanza kusikia hoja za ukabila, Lowassa alikuwa amefikia nafasi nzito sana kitaifa, kwa anavyobubujika toka ajiuzulu anaonekana kuwa hakujua hilo,

Kwamba nafasi aliyoifikia ni kubwa mno na influence aliyonayo kisiasa anaweza kutugawa akiendelea na hicho kilio chake, aende mahakamani, mbona hata Mtikila huenda huko kwenye sheria?
 
Quote: Lusekelo

I think Mr Ole Naiko is trying do some 'ndogo ndogo' for Ted Lowassa. Read it as a campaign to rehabilitate Ted. Mr Ole Naiko implies that Ted Lowassa is equal to all Maasai! Touch Ted and the entire Maasai ethnic group is vilified? Frankly, that is a load of rubbish! Rubbish and dangerous thinking.


Wananchi wengi wameshaanza kushitukia hizi kampeni za kujisafisha na kutugawa in the process!
 
Back
Top Bottom