Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 48,851
- 18,951
[LEFT Malecela: Msinigombanishe na Serikali
Na Kulwa Mzee, Dodoma
MBUNGE wa Mtera, Bw. John Malecela (CCM), amewasilisha
hoja binafsi bungeni huku akivijia juu baadhi ya vyombo
vya habari kwa kutoa habari zenye lengo la kumgombanisha
na Serikali.
Akitoa hoja hiyo jana bungeni, alisema upotoshaji huo ni wa
kitoto na usio na nia njema kwa nchi.
Bw. Malecela alisema alipoomba taarifa ya Kamati ya Rais ya Kuishauri Serikali kuhusu madini ijadiliwe na wabunge, alikuwa na nia nzuri na kwamba madai ya baadhi vya vyombo vya habari kuandika kuwa anaitega Serikali ni ya kichochezi.
Huu ni upotoshaji mkubwa wa nia nzuri niliyokuwa nayo ya
kuliwezesha Bunge kuijadili taarifa hiyo kwa kina, ili
Taifa lipate sera na sheria ya madini bora, alisema.
Mbunge huyo alisema Rais Jakaya Kiwete aliunda kamati
hiyo kwa nia njema ya kuitafutia sekta ya madini ufumbuzi wa kudumu wa matatizo mbalimbali ya kisera na kisheria iliyonayo.
Alisema uundaji huo wa kamati ya madini ni sehemu ya
utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ambayo inatamka kuwa Serikali ya CCM itapitia upya sera ya madini kwa lengo la kuiboresha katika maeneo mbalimbali.
Alisema uamuzi aliotoa Naibu Spika, Bibi Anne Makinda wa kulipa suala hilo muda maalumu kulijadili ni mzuri na wenye
tija kwa Taifa.
"Tafsiri kwamba hatua hii ni mtego kwa Serikali ni porojo,
na upotoshaji wa kitoto usio na nia njema kwa nchi yetu,
niliona niutolee maelezo mbele ya Bunge hili Tukufu, alisema Bw. Malecela.
Tuma
Na Kulwa Mzee, Dodoma
MBUNGE wa Mtera, Bw. John Malecela (CCM), amewasilisha
hoja binafsi bungeni huku akivijia juu baadhi ya vyombo
vya habari kwa kutoa habari zenye lengo la kumgombanisha
na Serikali.
Akitoa hoja hiyo jana bungeni, alisema upotoshaji huo ni wa
kitoto na usio na nia njema kwa nchi.
Bw. Malecela alisema alipoomba taarifa ya Kamati ya Rais ya Kuishauri Serikali kuhusu madini ijadiliwe na wabunge, alikuwa na nia nzuri na kwamba madai ya baadhi vya vyombo vya habari kuandika kuwa anaitega Serikali ni ya kichochezi.
Huu ni upotoshaji mkubwa wa nia nzuri niliyokuwa nayo ya
kuliwezesha Bunge kuijadili taarifa hiyo kwa kina, ili
Taifa lipate sera na sheria ya madini bora, alisema.
Mbunge huyo alisema Rais Jakaya Kiwete aliunda kamati
hiyo kwa nia njema ya kuitafutia sekta ya madini ufumbuzi wa kudumu wa matatizo mbalimbali ya kisera na kisheria iliyonayo.
Alisema uundaji huo wa kamati ya madini ni sehemu ya
utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ambayo inatamka kuwa Serikali ya CCM itapitia upya sera ya madini kwa lengo la kuiboresha katika maeneo mbalimbali.
Alisema uamuzi aliotoa Naibu Spika, Bibi Anne Makinda wa kulipa suala hilo muda maalumu kulijadili ni mzuri na wenye
tija kwa Taifa.
"Tafsiri kwamba hatua hii ni mtego kwa Serikali ni porojo,
na upotoshaji wa kitoto usio na nia njema kwa nchi yetu,
niliona niutolee maelezo mbele ya Bunge hili Tukufu, alisema Bw. Malecela.
Tuma